Kwa lipi Lowassa apewe nchi?

Kwa lipi Lowassa apewe nchi?

Lowassa urais atausikia tu baada ya kuhujumiwa na rafiki yake JK. Kauli ya Ridhiwani,ya kuwa rais hawezi kutoka kaskazini ni kauli ya Kikwete,how did he know? Ridh,yuko jikoni,kwa hyo anajua kinachopikwa.
Pia,Lowassa hawezi kuwa rais kwa sababu,vigogo wengi wa ccm hawamuungi mkono,akiwemo Sitta,Mwakyembe,Membe,Magufuli nk yeye kakazana na wajumbe wa halmashuri kuu ya ccm.
Makundi ndani ya ccm,hayawezi kumvusha ndg yangu huyu.
 
Tena acheni utani kabisa kwenye mambo ya msingi kwa maslahi mapana ya nchi yetu. Hivi kweli mnaompa moyo na kumpigia kampeni ya kugombea urais, mko serious kweli au mmeamua kumlia hela zake tu huku mkijua fika kuwa hawezi kupita hata nusu ya hatua kuanzia za kwenye chama!

Hata kama ndo watu wenye sifa wameisha ndani ya CCM ndo mumchague kabisa Lowassa akahimili vishindo vizito vya UKAWA kweli!

Jamani hivi kweli Lowassa awe rais wa nchi kweli! Hapana lazima ifike wakati tuwe serious! Hii nchi ni yetu sote! Hatuwezi kuwakabidhi mafisadi waongoze nchi! Yaani kampani ya akina Chenge majoka yenye makengeza yanayosaka pesa kwa namna yoyote ile zikiwemo chafu na haramu!

Cha kufanya ni kumshauri tu Lowassa ajiangalie afya yake ajitibie maradhi yake yanayomsibu ili aje ashuhudie mchuano mkali kati ya UKAWA na CCM october akiwa na afya yenye unafuu kuliko kuendelea na harakati ambazo ni dhahiri zitaishia njiani na kumuongezea maradhi yatakayohatarisha uhai wake!

Tafakari chukua hatua teamLowassa a.k.a TeamFisadi!
 
Tuna matumaini makubwa sana na wewe Mheshimiwa Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa kwani uwezo wako unajulikana na kila Mtanzania

1907513_966068363427614_4736803703485890492_n.png
 
Mbona jina lake haliishi vinywani mwenu!!!
 
Mbona jina lake haliishi vinywani mwenu!!!
Jibu kwanza kwanini unamuita waziri mkuu mstaafu wakati hakustaafu bali alijiuzulu kwa shinikizo kali la ubunge kutokana na kashfa nzito ya ufisadi wa richmond? Jibu hilo kwanza!
 
Jibu kwanza kwanini unamuita waziri mkuu mstaafu wakati hakustaafu bali alijiuzulu kwa shinikizo kali la ubunge kutokana na kashfa nzito ya ufisadi wa richmond? Jibu hilo kwanza!
mwaka huu mtahangaika sana na viungo vya Albino kwaajili ya huyu bwana!
 
Binafsi sitakuwa na amani rohoni kwangu kama Rais atatoka ndani ya CCM kwa mara nyingine tena, kwa sababu kuu zifuatazo:-
1. Mfumo wa uongozi ambao umepigiwa kelele kutwa kucha hautabadilika kwani sura ni zilezile na business as usual.
2. Hatma ya maisha ya baadae ya kizazi cha watoto ambao wapo chini ya miaka (10) itakuwa hatihati hasa kwa wale wanaotoka familia maskini. (hapa naongelea Afya, Lishe na Elimu yao)
3. Maisha ya watanzania kwa ujumla yataendelea kuwa magumu na maendeleo ya taifa kwa ujumla yataendelea kupiga hatua kurudi kinyume-nyume. Hapa naongelea Ardhi inaporwa na wajanja wachache wakijiita wawekezaji, Elimu ni kwa matabaka, Hicho kilimo tunachokitegemea tulio wengi kipo mahututi kama si mochware.

Na mengine mengi tu, Sasa cha msingi watanzania ni wakati sasa wa kubadilisha mfumo wa utawala wa taifa letu, kubadilisha Rais na mfumo ukabakia uleule hatutakuwa tumefanya kitu chochote kile ushahidi juu ya hili tunao, na baadaye tutabakia tukijilaumu tu kwa miaka mingine mitano kama kawaida yetu.

Mwezi wa Kumi watanzania tufanyeni maamuzi mazito. Rais ajaye asitokana na hawa jamaa, hawana nia njema na sisi.
 
