Kwa maswali na majibu kwa masuala ya kilimo tu

kuna madhara gani kama mwembe mmoja nikau graft aina tofauti za miembe kwenye matawi yake, mf kipande cha chini kiwe embe sindano matawini niunge embe mwaka, bolibo, na mingineyo.
 
kuna madhara gani kama mwembe mmoja nikau graft aina tofauti za miembe kwenye matawi yake, mf kipande cha chini kiwe embe sindano matawini niunge embe mwaka, bolibo, na mingineyo.

Hakuna madhara kazi ni kupata hayo matawi ya kuunga hivyo,embe mpaka wakati wa kuunga huwa na tawi moja tu
 
Mkuu naomba utuelezee jinsi ya kuchoma udongo na faida zake


Udongo kuna njia tofaut za kuuchoma,inajumuisha kwa kutumia chemicals,kutumia jua,kutumia mvuke n.k.rahisi na efficient ni ya mvuke,hii hufikisha udongo mpaka temp ya 127 degrees centigrade ambapo huu mpaka virusi,minyoo(nematodes) hufa temp ya 60 na bacteria hamful mostly temp ya 80.
Faida zake kwa uwezo wetu wa kitanzania huwa tunachoma udongo wa kutumia kwenye trays tu(nursery/kitalu) kwa makampuni makubwa wao huchoma shamba zima,kazi kuu kwa sisi wakulima wa kawaida ni kwa kuzalisha miche ambayo haina magonjwa hivyo kuwa na afya na kuweza kupambana na magonjwa ikipandwa shambani tofauti na mche ambao unakua na magonjwa toka kitaluni.
Kuchoma udongo unahtajika uwe na pipa 1 lililozibwa lote na kutobelewa njia moja tu yenye mpira/bomba la kupitisha maji na mvuke,mpira wa urefu wa mita 5 na wenye uwezo wa kupitisha mvuke pasi na kuyeyuka na wenye chuma cha kutolea mvuke upande mmoja,chanzo cha moto na boksi la mbao la kufunuka upande mmoja wa juu tu.Chukua media yako kama ni ya forest soil au yoyote chekecha upate fine soil and weka kwenye box la mbao (udongo uwe kwenye nylon),weka maji nusu pipa au robo kisha bandika jikon,unganisha mpira wako na pipa upande wenye chuma cha kutolea mvuke chomeka kwenye udongo ndan ya box kisha funika box kwa mfuniko wake,chochea maji yatachemka na mvuke utapita kwenye bomba mpaka kwenye udongo ndani ya box,mwanzo udongo utakua unatoa moshi mchafu kama vumbi endelea mpaka pale udongo utakapotoa moshi mweusi wa rangi ya udongo na mzito pia utaona udongo wako umetota kiasi basi tambua uko tayar,pia wakat unaweka udongo kwenye box unaweza weka na viazi ulaya(irish potato) kwenye pembe nne za box na kati kati ya udongo ndani ya box,viazi vikiiva jua udongo uko teyari.
Utoe uweke mahali upoe na epuka kuukutanisha na untreated soil kuepuka kuuambukiza tena.(nb nina picha bahati mbaya cwez z attach inagoma kabisa simu yangu.)ahsante
 
Mkuu naomba kujuzwa, ni mbegu kiasi gani ya vitunguui inaweza tosha eka moja kwa mavuno ya gunia 50-70 kwa eka.
Natanguliza shukrani kwa masaada wako.
 
Mkuu naomba kujuzwa, ni mbegu kiasi gani ya vitunguui inaweza tosha eka moja kwa mavuno ya gunia 50-70 kwa eka.
Natanguliza shukrani kwa masaada wako.

Mbegu kiasi cha kg 2.5 za vitunguu zinatosha kwa ekari,tumia nafasi ya kitunguu hadi kitunguu ni 8 sm na mstari na mstari ni 15 sm na baada ya mistari sita unaacha nafasi ya sm 30 ambayo kama utapanda kwa matuta itakua ndio nafasi ya tuta hadi tuta,hii itakua njia yako wakati wa kuhudumia shamba.karibu ndugu
 
Mbegu kiasi cha kg 2.5 za vitunguu zinatosha kwa ekari,tumia nafasi ya kitunguu hadi kitunguu ni 8 sm na mstari na mstari ni 15 sm na baada ya mistari sita unaacha nafasi ya sm 30 ambayo kama utapanda kwa matuta itakua ndio nafasi ya tuta hadi tuta,hii itakua njia yako wakati wa kuhudumia shamba.karibu ndugu

Mtaalamu nashukuru sana kwa majibu mazuri sana,nimekupata barabara kabisa.

Mkuu mbegu wakati wa kusia natakiwa kutawanya random au kwene mstari na natakiwa kuhamisha baada ya muda gani kutoka kitalu kwenda shambani?.
Standard size ya tuta la kitalu na shamba(lakuhamishia) ni kiasi gani?
Natanguliza shukrani, samahani kwa usumbufu mkuu.
 
Mtaalamu nashukuru sana kwa majibu mazuri sana,nimekupata barabara kabisa.

Mkuu mbegu wakati wa kusia natakiwa kutawanya random au kwene mstari na natakiwa kuhamisha baada ya muda gani kutoka kitalu kwenda shambani?.
Standard size ya tuta la kitalu na shamba(lakuhamishia) ni kiasi gani?
Natanguliza shukrani, samahani kwa usumbufu mkuu.

