Kwa miaka 47 kati ya 50 ya muungano, Zanzibar haijachangia fedha

Ileje

JF-Expert Member
Dec 20, 2011
8,821
12,274
Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar ilichangia gharama za kuendesha serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa miaka mitatu tu tangu 1965 - 1967 kwa asilimia kati ya 5 - 11.

Kwa mantiki hiyo Zanzibar inabebwa na Muungano! Hivyo gharama za mambo ya nje, jeshi, polisi, usalama wa taifa nk zinabebwa na Watanganyika.

Hivyo vyombo vyote hivyo ni mali ya Watanganyika! Zanzibar hawana chao!

Kwa muktadha huo endapo tutaunda serikali tatu, ni serikali ya Tanganyika itakayoumia. Au kwa maneno mengine ni Kodi za Watanganyika zitakazotumika.

Endapo muungano utavunjika rasilimali zote za jeshi, polisi, usalama wa taifa nk itabidi zirudishwe Tanganyika. Zanzibar itabaki bila jeshi, polisi wala usalama wa taifa nk. Usalama wa taifa la Zanzibar utakuwa mashakani.

Ni vema Wazanzibari wakaanza kujitafakari hivi sasa! Kuna hatari kubwa ipo mbele yao!

Zanzibar tafakari kabla hamjaamua! Heri kinga kuliko tiba!
 
Kwa mantiki hiyo Zanzibar inabebwa na Muungano! Hivyo gharama za mambo ya nje, jeshi, polisi, usalama wa taifa nk zinabebwa na Watanganyika.

Hivyo vyombo vyote hivyo ni mali ya Watanganyika! Zanzibar hawana chao!


Endapo muungano utavunjika rasilimali zote za jeshi, polisi, usalama wa taifa nk itabidi zirudishwe Tanganyika. Zanzibar itabaki bila jeshi, polisi wala usalama wa taifa nk. Usalama wa taifa la Zanzibar utakuwa mashakani.

Ni vema Wazanzibari wakaanza kujitafakari hivi sasa! Kuna hatari kubwa ipo mbele yao!
Nani aliyekwambia kuwa muungano wa kinchi huvunjwa ghafla bin vuu?

Nchi zote mbili hupewa nafasi ya kujipanga kwanza kabla ya kuvunja muungano wowote ule.

...huna hoja, kajipange upya.
 
Nani aliyekwambia kuwa muungano wa kinchi huvunjwa ghafla bin vuu?

Nchi zote mbili hupewa nafasi ya kujipanga kwanza kabla ya kuvunja muungano wowote ule.

...huna hoja, kajipange upya.


Ndiyo unaamka, mbona unakurupuka! To a data wapi muungano wa nchi ulivunjika polepole!
 
Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar ilichangia gharama za kuendesha serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa miaka mitatu tu tangu 1965 - 1967 kwa asilimia kati ya 5 - 11.

Kwa mantiki hiyo Zanzibar inabebwa na Muungano! Hivyo gharama za mambo ya nje, jeshi, polisi, usalama wa taifa nk zinabebwa na Watanganyika.

Hivyo vyombo vyote hivyo ni mali ya Watanganyika! Zanzibar hawana chao!

Kwa muktadha huo endapo tutaunda serikali tatu, ni serikali ya Tanganyika itakayoumia. Au kwa maneno mengine ni Kodi za Watanganyika zitakazotumika.

Endapo muungano utavunjika rasilimali zote za jeshi, polisi, usalama wa taifa nk itabidi zirudishwe Tanganyika. Zanzibar itabaki bila jeshi, polisi wala usalama wa taifa nk. Usalama wa taifa la Zanzibar utakuwa mashakani.

Ni vema Wazanzibari wakaanza kujitafakari hivi sasa! Kuna hatari kubwa ipo mbele yao!

Zanzibar tafakari kabla hamjaamua! Heri kinga kuliko tiba!
Mkuu Ileje, mnyonge mnyongeni haki yake mpeni!, baada ya muungano, Zanzibar pia imetoa majeshi, polisi na wana usalama wake ndani ya majeshi yetu ya ulinzi na usalama!.

Hili la kutochangia gharama za muungano pia kwa Zanzibar ni haki yao!, kwa sababu hakuna mahali popote panapoonyesha gharama za muungano ni zipi na gharama za Tanganyika ni zipi?!. Kero hii haina dawa nyingine zaidi ya serikali moja au serikali tatu!.

Kwa zile wizara za muungano, zinashughulikia mambo ya muungano, na mambo ya bara, hakuna mchanganuo wowote wa gharama za muungano ni kiasi gani, hivyo Zanzibar wako very right, hawawezi kuchangia, bila kujua wanachangia nini kwa mahitaji gani?!.

Muungano ni kama ndoa, ikivunjika, wanandoa wanagawana pasu pasu regardless mwanandoa mmoja amechangia nini!.
Pasco
 
Hata kisiasa haupo, upo kikanisa zaidi, huo ndio ukweli.