Jibu kwanza kwanini asiwe Rais then uje na hoja nzito sio fantasy unazosikia vijiweni na kwenye magazeti ya udaku.alafu ukae ukijua wanaomsapoti lowasa hawachukui hata senti tano yake.
 
MKUU!

KUNA MAKUNDI MATATU YA WATU WANAOMSEMEA LOWASSA NA KUTAKA KUTUAMINISHA KWAMBA NI MTU MWENYE SIFA NZURI ZA HADI KUPEWA URAIS.

1.
Kundi la watu amabao kwa kupitia mitandao aliyojiwekea huyu Bwana Edward wanamwagiwa pesa ili kuendelea kumpigia kampeni. Na hili huyu Bwana ameliweza sana maana ukweli ni kwamba pesa anayo. Kundi hili ni la waganga njaa, wachumia tumbo na walafi wasio na aibu.

2. Kuna kundi la watu ambao wanajiwekea matumaini kuwa huyu Bwana Edward akipita basi na wao watakumbukwa katika ufalme wake na kupata nafasi za kujinufaisha kwenye huo mfumo atakao weka wa uongozi. Huyu Bwana Edward hasiti kuwaambia hao watu, 'fanyeni kazi maana siku ikifika nanyi muingie huku kunako starehe za utawala.' Kundi hili ni la wabinafsi, wenye tamaa, na uchu uliojaa usongo kiasi kwamba hata ukweli wanaoujua kuhusu huyu Edward hawako tayari kuukubali.

3. Kundi la tatu ni la watu ambao kwa nafasi zao mbalimbali na hasa za uongozi wanalazimika kusema mara moja moja kuhusu Lowasa. Mara utasikia kiongozi huyu amemmwagia sifa Edward, mara mwingine atasema Edward ni chaguo la wengi na hata Mama mmoja kiongozi wa juu aliwahi kusema "Hakuna mwanamume kama Lowassa! "Hili ni kundi la wanafiki, na ndilo kundi baya kuliko mengine. Wengine kundini humu wanasema ya kumsifia Edward kama vile kumpooza kwa masaibu yaliyomkuta - haswa kufukuzwa uwaziri mkuu, lakini wengine ni kwa sababu tu ya kubalance mambo ya kisiasa kwenye Chama!

Makundi yote hayo ni ya watu walioingiwa na upofu, na mtindio wa mawazo kiasi kwamba hawaoni kwamba wanataka kuliuza taifa hili kwa tamaa zao, na bila hata haya wala soni, wakiendekeza mapungufu yao ya tamaa, unafiki, na ulafi usio na mfano.

Sijui sura zao watakuja zificha wapi siku uhaini wao huu ukituingiza kwenye matatizo kama taifa ikija tokea huko mbele!
 
Tena acheni utani kabisa kwenye mambo ya msingi kwa maslahi mapana ya nchi yetu. Hivi kweli mnaompa moyo na kumpigia kampeni ya kugombea urais, mko serious kweli au mmeamua kumlia hela zake tu huku mkijua fika kuwa hawezi kupita hata nusu ya hatua kuanzia za kwenye chama!

Hata kama ndo watu wenye sifa wameisha ndani ya CCM ndo mumchague kabisa Lowassa akahimili vishindo vizito vya UKAWA kweli!

Jamani hivi kweli Lowassa awe rais wa nchi kweli! Hapana lazima ifike wakati tuwe serious! Hii nchi ni yetu sote! Hatuwezi kuwakabidhi mafisadi waongoze nchi! Yaani kampani ya akina Chenge majoka yenye makengeza yanayosaka pesa kwa namna yoyote ile zikiwemo chafu na haramu!

Cha kufanya ni kumshauri tu Lowassa ajiangalie afya yake ajitibie maradhi yake yanayomsibu ili aje ashuhudie mchuano mkali kati ya UKAWA na CCM october akiwa na afya yenye unafuu kuliko kuendelea na harakati ambazo ni dhahiri zitaishia njiani na kumuongezea maradhi yatakayohatarisha uhai wake!

Tafakari chukua hatua teamLowassa a.k.a TeamFisadi!

lowasa ndo rais ajae taka usitake.We hela ngapi zimepigwa je kazipiga zote lowasa?Kama makanisani na misikitin dili zinaiga yeye lowasa kawazidi na roho ya kiimani kuliko hao wa nyumba za ibada au hata JK mwenywe? wivu wa kwenye chupi huo
 
Back
Top Bottom