Nyanya 50-60x75
Tikiti 100-150x150
Kabeji 40-50x40
Vitungu 7-10x15x(30 njia)
Karoti 5x15(x30 njia)
Bamia 45x45
Hizi ni kwa kilimo cha umwagiliaj wa kawaida,kwa drip nyingne zinachange kama nyanya ya drip n 40x40x150 kwa determinate type na 30x30x150 kwa indeterminate type.
Vipimo vyote ni kwa sentimita
Nyanya hybrid tuna tylika eden kilele anna kipato assla moyo na zingine toka rick zwan opv ni nyingi hoho kuna tycoon na pepite c and y wonder.
Ningependa tuanzishe thread mpya kwa kila tunda/zao
Kwa mfano tuzungumzie tikiti kuanzia mbegu zake
Upatikanaji
Upandaji
Madawa
Mgonjwa yake nauuzwaji pamoja na faida yake nadhani hiyo itasaidia zaidi!
Whatsapp Group KWA WAKULIMA NA WAFUGAJI TU 0717269137
Kilimo cha parachi ndugu sio kigumu sema kina mengi mpaka pa kuanzia shughuli,tuanze na mbegu
Parachichi huoteshwa kwa njia mbili ,moja kupanda miche pili kupanda mbegu,hapo pa miche kuna ya kuungwa(grafted) na ambayo haijaungwa.Iliyoungwa inafaida ya kuweza kupambana na magonjwa ya kwenye udongo ya sehemu husika sababu wanatumia mbegu za asili za parachichi(mbegu ya asili huwa ya duara wakati ya kisasa/kizungu huwa yamechongoka upand mmoja) pia ya kuunga huchukua muda mfupi toka kuotesha mpaka kuanza kuvuna.Aina nzuri ni Fuerte na Hasi.
Ya kienyeji hupandwa mbegu shambani moja kwa moja,hukua hata kwenye mazingira magumu,hukaa muda mrefu sema utachelewa kuanza kuvuna
Ndugu zanguni,naombeni kuelimishwa juu ya kilimo cha parachichi.
Mkuu vipi kilimo kwanza kimefikia wapi utekelezaji wake?hebu tupe data hapa
Mimepanda Passion na Ndizi, nimeshaanza kuvuna, nafahamu kuwa haya matuna unavuna mwaka mzima, sasa Naomba unishauri ni yapi mengine
Kilimo cha parachi ndugu sio kigumu sema kina mengi mpaka pa kuanzia shughuli,tuanze na mbegu
Parachichi huoteshwa kwa njia mbili ,moja kupanda miche pili kupanda mbegu,hapo pa miche kuna ya kuungwa(grafted) na ambayo haijaungwa.Iliyoungwa inafaida ya kuweza kupambana na magonjwa ya kwenye udongo ya sehemu husika sababu wanatumia mbegu za asili za parachichi(mbegu ya asili huwa ya duara wakati ya kisasa/kizungu huwa yamechongoka upand mmoja) pia ya kuunga huchukua muda mfupi toka kuotesha mpaka kuanza kuvuna.Aina common ni Fuerte na Hass.
Ya kienyeji hupandwa mbegu shambani moja kwa moja,hukua hata kwenye mazingira magumu,hukaa muda mrefu sema utachelewa kuanza kuvuna.Ya kuungwa huza baada ya mwaka mpaka miaka miwili na ya kupanda mbegu huzaa kuanzia mwaka wa tano mpaka wa saba,parachichi uhitaji sehemu za baridi na udongo wa ph ya 5 mpaka 7.uhitaji sehemu yenye hali ya hewa ya degrees celcius 15 mpaka 20 kwa usiku na 25 mpaka 30 kwa mchana(ujumla ukanda wa baridi).nafasi ya mti kwa mti ni 7.5x7.5mita kwa mikubwa ni 10x10mita shimo la kupanda liwe na urefu na upana wa 0.6mita.
Toka kutoa maua uchukua miezi 6 mpaka 8 kwa parachichi kuwa tayari kuvunywa kwa miparachichi midogo(mexican type) na huchukua miezi 12 mpaka 18 kwa miti mikubwa (guetemalan type?.
Kama uko karibu na Moshi waone Africado ndugu wanambegu na wanatoa wataalam na wananunua kwako ukivuna.
Mche huwa kati ya tsh 2500 mpaka 5000
Ahsante mkuu ubarikiwe
Sawa boss wangu hapa kwetu Mlali na Mgeta twatumia hizi ili plant population iwe sawa. Siko hapa kupinga
Na katika uzi huu niliona spacing ya 150 toka tuta mpaka tuta ni kubwa pia 40 kwa 40 hizi sio kwa bush nyanya sie hata hoho twatumia 45
Mgeta bunda na serengeti hali ya hewa si moja, poa wape hi bunda msalimie mkelewe na makono hapo