Linaloutaka muungano zaidi ni kanisa. Ni siri isiyofichika Muungano ukivunjika na kanisa limevunjika Zanzibar.

Akili yako imetimia kweli... Kanisa linahusikaje na muungano? Wewe utakuwa unatumia nini kufikiri... Nadhani ni ...ko
 
Nani aliyekwambia kuwa muungano wa kinchi huvunjwa ghafla bin vuu?

Nchi zote mbili hupewa nafasi ya kujipanga kwanza kabla ya kuvunja muungano wowote ule.

...huna hoja, kajipange upya.

Ndiyo unaamka, mbona unakurupuka! To a data wapi muungano wa nchi ulivunjika polepole!

Kumbukumbu ya kuvunjika kwa EAC ipo?
Huwa hakuna makubaliano!!!!!!!!
 
Mkuu Ileje, mnyonge mnyongeni haki yake mpeni!, baada ya muungano, Zanzibar pia imetoa majeshi, polisi na wana usalama wake ndani ya majeshi yetu ya ulinzi na usalama!.

Hili la kutochangia gharama za muungano pia kwa Zanzibar ni haki yao!, kwa sababu hakuna mahali popote panapoonyesha gharama za muungano ni zipi na gharama za Tanganyika ni zipi?!. Kero hii haina dawa nyingine zaidi ya serikali moja au serikali tatu!.

Kwa zile wizara za muungano, zinashughulikia mambo ya muungano, na mambo ya bara, hakuna mchanganuo wowote wa gharama za muungano ni kiasi gani, hivyo Zanzibar wako very right, hawawezi kuchangia, bila kujua wanachangia nini kwa mahitaji gani?!.

Muungano ni kama ndoa, ikivunjika, wanandoa wanagawana pasu pasu regardless mwanandoa mmoja amechangia nini!.
Pasco

Mhe Pasco si kweli gharama za muungano hazifahamiki! Na pia si kweli kuwa zinafanya mambo ya Tanganyika!

Zanzibar inapaswa kulipia gharama za kuendesha muungano kwa proportion; yaani asilimia 4, 8, au 10 kulingana namna inavyonufaika! Na pia mambo ya muungano yanayofanywa Tanganyika ni kulingana na eneo lake na idadi ya watu kama ilivyo kwa Zanzibar!
 
Kumbukumbu ya kuvunji kwa EAC ipo?
Huwa hakuna makubaliano!!!!!!!!

Jumuiya ya Afrika Mashariki ilivunjika bin vuu! Ndiyo maana kila nchi ilichukua kile kilichokuwepo nchini kwake!

Ili kusuluhisha tatizo hili Benki ya Dunia ilileta msuluhishi Dr. Umbrich ambaye alitengeneza formula ya kugawana mali za jumuiya! Kutokana na formula hiyo Kenya ililazimika kuzilipa Tanzania na Uganda!
 
Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar ilichangia gharama za kuendesha serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa miaka mitatu tu tangu 1965 - 1967 kwa asilimia kati ya 5 - 11.

Kwa mantiki hiyo Zanzibar inabebwa na Muungano! Hivyo gharama za mambo ya nje, jeshi, polisi, usalama wa taifa nk zinabebwa na Watanganyika.

Hivyo vyombo vyote hivyo ni mali ya Watanganyika! Zanzibar hawana chao!

Kwa muktadha huo endapo tutaunda serikali tatu, ni serikali ya Tanganyika itakayoumia. Au kwa maneno mengine ni Kodi za Watanganyika zitakazotumika.

Endapo muungano utavunjika rasilimali zote za jeshi, polisi, usalama wa taifa nk itabidi zirudishwe Tanganyika. Zanzibar itabaki bila jeshi, polisi wala usalama wa taifa nk. Usalama wa taifa la Zanzibar utakuwa mashakani.

Ni vema Wazanzibari wakaanza kujitafakari hivi sasa! Kuna hatari kubwa ipo mbele yao!

Zanzibar tafakari kabla hamjaamua! Heri kinga kuliko tiba!

1.Kwa kipindi cha miaka 50 hatujapigana na mtu si comorrow wala Kenya sasa hilo jeshi la nini kwetu?
2.Kule kwetu kuna JKU, Valantia,KMKM , Zimamoto na Janjawidi (Kikosi cha CCM) wanaofanya kazi za kipolisi, sasa tulipie nini?
3.Sisi hatuna mahusiano na nchi za nje (tulipojiunga na OIC mkatulazimisha tujitowe) sasa hayo mambo ya nje tunalipia nini?
4.Bunge linatunga sheria za Tanganyika, sisi tuna Baraza letu la kutunga sheria, sasa tunalipia nini?
5.Uhamiaji pasipoti tunanunua kwa pesa zetu sasa tulipe nini?

