Ileje
JF-Expert Member
- Dec 20, 2011
- 8,821
- 12,274
Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar ilichangia gharama za kuendesha serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa miaka mitatu tu tangu 1965 - 1967 kwa asilimia kati ya 5 - 11.
Kwa mantiki hiyo Zanzibar inabebwa na Muungano! Hivyo gharama za mambo ya nje, jeshi, polisi, usalama wa taifa nk zinabebwa na Watanganyika.
Hivyo vyombo vyote hivyo ni mali ya Watanganyika! Zanzibar hawana chao!
Kwa muktadha huo endapo tutaunda serikali tatu, ni serikali ya Tanganyika itakayoumia. Au kwa maneno mengine ni Kodi za Watanganyika zitakazotumika.
Endapo muungano utavunjika rasilimali zote za jeshi, polisi, usalama wa taifa nk itabidi zirudishwe Tanganyika. Zanzibar itabaki bila jeshi, polisi wala usalama wa taifa nk. Usalama wa taifa la Zanzibar utakuwa mashakani.
Ni vema Wazanzibari wakaanza kujitafakari hivi sasa! Kuna hatari kubwa ipo mbele yao!
Zanzibar tafakari kabla hamjaamua! Heri kinga kuliko tiba!
Kwa mantiki hiyo Zanzibar inabebwa na Muungano! Hivyo gharama za mambo ya nje, jeshi, polisi, usalama wa taifa nk zinabebwa na Watanganyika.
Hivyo vyombo vyote hivyo ni mali ya Watanganyika! Zanzibar hawana chao!
Kwa muktadha huo endapo tutaunda serikali tatu, ni serikali ya Tanganyika itakayoumia. Au kwa maneno mengine ni Kodi za Watanganyika zitakazotumika.
Endapo muungano utavunjika rasilimali zote za jeshi, polisi, usalama wa taifa nk itabidi zirudishwe Tanganyika. Zanzibar itabaki bila jeshi, polisi wala usalama wa taifa nk. Usalama wa taifa la Zanzibar utakuwa mashakani.
Ni vema Wazanzibari wakaanza kujitafakari hivi sasa! Kuna hatari kubwa ipo mbele yao!
Zanzibar tafakari kabla hamjaamua! Heri kinga kuliko tiba!