NHIF kaeni mbali na mchakato wa utekelezaji wa bima ya Afya kwa wote

jingalao

JF-Expert Member
Oct 12, 2011
35,053
28,245
Wasalaamu wanaJF

Herini ya Krismasi na maandalizi ya funga mwaka 2023.

Leo tena ninarudi jamvini nikija na ushauri kuntu kwa wizara zote zinazohusika na afya pamoja na wadau wa sekta ya afya.

Utambulisho
Nirejee kwa kujitambulisha kuwa kwa miaka kadhaa kama raia, mwanaJF, mdau wa maswala ya siasa, mdau wa maswala yanayolalamikiwa na wananchi, mdau wa Sera mbalimbali za nchi, mdau katika sekta ya afya ,mdau wa bima ya afya kwa wote,mdau wa afya ya msingi kwa wote, mdau korofi wa kuona Tanzania inajitegemea katika maswala ya afya lakini pia mzalendo asiye na simile/smile inapokuja suala la uhuru kamili wa Tanzania bila msaada wa walami.

#MWANZO WA HOJA YANGU#
Wakati tunapata uhuru mwalimu Nyerere alitupa muelekeo wa kupambana na maadui watatu muhimu ikiwemo Ujinga,maradhi na umasikini.

Hadi leo bado kama nchi tunayo dira,mipango na mikakati dhidi ya maadui hawa watatu. Kwa kiasi kikubwa Serikali, viongozi wa siasa na jamii wameshirikiana na wananchi katika kukabiliana na maadui hawa kwa ufanisi mkubwa na KAZI INAENDELEA.

Nikijikita katika adui maradhi ni wazi kuwa kumekuwepo na Mabadiliko muhimu mbalimbali yaliyoashiria utekelezaji wenye matokeo.Zaidi tumejionea utekelezaji mkubwa wa kimatokeo hususani katika kipindi cha miaka 7 ya hivi karibuni japo mabadiliko hayo hayana msingi au egemeo la kisiasa(kisera), nasema hivi kwa kuwa bado tuna sera ya afya ya mwaka 2007 mwezi juni.

Kwa muktadha huu tunaweza kuwa tumepiga hatua kubwa bila kuwa na idhini au baraka za kisera. Aidha natambua kuwa Tuna sheria iliyoanzisha mfuko wa bima ya afya ya Taifa (NHIF) kama sikosei ilianza 1999 na marekebisho yaliyofanyika mara kwa mara. Kama nikirejea sawasawa mojawapo ya majukumu ya chombo hiki (kumbukumbu zangu tu zinaniambia niliwahi kusoma sehemu) ni kusimamia utekelezaji wa bima ya afya kwa wote.

Pia niseme kwa maoni yangu kuwa moja ya jukumu la NHIF la kuikuza bima ya afya kwa wote lilishindwa kutekelezwa hadi tukafikia hatua ya wadau wengine au vyombo vingine kuingilia kati.

Nirejee kuipongeza Serikali chini ya Wizara ya Afya na OR TAMISEMI kufikia hatua kubwa ambayo imepelekea kuwa na Sheria ya bima ya afya kwa wote hivi karibuni ambayo inasubiri kutengenezewa kanuni.

VURUGU ZA NHIF KWA SASA
Wakati wadau, wizara za kisekta na za utekekezaji, wanufaika na wananchi wakisubiri maekelekezo mujarabu ya utekelezaji wa sheria ya bima ya afya kwa wote naona NHIF wakijitoa ufahamu iwe kwa kupangwa au kwa kupotoka au vyovyote vile wakiibua sintofahamu katika jamii. Yaani wameibuka na Price list ya huduma watakazogharamia kwa level mbalimbali za huduma bila kuwashirikisha wadau hususani wa afya na wanaotoa huduma za afya.

