Jobless nipo Mitaa ya Kanyenye hapa,Maisha yanatisha Usawa unakaba.
Hali ni ngumu napata mawazo kibao ninadamu ya kunguni.
Harakati kibao bado Ulimwengu unataka kunimeza,Ulimwengu hauna huruma.
Nakumbuka siku moja natoka kanyenye nakwenda Isevya (TBR) mida ya jioni mawazo lukuki ghafla nikajikuta nimepiga magoti chini nikainunua mikono Juu nikanena kwa sauti.
"Ulimwengu ndio Mama What'sp Jay Moe"
Wakati mwingine nawaza hivi lini nitakuwa fisadi..? mke na watoto wapate chai safi,gari la kifahari na jumba la kifahari kama ofisi ya serikali.Mawazo ya kifisadi-fisadi.
Nigga nimestay broke Marafiki wanafiki wakichekelea full shangwe kama Fiesta,Wananichekea machoni kisogoni wananisema.
Maisha ni vita, kidume napambana,Kukata tamaa Mwiko.
Dunia ni gunia na gunia halibebi Maji.