Tuta la kitalu tumia upana wa sm80 na tuta la shamba liwe la sm 100 urefu wowote ule ila iwe juu ya mita 5,tuta moja hadi lingine acha njia ya 30 sm.ukisia kwenye kitalu chora mistar ya umbali wa sm 15 ime imekata tuta na isinyooke kufuata urefu sia mbegu kisha funika na majan makavu hata ya mgomb au majan kuzuia ukmwagilia mbegu zisisombwe na maji na kutawanywishwa.Shambani mistari ifuate urefu wa tuta.
Karibu sana ndugu
 
the horticulturist;
Naomba unisaidie, hivi drip lines(pipes)huwa wanauza moja ndefu na unakata ww kwa vipimo vyako au inakua ktk vipande? kama iko ktk vipande vina urefu gan? natanguliza shukran
 
the horticulturist;
Naomba unisaidie, hivi drip lines(pipes)huwa wanauza moja ndefu na unakata ww kwa vipimo vyako au inakua ktk vipande? kama iko ktk vipande vina urefu gan? natanguliza shukran

Umenichanganya maana umeongelea drip line na pipes,pipes ni pvc pipes zina urefu wa mita 10 na kwa drip line inauzwa kwa roller ndugu
 
Umenichanganya maana umeongelea drip line na pipes,pipes ni pvc pipes zina urefu wa mita 10 na kwa drip line inauzwa kwa roller ndugu

Nimekupata, nilimaanisha hasa drip lines. ohoo kumbe unanunua roller unakuja kukata mwenyewe kutegemea na shamba lako. hapo sawa. pia tank la lita 1000 litafaa kutumia kwa kilimo cha kabeji kwenye eneo la 500mita za eneo?
 
Hakika mnatumia opv ndugu wanawadanganya ni hybrid mfano tengeru 97 ni opv ila wauza duka la pembejeo watakueleza n hybrid,nimelima anna f1 na shanti ,anna f1 mbegu ya eka ina cost tsh 270,000 na hupati maduka ya kawaida ndugu.pili pili hoho qsem mche wanauza tsh 300 hoho za njano na nyekundu(ilanga na parsilela),mnatumia hizo ndugu au mnauziwa tu za opvs?

unaposema Opv, unamaanisha nini? mtaalamu.
 
unaposema Opv, unamaanisha nini? mtaalamu.

Open pollinated varieties,ni mbegu ambazo si hybrid na zinahitaji pollination(uchavushaji)ili kutoa mazao mara nying hupandwa nnje si kwenye green house,kuna hybrid ambazo huzaa hata bila ya uchavushaji
 
Open pollinated varieties,ni mbegu ambazo si hybrid na zinahitaji pollination(uchavushaji)ili kutoa mazao mara nying hupandwa nnje si kwenye green house,kuna hybrid ambazo huzaa hata bila ya uchavushaji

asante mtaalamu mimi mwezi wa pili nilipanda nyanya, na niliuziwa mbegu ambayo muuzaji alidai ni Ana f1, lakini cha ajabu ile nyanya ilikua ikishambuliwa sana na magonjwa pamoja na kufuata masharti yote ya upigaji madawa, kwa maelezo yako, napata picha kuwa Ile mbegu huenda ilikua hiyo Opv uliyosema, mwaka huu mwezi wa kumi na plan nifanye tena mradi huu, hivyo ntaomba unielekeze sehemu ntakayo pata hiyo genuine hybrid. mimi niko morogoro. asante
 
Nimekupata, nilimaanisha hasa drip lines. ohoo kumbe unanunua roller unakuja kukata mwenyewe kutegemea na shamba lako. hapo sawa. pia tank la lita 1000 litafaa kutumia kwa kilimo cha kabeji kwenye eneo la 500mita za eneo?

Halitoshi ndugu chukua kubwa eneo hilo ni kubwa nilitumia la 750 lita ktk eneo la 120 mita na lilisumbua
 
asante mtaalamu mimi mwezi wa pili nilipanda nyanya, na niliuziwa mbegu ambayo muuzaji alidai ni Ana f1, lakini cha ajabu ile nyanya ilikua ikishambuliwa sana na magonjwa pamoja na kufuata masharti yote ya upigaji madawa, kwa maelezo yako, napata picha kuwa Ile mbegu huenda ilikua hiyo Opv uliyosema, mwaka huu mwezi wa kumi na plan nifanye tena mradi huu, hivyo ntaomba unielekeze sehemu ntakayo pata hiyo genuine hybrid. mimi niko morogoro. asante

Nunua product yoyote ya kilimo toka kwa muuzaji mwenyewe au authorised dealer,kama ni product ya kibo,balton,syngenta hakikisha umenunua kwa wakala wao au kampuni branch zao mbali na hivyo utakumbana na zilizochakachuliwa ndugu,watanzania ujanja umezidi,pia ukinunua kwao au wakala bei ni rahisi pia
 
Nunua product yoyote ya kilimo toka kwa muuzaji mwenyewe au authorised dealer,kama ni product ya kibo,balton,syngenta hakikisha umenunua kwa wakala wao au kampuni branch zao mbali na hivyo utakumbana na zilizochakachuliwa ndugu,watanzania ujanja umezidi,pia ukinunua kwao au wakala bei ni rahisi pia

naomba unisaidie ni mbegu gani ya Nyanya hybrid inayoweza limwa ukanda wa pwani hasa mkuranga na ni ipi yenye soko kubwa kwa Dar es salaam.
 
Strawberries zinastawi hapa Tanzania? Mikoani gani haswa? Mbegu au miche yake inapatikana wapi?
 
Nimeupenda sana Uzi wako na nimejifunza vitu kutoka kwenye maelezo yako, big up. Kwa wale wajasiriamali wanaopenda kubadilishana mawazo kwa njia ya whataap tuwasiliane 0762600100
 
Back
Top Bottom