Kwangu mimi hii naona ni vurugu na pengine ni hujuma dhidi ya sheria hii iliyopita kwa shida na mashaka mengi.
kuna kipindi niliwalaumu waheshimiwa wabunge walivyokataa kuipitisha ila kwa sasa nawaelewa kwa nini walikuwa na mashaka!pengine walipata hisia chafu ya kutengwa kwa mwananchi wa kawaida katika utekelezwaji wa sheria hii.

MAONI NA USHAURI WANGU KWA NHIF/WIZARA YA KISEKTA
-Kwanza kabisa NHIF ijiondoshe na kujiepusha kimkakati (strategic retreate) katika utekelezaji wa mchakato wa bima ya afya kwa wote.NHIF ijiweke kama mdau anayetakiwa kupangwa na kupangiwa katika utekelezaji wa sheria hii mpya, sio kwa ubaya bali kwa maslahi mapana ya wanufaika wote.
-Utungaji wa kanuni na mchakato wake usimamiwe na wizara ya Afya kwa kushirikisha kikamilifu Ofisi ya Rais Tamisemi, Ofisi ya Waziri Mkuu,Wizara mtambuka, Mikoa na Halmashauri sekta binafsi, bunge na jamii kwa ujumla.

Hapa namaanisha USHIRIKISHAJI KAMILIFU na sio semina za kisanii.

-NHIF isitishe michakato yake ya price list inayotarajiwa kuanza mwezi januari 2024 ambayo inakiuka mikataba waliyoingia na watoa huduma ...hii inaangazia na kuakisi maswala ya kibajeti na kisheria ya taasisi mbalimbali ambazo ziliingia mikataba na NHIF.

-Wadau wote wanaohusika waratibiwe kuandaa mapendekezo (yawe kimaandishi) ili yawasilishwe kwa wizara ya afya ili kuunda kanuni za utekelezaji wa sheria ya bima ya afya.
-Ni vyema na ikibidi wizara ya Afya ipeleke bungeni kanuni hizo kwa maridhiano kamilifu ya utekekezaji.

-Wizara ya Afya itambue kuwa Afya kwa kiasi kikubwa inaanzia ngazi ya jamii,zahanati,vituo vya afya ,hospitali za wilaya halafu ndio hospitali za mikoa, kanda na kitaifa.wadau muhimu wa afya wapo ngazi ya msingi na sio ngazi ya rufaa. Wananchi na wagonjwa zaidi ya 80% wanaanzia au wanafaidika na afya ya msingi na sio vinginevyo.

Heri ya Krismasi na mwaka mpya.

KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA!
 
Nhif hawana uhalali they will take thirr own death. They're working for the government. It means its irrelevant
 
Upo 👌🏽👌🏽👌🏽
Hiyo ya ujinga huwa sielewi y imejaa % kubwa ya wananchi hata uongozini .. kwa siku hizi wivu na tamaa vinaleta majanga nchini pia.
 
Wasalaamu wanaJF !
Herini ya Krismasi na maandalizi ya funga mwaka 2023.
Leo tena ninarudi jamvini nikija na ushauri kuntu kwa wizara zote zinazohusika na afya pamoja na wadau wa sekta ya afya.
Utambulisho
Nirejee kwa kujitambulisha kuwa kwa miaka kadhaa kama raia ,mwanaJF,mdau wa maswala ya siasa,mdau wa maswala yanayolalamikiwa na wananchi ,mdau wa Sera mbalimbali za nchi ,mdau katika sekta ya afya ,mdau wa bima ya afya kwa wote,mdau wa afya ya msingi kwa wote,mdau korofi wa kuona Tanzania inajitegemea katika maswala ya afya lakini pia mzalendo asiye na simila inapokuja suala la uhuru kamili wa Tanzania bila msaada wa walami.

