Saplaiz
JF-Expert Member
- Mar 26, 2014
- 283
- 287
Mtakufa kwa presha EL asipokuwa Raid by e vibaraka wake. In short EL can't be our president, amechafuka!!
Nani msafi....
Mtakufa kwa presha EL asipokuwa Raid by e vibaraka wake. In short EL can't be our president, amechafuka!!
Nikimuona mtu anamsifia fisadi Lowasa anatamani nimwagie hata maji ya moto unampigiaje debe mtu mwizi kama lowasa?
Mafisadi wajiandaa kuchafua Chama Cha Mapinduzi na Serikali yake: Taarifa tulizozipata zisizotiliwa shaka ,Ni kwamba Genge la Mafisadi likiongozwa na baadhi ya wahariri na kijana mmoja Mwenye asili ya Kisomali anayetoka kanda ya Ziwa,limejipanga kwa vita ya kuanza kuwachafua, baadhi ya viongozi wa chama na waasisi wa Taifa hili ikiwemo Familia ya mwalimu Nyerere.Kwa lipi la maana alilolifanya Lowassa hadi apewe nchi?
Kuna sababu nyingi za kusema Lowassa hafai kuwa rais wa nchi hii licha ya kuwa mgonjwa wa macho na mgongo pia ni mmoja wa watu 11 waliotajwa kuwa ni mafisadi.
Amefanya nini la maana hadi tumpe nchi? Unamkumbuka kwa lipi zaidi ya kujiuzulu?
Pesa zake sio tiketi kuwepo ulazima wa kuingia ikulu. Kama anatafuta umaarufu,umaarufu sio kwa mazuri tu hata ufisadi na kujiuzulu napo aljulikana ndani na nje ya nchi.
Sababu zipi za kunishawishi kumpigia kura Lowassa awe Rais wa awamu ya tano?
Ndugu Masese Nakuunga Mkono sana, Edward ni kiongozi mwenye uamuzi , mtendaji na pia Fisadi (Japo ni mtenda kazi makini lakini hilo lipo) Juu ya ufisadi wake yeye anazitumia hizo pesa nchini na zinasaidi uchumi wetu, kuliko wale walioiba na kuziweka Uswisi. Ninachoogopa Jee tukimpa madaraka, ataendelea na mtindo wa kujilimbikizia mali kufidia alizotumia kuutafuta utawala kwa nguvu ya pesa zetu????
Tabia ya kuwaaminisha watu maneno yasiyokuwa kweli si nzuri. Hivi ni maamuzi gani muhimu yanayohusu nchi aliyafanya Lowassa kama Lowassa? Pia ni jambo la busara kujiuliza mazingira aliyofanya hayo maamuzi. Ni siri ambayo iko wazi kwamba Lowassa alikuwa na mchango mkubwa wa kumuweka JK ikulu na hivyo kama hayo maamuzi magumu aliyafanya rais akiwa huyo swahiba ni vyema tukayaangalia kwa mazingira hayo. Hivi mtu utashindwaje kuonekana una maamuzi kama aliye juu yako una nguvu juu yake? Wote munaosema Lowassa ana maamuzi magumu hebu tupe mifano halisi ya maamuzi aliyoyafanya kwa akili yake mwenyewe kama siyo kufuatilia plan za katibu mkuu wake?