Waziri Mkuu msataafu na mbunge wa monduli amedhihirisha kuwa ana hazina kubwa ya vijana wakina mama na hata wapinzani katika siasa za Tanzania.
Ikiwa Edward Lowassa amesimamishwa na kamati ya maadili ya chama cha mapinduzi vijana wapatao elfu moja walijitokeza chini ya utaratibu wa vuguvugu lao la mabadiliko linalo amini mabadiliko huanzia kwa mtu mmoja (
4U Movement | FRIENDS OF LOWASSA).
Hata hivyo nilipo wadadisi vijana hao kuwa labda mmetumwa au lava , walijinasibu kuwa wao wapo tayari si kusapoti chama bali uongozi utakao kuwa unafuata misingi mikuu minne yaani UTUMISHI, UWAJIBIKAJI, UMOJA NA UZALENDO ambavyo wanaamini Edward anavitekeleza na ndio Kiu yao ya kumsaport.
Nilikwenda mbali kuwahoji kuwa hamhofii chama kitamuadhibu kufanya kampeni kama walivyo msimamisha?? Basi majibu yao yalikuwa hivi wao ni marafiki na mashabiki wa Lowassa na aliezuiwa ni Lowassa na kamati ya mangula , na wao kama watanzania wana Uhuru wakupendekeza na kushawishi kiongozi wamtakaye na hakuna wakuwazuia kwani ni Uhuru wakikatiba wanautumia.
Basi namimi kunufanya kuamini huu ni wakati wa Lowassa wenye MAAMUZI NA MATUMAINI MAPYA KWA WATANZANIA WOTE.
hakika Lowassa hakamatiki, Hazuiliki, haepukiki , Chama cha mapinduzi kuvuna mbivu au mbichi.