Kwa jinsi Waziri wa Afya alivyokuwa na maono, kinachofuata ni kuongeza makato kwa wachangiaji

Mzalendo Uchwara

JF-Expert Member
Jan 26, 2020
3,718
11,708
Hili la NHIF na hospitali binafsi limeonesha uwezo mdogo wa kutatua matatizo alionao waziri wa afya pamoja na huyo bosi wa NHIF.

NHIF ina changamoto kuu mbili

1. Matumizi makubwa ya fedha kwa shughuli za kuendesha ofisi, hata ripoti za CAG zimeonesha namna wanavyotumia fedha hovyo.

2. Udanganyifu wa watoa huduma za afya.

Sasa jawabu walilokuja nalo ni kulazimisha kupunguza bei za huduma za afya jambo ambalo halina uhalisia.

Kwa jinsi walivyo wavivu wa kufikiri, likiwashinda hili basi watakimbilia kuongeza asilimia ya makato kwa wachangiaji.

Mara zote wanakombilia majibu rahisi kwenye changamoto ngumu za kimfumo.

SSH aache kulea uzembe, Waziri kazi imemshinda, aletwe mtu mwingine. Kwani Dr. Gwajima alikuwa na shida gani?
 
Hili la NHIF na hospitali binafsi limeonesha uwezo mdogo wa kutatua matatizo alionao waziri wa afya pamoja na huyo bosi wa NHIF.

NHIF ina changamoto kuu mbili

1. Matumizi makubwa ya fedha kwa shughuli za kuendesha ofisi, hata ripoti za CAG zimeonesha namna wanavyotumia fedha hovyo.

2. Udanganyifu wa watoa huduma za afya.

Sasa jawabu walilokuja nalo ni kulazimisha kupunguza bei za huduma za afya jambo ambalo halina uhalisia.

Kwa jinsi walivyo wavivu wa kufikiri, likiwashinda hili basi watakimbilia kuongeza asilimia ya makato kwa wachangiaji.

Mara zote wanakombilia majibu rahisi kwenye changamoto ngumu za kimfumo.

SSH aache kulea uzembe, Waziri kazi imemshinda, aletwe mtu mwingine. Kwani Dr. Gwajima alikuwa na shida gani?
Dr Gwajima na Dr Hussein Mwinyi ndiyo pekee waliyo iweza hiyo wizara
 
Hapo hamna zaidi ya wanachama kulipishwa mamilioni tu😂 nachokiona wangejenga hospitali zao wenyewe tu kama kuwalipa bill wenye hospitali binafsi inakuwa ngumu
 
Hakuna Sector iliyosaidia Serikali kutoa Afya Kwa Wananchi kama Private hospitals. Huduma zao zilindwe na kuheshimiwa. Hivi mlishawahi kuumwa ukaenda Amana au Temeke au mwananyamala? Huko maybe Wana Huduma nzuri Kwa Martenal Health tuu. Msongamano mkubwa Daktari anakulipua ahudumie Wengine. Vipimo hakuna au mmejazana hukoo hadi Usiku. Afya ilindwe Wananchi waendelee kupata Huduma wanapotaka.
 
Sasa mbona umesema ana maono? Au mimi ndio sielewi kiswahili? Nilipoona kichwa cha habari nikastuka kama kuna mtu anaweza akamtetea Ummy kwenye hili
Nikwamba wametutikisa kwa sinema iliyotungwa, sasa watakuja na hoja ya kuongeza asilimia kwenye makato ya wafanyakazi.
Kwamba gharama za vifaa tiba zimepanda.
 
Dr Gwajima na Dr Hussein Mwinyi ndiyo pekee waliyo iweza hiyo wizara
Hao wote ni magarasa matupu.
Mwinyi alishindwa kutatua mgomo mkubwa wa madaktari, Gwajima aliishia kufukiza watu madawa ya kienyeji ili kutibu Corona.

Kwangu mimi, Ummy Mwalimu amewaacha hao wengine (Gwajima, Mwinyi) mbali sana, yule mother ni msikivu mnoo na amekuwa calm kwenda na beats za wataalamu wa Afya, hili la NHIF la sasa ni changamoto kubwa kwake kwa sababu lipo nje ya uwezo wake wa kimaamuzi, ni mpango wa maazimio uliopitia kwenye baraza la mawaziri (Samia, Mpango, Majaliwa na Mwigulu wanalijua vyema), ulikuwa ni uamuzi wa kipuuzi uliofanywa ili kuunusuru mfuko wa NHIF unaoelekea kufa.

Mpaka sasa, waziri pekee aliyefanya reform kubwa na nzuri kwenye sekta ya afya na kutuliza mawimbi yote ya misukosuko ni Professor Mwakyusa. Kile kichwa ni akili mingi sana.
 
Sasa mbona umesema ana maono? Au mimi ndio sielewi kiswahili? Nilipoona kichwa cha habari nikastuka kama kuna mtu anaweza akamtetea Ummy kwenye hili
Hili tatizo la "a" badala ya "h" na la "h" badala ya "a" , ni kubwa kuliko BAKITA wanavyoweza kufikiria.
 
Na hiki ndicho kilichokuwa kinatafutwa..it was just a calculated move.
Makato kwa wafanyakazi/watumishi lazima yaongezeke.
 
Hili la NHIF na hospitali binafsi limeonesha uwezo mdogo wa kutatua matatizo alionao waziri wa afya pamoja na huyo bosi wa NHIF.

NHIF ina changamoto kuu mbili

1. Matumizi makubwa ya fedha kwa shughuli za kuendesha ofisi, hata ripoti za CAG zimeonesha namna wanavyotumia fedha hovyo.

2. Udanganyifu wa watoa huduma za afya.

Sasa jawabu walilokuja nalo ni kulazimisha kupunguza bei za huduma za afya jambo ambalo halina uhalisia.

Kwa jinsi walivyo wavivu wa kufikiri, likiwashinda hili basi watakimbilia kuongeza asilimia ya makato kwa wachangiaji.

Mara zote wanakombilia majibu rahisi kwenye changamoto ngumu za kimfumo.

SSH aache kulea uzembe, Waziri kazi imemshinda, aletwe mtu mwingine. Kwani Dr. Gwajima alikuwa na shida gani?
ni shosti yake usitegemee chochote
 
Back
Top Bottom