#MWANZO WA HOJA YANGU#
Wakati tunapata uhuru mwalimu Nyerere alitupa muelekeo wa kupambana na maadui watatu muhimu ikiwemo Ujinga,maradhi na umasikini.
Hadi leo bado kama nchi tunayo dira,mipango na mikakati dhidi ya maadui hawa watatu.
Kwa kiasi kikubwa Serikali ,viongozi wa siasa na jamii wameshirikiana na wananchi katika kukabiliana na maadui hawa kwa ufanisi mkubwa na KAZI INAENDELEA.
Nikijikita katika adui maradhi ni wazi kuwa kumekuwepo na Mabadiliko muhimu mbalimbali yaliyoashiria utekekezaji wenye matokeo.Zaidi tumejionea utekekezaji mkubwa wa kimatokeo hususani katika kipindi cha miaka 7 ya hivi karibuni japo mabadiliko hayo hayana msingi au egemeo la kisiasa(kisera) ...nasema hivi kwa kuwa bado tuna sera ya afya ya mwaka 2007 mwezi juni.
Kwa muktadha huu tunaweza kuwa tumepiga hatua kubwa bila kuwa na idhini au baraka za kisera.
Aidha natambua kuwa Tuna sheria iliyoanzisha mfuko wa bima ya afya ya Taifa (NHIF) kama sikosei ilianza 1999 na marekebisho yaliyofanyika mara kwa mara.Kama nikirejea sawasawa mojawapo ya majukumu ya chombo hiki (kumbukumbu zangu tu zinaniambia niliwahi kusoma sehemu) ni kusimamia utekelezaji wa bima ya afya kwa wote.
Pia niseme kwa maoni yangu kuwa moja ya jukumu la NHIF la kuikuza bima ya afya kwa wote lilishindwa kutekelezwa hadi tukafikia hatua ya wadau wengine au vyombo vingine kuingilia kati.

Nirejee kuipongeza Serikali chini ya Wizara ya Afya na OR TAMISEMI kufikia hatua kubwa ambayo imepelekea kuwa na Sheria ya bima ya afya kwa wote hivi karibuni ambayo inasubiri kutengenezewa kanuni.

#VURUGU ZA NHIF KWA SASA#
Wakati wadau ,wizara za kisekta na za utekekezaji ,wanufaika na wananchi wakisubiri maekelekezo mujarabu ya utekelezaji wa sheria ya bima ya afya kwa wote naona NHIF wakijitoa ufahamu iwe kwa kupangwa au kwa kupotoka au vyovyote vile wakiibua sintofahamu katika jamii.yaani wameibuka na Price list ya huduma watakazogharamia kwa level mbalimbali za huduma bila kuwashirikisha wadau hususani wa afya na wanaotoa huduma za afya.
Kwangu mimi hii naona ni vurugu na pengine ni hujuma dhidi ya sheria hii iliyopita kwa shida na mashaka mengi.
kuna kipindi niliwalaumu waheshimiwa wabunge walivyokataa kuipitisha ila kwa sasa nawaelewa kwa nini walikuwa na mashaka!pengine walipata hisia chafu ya kutengwa kwa mwananchi wa kawaida katika utekelezwaji wa sheria hii.

