masai dada na wengine, nawatakieni heri na mafanikio tele katika mwaka huu mpya.
Nafikiri tatizo linaanzia kwenye tamaduni hasa zile zenye mlengo wa kiume (patrilineal) ambazo kwa sehemu kubwa watoto (na mali) ni wa baba(ukoo wa mwanaume). Katika tamaduni za namna hii, ni WAJIBU wa baba au ukoo wa baba kulea "watoto" wao katika ukoo (waliozaliwa ndani ya ndoa na hata wa nje).
Kwa hivyo, ukiona mwanamke kaachiwa kulea watoto, basi ujue huyo mwanaume au ukoo wake umeshindwa kutimiza wajibu wao. Utaratibu huu wa patrilineal (kama ukifanya kazi vizuri) unazo faida zake (kubwa ni uhakika wa malezi ya watoto wa ukoo huo). Infact, kama mwanamke amefiwa na mumewe, basi anaweza patiwa mrithi katika ukoo huo (ndugu wa kiume wa marehemu - hili najua lina magumu yake katika mazingira ya sasa), au kama hataki kurithiwa bado anaweza kubaki katika ukoo husika (provided haulewi na mwanaume wa ukoo mwingine) akisaidiwa na wanaukoo kulea watoto au kama anaamua kuolewa nje ya ukoo, basi hulazimika kuhama katika nyumba na kuachia mali za ukoo (ikiwemo watoto) kwa wanaukoo.
Kwa hivyo unaweza kuona katika utaratibu huu, huwezi kuta mwanamke analea watoto peke yake au mwanaume kulea watoto wa ukoo mwingine(watakushangaa!). Katika utaratibu huu kama mwanaume amezaa na mwanamke na kwa sababu moja ama nyingine hawakuoana basi ukoo wa mwanaume unao wajibu wa kuwakomboa (kuna faini inalipwa kwa "kuingia bila hodi" au "kufanya uharibifu" ) watoto hao (wakifikia umri wa kuweza kutenganishwa na mama-aghalabu miaka 3 hivi). Mkishindwa kuwakomboa mara nyingi watoto hao hubakia katika ukoo wa mwanake (kulelewa na babu au wajomba) na kuchukua majina ya ukoo huo ("ujombani"). Hata ikitokea kuachana bado watoto wanabaki kwa baba au ukoo wa baba (ni "haki" na wajibu wao).
Matatizo yanayotokea sasa (Hilo la mwanamke kuachwa wa watoto, na hivyo kupelekea mwanaume mwingine kumkuta nao) ni matokeo ya tamaduni hizi kupungua (kutozingatiwa, kufuata baadhi ya misingi na kuacha mingine), mchanganyiko katika kuoana watu wa tamaduni tofauti (intermarriages) - matrileneal na patrilineal etc., kuiga tamaduni zingine bila kuwa na mifumo ya kijamii inayo support tamaduni hizo nk. Watoto wa mitaani (na hata hawa "panya road" and the likes) wa ni mojawapo ya viashiria vya kuporomoka kwa tamaduni zetu (ambazo zilikuwa zinaprovide some form of life insurance kwa watoto na hata wajane) na kushindwa kwa tamaduni mpya na kuna masuala ya kiuchumi pia. Bila ya shaka, kuna mengi ya ku debate katika hili.