Vituka
JF-Expert Member
- Nov 9, 2011
- 2,257
- 1,247
Naombeni ushauri wana jammii. Nimeishi na mwanaume wa kikurya kwa miaka saba sasa na tuna mtoto mmoa. Familia ya mwanaume huyu ni ya ajabu sijawahi kuona!Ndugu na wazazi wake ni watu wa ajabu kiasi kwamba nashindwa kuelezea!Kilichonisikitisha ni kitendo cha kuzuia harusi iliyokuwa ifanyike mwisho wa mwaka huu, sababu eti kwanza mie msomi, pili kijana wao akinioa (sio mkurya mwenzie) basi wao watampoteza mtoto wao na hawatapata tena msaada toka kwake. Jamani hebi nipeni mawazo yenu, nifanyeje?