#MAONI NA USHAURI WANGU KWA NHIF/WIZARA YA KISEKTA#
-Kwanza kabisa NHIF ijiondoshe na kujiepusha kimkakati (strategic retreate) katika utekelezaji wa mchakato wa bima ya afya kwa wote.NHIF ijiweke kama mdau anayetakiwa kupangwa na kupangiwa katika utekelezaji wa sheria hii mpya...sio kwa ubaya bali kwa maslahi mapana ya wanufaika wote.
-Utungaji wa kanuni na mchakato wake usimamiwe na wizara ya Afya kwa kushirikisha kikamilifu Ofisi ya Rais Tamisemi, Ofisi ya Waziri Mkuu,Wizara mtambuka,Mikoa na Halmashauri ,sekta binafsi ,bunge na jamii kwa ujumla.
Hapa namaanisha USHIRIKISHAJI KAMILIFU na sio semina za kisanii.
-NHIF isitishe michakato yake ya price list inayotarajiwa kuanza mwezi januari 2024 ambayo inakiuka mikataba waliyoingia na watoa huduma ...hii inaangazia na kuakisi maswala ya kibajeti na kisheria ya taasisi mbalimbali ambazo ziliingia mikataba na NHIF.
-Wadau wote wanaohusika waratibiwe kuandaa mapendekezo (yawe kimaandishi) ili yawasilishwe kwa wizara ya afya ili kuunda kanuni za utekelezaji wa sheria ya bima ya afya.
-Ni vyema na ikibidi wizara ya Afya ipeleke bungeni kanuni hizo kwa maridhiano kamilifu ya utekekezaji.
-Wizara ya Afya itambue kuwa Afya kwa kiasi kikubwa inaanzia ngazi ya jamii,zahanati,vituo vya afya ,hospitali za wilaya ..halafu ndio hospitali za mikoa,kanda na kitaifa.wadau muhimu wa afya wapo ngazi ya msingi na sio ngazi ya rufaa.wananchi na wagonjwa zaidi ya 80% wanaanzia au wanafaidika na afya ya msingi na sio vinginevyo.

Heri ya Krismasi na mwaka mpya.

KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA!!!
Hoja imeungwa mkono. Ikibidi tuanze upya na chombo kipya cha kusimamia huduma hii muhimu!
 
Wasalaamu wanaJF !
Herini ya Krismasi na maandalizi ya funga mwaka 2023.
Leo tena ninarudi jamvini nikija na ushauri kuntu kwa wizara zote zinazohusika na afya pamoja na wadau wa sekta ya afya.
Utambulisho
Nirejee kwa kujitambulisha kuwa kwa miaka kadhaa kama raia ,mwanaJF,mdau wa maswala ya siasa,mdau wa maswala yanayolalamikiwa na wananchi ,mdau wa Sera mbalimbali za nchi ,mdau katika sekta ya afya ,mdau wa bima ya afya kwa wote,mdau wa afya ya msingi kwa wote,mdau korofi wa kuona Tanzania inajitegemea katika maswala ya afya lakini pia mzalendo asiye na simila inapokuja suala la uhuru kamili wa Tanzania bila msaada wa walami.

#MWANZO WA HOJA YANGU#
Wakati tunapata uhuru mwalimu Nyerere alitupa muelekeo wa kupambana na maadui watatu muhimu ikiwemo Ujinga,maradhi na umasikini.
Hadi leo bado kama nchi tunayo dira,mipango na mikakati dhidi ya maadui hawa watatu.
Kwa kiasi kikubwa Serikali ,viongozi wa siasa na jamii wameshirikiana na wananchi katika kukabiliana na maadui hawa kwa ufanisi mkubwa na KAZI INAENDELEA.
Nikijikita katika adui maradhi ni wazi kuwa kumekuwepo na Mabadiliko muhimu mbalimbali yaliyoashiria utekekezaji wenye matokeo.Zaidi tumejionea utekekezaji mkubwa wa kimatokeo hususani katika kipindi cha miaka 7 ya hivi karibuni japo mabadiliko hayo hayana msingi au egemeo la kisiasa(kisera) ...nasema hivi kwa kuwa bado tuna sera ya afya ya mwaka 2007 mwezi juni.
Kwa muktadha huu tunaweza kuwa tumepiga hatua kubwa bila kuwa na idhini au baraka za kisera.
Aidha natambua kuwa Tuna sheria iliyoanzisha mfuko wa bima ya afya ya Taifa (NHIF) kama sikosei ilianza 1999 na marekebisho yaliyofanyika mara kwa mara.Kama nikirejea sawasawa mojawapo ya majukumu ya chombo hiki (kumbukumbu zangu tu zinaniambia niliwahi kusoma sehemu) ni kusimamia utekelezaji wa bima ya afya kwa wote.
Pia niseme kwa maoni yangu kuwa moja ya jukumu la NHIF la kuikuza bima ya afya kwa wote lilishindwa kutekelezwa hadi tukafikia hatua ya wadau wengine au vyombo vingine kuingilia kati.

