Kwa lipi Lowassa apewe nchi?

Kwa lipi Lowassa apewe nchi?

Ukiwa na mawazo ya busara huitaji mtu kuyapandisha paan ili wengine wayaone, taifa taifa c chumba cha dada zako,kama ni mmasai mwezio cc hatuujui huo umasai tunaitaj yle watanzania wanaitaj sio wamasai
 
kweli lowasa ni shujaa na anakublika kwa watanzania wenye akili timamu lakn wale wanafiki wanamsengenya sana,acheni sentesi zenye kukengeusha kwa watanzania
 
wote tutasema lakin watazania watahukumu nan? apewe dhamana ya nchi yetu,hilo tusubl uchaguzi,
 
kweli lowasa ni shujaa na anakublika kwa watanzania wenye akili timamu lakn wale wanafiki wanamsengenya sana,acheni sentesi zenye kukengeusha kwa watanzania

Shida ya watz wanaopenda mipira ya kona hawawez kumkubal EL kwasababu wanaamini akirudi mtandaoni mirija itakatwa, na ndiomaana hatapalipo pachafu wanafunika shela la harusi badala la ya sanda.
 

Bw.Lowasa hapewi Nchi bali anachukua Nchi!


Kuchukua nchi ni kupindua na kupata madaraka kimabavu. Ndio njia pekee EL atapata urais.
Hivi nani kasema lazima awe rais? Over our dead bodies kupata urais.
 
Kichefuchefu. Labda rais wa ukoo wake.
 
Kwa hili hapa lowasa apewe.
 

Attachments

  • 1418122156535.jpg
    1418122156535.jpg
    43 KB · Views: 135
Nikukumbushe ameuliza swali zuri sana.nashukuru watanzania tumeanza kufunguka macho kuwa inabidi rais ajaye awe imara kupiga vita ufisadi na rushwa. Tukiendelea hivi nchi itaangamia.
Kwa sasa bahati mbaya lowasa hana sifa hiyo.track record yake inamshtaki.pia amezungukwa na wezi, wakwepa kodi na wafanya magendo.hawa wote wanampa y pesa zao ili akichukua urais waibe, wakwepe kodi, wauze madawa ya kulevya na y nk.haya mambo ndugu zangu sio masuala ya ushabiki, ni masuala mazito yanayohusu mustakabali wa nchi yetu.tusipokuwa makini tutaangamia. Hivyo ushauri wangu kwa wana jamiiforum,tunapotafakari nani ndiye rais ajaye tuache ushabiki wa kitoto...ushabiki huo ndio unaiponza nchi yetu mpaka sasa.
Kama mtu umepata bajaría que ya kuwa kwenye hizo kambi zinazomwaga mapesa, chukua kama alivyoshairi sumaye.lakini acha kupigia kampeni ufisadi halafu fedha za escrow zikitafunwa y unalia. Kumpigia kampeni lowasa ni kuwasifu wezi na y wabadhirifu wa mali ya umma.ni sawasawa na kuunga mkono ufisadi. Ndugu zangu, tuamke.tuache kutumiwa halafu tunacheka kama mazuzu wakati ndugu zetu wanakufa njaa vijijini.
 
Tunamuogopa sisi lkn hatuna sababu ya kumuogopa kwa sababu haogopeshi mtu ni sisi tu ndiyo tunaogopa kwa sababu ni waoga wa kuwa na kiongozi mwenye uwezo wa kuwaambia wapambe kuwa ikuru ni sehemu takatifu. Tusimuogope E. Lowasa 2015
 
Ningetamani sana rais wa awamu ya tano asitokee CCM kwani hakuna msafi hata mtoto mdogo aliyezaliwa kwenye familia ya mwanachama wa CCM.
Wote ndani ya CCM ni tumbili wanakula mahindi ya nchi hii.

Ukisikia tumbili wanagombana usije ukafikiri kwamba wanakemeana wasiibe mahindi bali ujue wanagombania mahindi.

Ikitokea kwa bahati mbaya hii nchi ikabaki chini ya pori la tumbili hawa CCM basi Lowassa anaweza akatumia kushiba kwake na kuwadhibiti tumbili wanaojiandaa kuvamia shamba na njaa zao wakitamani kushiba kama Lowassa.

Fisadi au tumbili mwingine anyeweza ni Pombe Magufuli.Huyu naye ni fisadi mchapa kazi sio kilaza.

Watanzania tusirubunike ndani ya CCM hakuna cha mlokole wala ustadhi wote lao ni moja, kula na kuiba mali za Umma tu huku ubunifu wao ukiwa ziro.

Ukitaka kujua kama CCM wote ni kitu kimoja kumbuka walichofanya Dodoma kwenye Bunge Maalumu la Katiba. Hakuna waziri au mbunge wa CCM aliyesimama na kutetea makosa makubwa ya uchakachuaji wa mawazo ya wananchi. Tusitegemee jipya kutoka mgombea wa uraisi kutoka CCM kama akichaguliwa kwenye kiti cha uraisi 2015. Hakuna sijui EL, sijui Membe, sijui Wassira, sijui Pinda, sijui J. Makamba wote hawa ni kitu kimoja! Tafakari. .....
 
Yatakuwa yale yale ya Tibaijuka,BMK walipitisha wao kwa kuona kwamba,waziri lazima atokane na wabunge leo hii anapinga mbunge kuwa waziri kwa kuwa amefukuzwa uwaziri.
Ukitaka kujua kama CCM wote ni kitu kimoja kumbuka walichofanya Dodoma kwenye Bunge Maalumu la Katiba. Hakuna waziri au mbunge wa CCM aliyesimama na kutetea makosa makubwa ya uchakachuaji wa mawazo ya wananchi. Tusitegemee jipya kutoka mgombea wa uraisi kutoka CCM kama akichaguliwa kwenye kiti cha uraisi 2015. Hakuna sijui EL, sijui Membe, sijui Wassira, sijui Pinda, sijui J. Makamba wote hawa ni kitu kimoja! Tafakari. .....
 
Back
Top Bottom