Hitaji la Taifa.
Taifa linahitaji kiongozi wa nchi,kiongozi atakaye waunganisha watanzania nakuendeleza pale alipoishia Mh.wetu Jakaya,
Nchi inahitaji mtu mmoja,mtu atakaye aminiwa akisema,kiongozi atakaye jua na anayejua mahitaji ya wakati ya nchi katika zama hizi za ushindani wa kiuchumi,Huyu lazima alete matumaini kwa maskini katika sekta za Elimu, Afya,Kilimo na uzalishaji katika viwanda,huyu lazima awe na mikakati katika kufufua ajira na kupata masoko.
Nchi haihitaji kupewa Malaika wasio na mabawaa kuongoza,Bali kiongozi mwenye njozi hata akiwa na mapungufu akubali kuwa chini ya kivuli cha Mungu wa Abrahamu,
Rais atakayejua umoja na amani ni matokeo ya Haki kwa wananchi,Rais atakajua raalimali zetu ni Amana na akiba ya kuweka kukopa katika Dunia na kuinua uchumi wa nchi,
Kiongozi atakayefufua reli ya kati na kupunguza gharama za kuharibu Barbara,Rais atakaye saidia walimu kupata nyumba za kuishi,kutoa uhakika wa madawati kwa watoto wa maskini na kuwalipa walimu mishahara bora Polisi na vyombo vya ulinzi na usalama kupata makazi bora na masirahi zaidi.
Nchi inahitaji kiongozi mwenye maono kutoka hapa alipojitahidi Jakaya,
Rais wa nchi lazima awe na agenda kwa nchi,hawezi kuambiwa ndani ya miezi minne aongoze watu na nnchi,lazima yeye awe na nia binafsi ya kiutumishi na maono kwa kuivusha nchi katika bahari ya Shamu,
Huyu hawezi kuwa wa kikundi cha watu wachache kwa maslahi ya wachache,huyu atajulikana kwa matendo na mwitikio kwa umma,
Huyu lazima awe na huruma kwa watu miln 45,lazima ajue marafiki wakimsaidia akashinda wampe Uhuru wa kimkakati kulitumikia Taifa na kuleta matumaini mapya,
Rais huyu lazima ajue Mungu ni mtawala wa mbingu na nchi akubali maongozo ya kimbingu katika kuikataa laana katika nchi apewayo na Bwana Mungu wake,
Ndugu zangu huyu si mwingine ni huyu mzalendo,Edward Ngoyai Lowassa kiongozi mvumilivu na mstahimilivu,kiongozi akiyejivika ukondoo kulinda umoja wa nchi,kiongozi aliyevumilia dhihaka na kubali mwaminifu kwa chama chake,CCM leo ingekua na hofu ya Mungu huyu angetunukiwa tuzo ya mapenz na uaminifu katika chama,huyu angepewa heshima kwa kunyamaza kimya alipoimbwa kila kona ya nchi kuwa hafai,
Kama si huruma zako Mungu sisi tungeangamia Okoa nchi yetu Mungu
Edward tunakuhitaji si kwa faida yetu,lakini kwa matumani mapya kwa mama mpika mandazi juu ya Elimu ya mtoto wake,
Mungu wa Isac na Yacob yule aliyegeuza bahari kufanya njia wakati wayahudi nyuma walifuatwa na magari ya farao yakiwa na silaha nzito,pembeni mwao ilikua milima mirefu ambayo ilijaaa wanyama wakali na mbele bahari,hata lile wingu lililokua likiwapa matumaini siku farao anawafuata lilitoweka wakakata tamaa,Mungu alimuuliza Musa unanini mkononi,akaambiwa inua fimbo yako ukayapige maji,
Lowassa unanini mkononi tunajua unawatu waliokupa Imani waambie watu wako tuvuke daraja sasa.
Long live Tanzania
Uu Goshem ya Afrika EL2015 may5