Wafanyakazi, mapolisi na majeshi (wanakufa kukulindeni nyie na kukupeni sifa) wanakutumikieni nynyi na serikali yenu, mnataka walipwe na nani? Hata wabunge wa Zanzibar wanakusaidieni kutunga sheria zenu kama maexpert na mawaziri waliotoka Zanzibar nao ni experts katika kujenga nchi yenu Tanganyika
 
1.Kwa kipindi cha miaka 50 hatujapigana na mtu si comorrow wala Kenya sasa hilo jeshi la nini kwetu?
2.Kule kwetu kuna JKU, Valantia,KMKM , Zimamoto na Janjawidi (Kikosi cha CCM) wanaofanya kazi za kipolisi, sasa tulipie nini?
3.Sisi hatuna mahusiano na nchi za nje (tulipojiunga na OIC mkatulazimisha tujitowe) sasa hayo mambo ya nje tunalipia nini?
4.Bunge linatunga sheria za Tanganyika, sisi tuna Baraza letu la kutunga sheria, sasa tunalipia nini?
5.Uhamiaji pasipoti tunanunua kwa pesa zetu sasa tulipe nini?

Wafanyakazi, mapolisi na majeshi (wanakufa kukulindeni nyie na kukupeni sifa) wanakutumikieni nynyi na serikali yenu, mnataka walipwe na nani? Hata wabunge wa Zanzibar wanakusaidieni kutunga sheria zenu kama maexpert na mawaziri waliotoka Zanzibar nao ni experts katika kujenga nchi yenu Tanganyika

Kweli akili ni nywele kila mtu ana zake!
1.Tanganyika ndiyo inailinda Zanzibar;
2. Wazanzibari wananufaika kwa ajira, masomo katika vyuo vikuu;
3. Kwenye balozi zetu nje wamejaa Wazanzibari!;
4. Wazanzibari wanamiliki ardhi Tanganyika; nk

Yote haya mnayofanyiwa hakuna hata shukrani?!
 
Mhe Pasco si kweli gharama za muungano hazifahamiki! Na pia si kweli kuwa zinafanya mambo ya Tanganyika!

Zanzibar inapaswa kulipia gharama za kuendesha muungano kwa proportion; yaani asilimia 4, 8, au 10 kulingana namna inavyonufaika! Na pia mambo ya muungano yanayofanywa Tanganyika ni kulingana na eneo lake na idadi ya watu kama ilivyo kwa Zanzibar!

Na kinachokusanywa kwa pamoja kinaenda wapi?
 
Hata kisiasa haupo, upo kikanisa zaidi, huo ndio ukweli.

Linaloutaka muungano zaidi ni kanisa. Ni siri isiyofichika Muungano ukivunjika na kanisa limevunjika Zanzibar.

naomba utufafanulie hapo. Ninachojua ni kuwa 'kanisa' pande hizi za East Africa liliingilia kupitia zanzibar. sasa itakuwaje kanisa ambalo liliingia bara kupitia zanzibar litegemee bara ili kuishi zanzibar?
 
Kweli akili ni nywele kila mtu ana zake!
1.Tanganyika ndiyo inailinda Zanzibar;
2. Wazanzibari wananufaika kwa ajira, masomo katika vyuo vikuu;
3. Kwenye balozi zetu nje wamejaa Wazanzibari!;
4. Wazanzibari wanamiliki ardhi Tanganyika; nk

Yote haya mnayofanyiwa hakuna hata shukrani?!

Wacha uji nga wewe? Tanganyika inailinda Zanzibar na nani CUF na UAMSHO?
Majeneza mangapi yameletwa Tanganyika kutokana na kuwapiganuia Wazanzibari?
Balozi za nje wanalipwa si wanafanya kazi ya kuijenga Mwanza Arusha, Dodoma na kengineko Tanganyika, jee wanasaidia nini kwa Serikali ya Zanzibar?
Wazanzibari kumiliki ardhi Tanganyika ni sawa na wawekezaji, wao ndio wenye kujenga mimji, na kutowa kodi nyingi, unataka hisani gani tena kwani si mnaiita wawekezaji?
 
Wacha uji nga wewe? Tanganyika inailinda Zanzibar na nani CUF na UAMSHO?
Majeneza mangapi yameletwa Tanganyika kutokana na kuwapiganuia Wazanzibari?
Balozi za nje wanalipwa si wanafanya kazi ya kuijenga Mwanza Arusha, Dodoma na kengineko Tanganyika, jee wanasaidia nini kwa Serikali ya Zanzibar?
Wazanzibari kumiliki ardhi Tanganyika ni sawa na wawekezaji, wao ndio wenye kujenga mimji, na kutowa kodi nyingi, unataka hisani gani tena kwani si mnaiita wawekezaji?

Siwezi kuendelea kubishana na MPU-MBA-VU maana watu watashindwa kututofautisha!
 
Back
Top Bottom