dazu
JF-Expert Member
- Feb 26, 2011
- 365
- 76
Unapotokea msiba, tunalia sana. Hasa ndugu na jamaa wa karibu. Uchunguzi usio rasmi umeonesha kwamba, kila mmoja hulia kwa sababu tofauti na ni wachache sana ambao wanalia kwa mapenzi ya dhati waliyonayo kwa marehemu (wanaulilia utu wake). Wengi wanajililia wenyewe kwamba misaada au faida mbalimbali ambazo wamekua wanazipata kutoka kwa marehemu hawatazipata tena. Mfano, leo kuna taarifa kwamba 'babu' wa Loliondo amepata msiba. Huku kwetu taarifa hizo zilipotoshwa kwamba 'babu' amefariki. Watu wamesikitika na wengine kulia sana. Nimejiuliza; wanamlilia 'babu' au wanaililia dawa yake? ....Unapolia msibani, unamlilia marehemu au unalilia faida utakazozikosa kutokana na kifo chake? Tutafakari waungwana.