Nirejee kuipongeza Serikali chini ya Wizara ya Afya na OR TAMISEMI kufikia hatua kubwa ambayo imepelekea kuwa na Sheria ya bima ya afya kwa wote hivi karibuni ambayo inasubiri kutengenezewa kanuni.

#VURUGU ZA NHIF KWA SASA#
Wakati wadau ,wizara za kisekta na za utekekezaji ,wanufaika na wananchi wakisubiri maekelekezo mujarabu ya utekelezaji wa sheria ya bima ya afya kwa wote naona NHIF wakijitoa ufahamu iwe kwa kupangwa au kwa kupotoka au vyovyote vile wakiibua sintofahamu katika jamii.yaani wameibuka na Price list ya huduma watakazogharamia kwa level mbalimbali za huduma bila kuwashirikisha wadau hususani wa afya na wanaotoa huduma za afya.
Kwangu mimi hii naona ni vurugu na pengine ni hujuma dhidi ya sheria hii iliyopita kwa shida na mashaka mengi.
kuna kipindi niliwalaumu waheshimiwa wabunge walivyokataa kuipitisha ila kwa sasa nawaelewa kwa nini walikuwa na mashaka!pengine walipata hisia chafu ya kutengwa kwa mwananchi wa kawaida katika utekelezwaji wa sheria hii.

#MAONI NA USHAURI WANGU KWA NHIF/WIZARA YA KISEKTA#
-Kwanza kabisa NHIF ijiondoshe na kujiepusha kimkakati (strategic retreate) katika utekelezaji wa mchakato wa bima ya afya kwa wote.NHIF ijiweke kama mdau anayetakiwa kupangwa na kupangiwa katika utekelezaji wa sheria hii mpya...sio kwa ubaya bali kwa maslahi mapana ya wanufaika wote.
-Utungaji wa kanuni na mchakato wake usimamiwe na wizara ya Afya kwa kushirikisha kikamilifu Ofisi ya Rais Tamisemi, Ofisi ya Waziri Mkuu,Wizara mtambuka,Mikoa na Halmashauri ,sekta binafsi ,bunge na jamii kwa ujumla.
Hapa namaanisha USHIRIKISHAJI KAMILIFU na sio semina za kisanii.
-NHIF isitishe michakato yake ya price list inayotarajiwa kuanza mwezi januari 2024 ambayo inakiuka mikataba waliyoingia na watoa huduma ...hii inaangazia na kuakisi maswala ya kibajeti na kisheria ya taasisi mbalimbali ambazo ziliingia mikataba na NHIF.
-Wadau wote wanaohusika waratibiwe kuandaa mapendekezo (yawe kimaandishi) ili yawasilishwe kwa wizara ya afya ili kuunda kanuni za utekelezaji wa sheria ya bima ya afya.
-Ni vyema na ikibidi wizara ya Afya ipeleke bungeni kanuni hizo kwa maridhiano kamilifu ya utekekezaji.
-Wizara ya Afya itambue kuwa Afya kwa kiasi kikubwa inaanzia ngazi ya jamii,zahanati,vituo vya afya ,hospitali za wilaya ..halafu ndio hospitali za mikoa,kanda na kitaifa.wadau muhimu wa afya wapo ngazi ya msingi na sio ngazi ya rufaa.wananchi na wagonjwa zaidi ya 80% wanaanzia au wanafaidika na afya ya msingi na sio vinginevyo.

Heri ya Krismasi na mwaka mpya.

KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA!!!
Natumai umeisoma sheria ya bima ya Afya kwawote. Msimamizi si NHIF ni TIRA.
 
Wasalaamu wanaJF !
Herini ya Krismasi na maandalizi ya funga mwaka 2023.
Leo tena ninarudi jamvini nikija na ushauri kuntu kwa wizara zote zinazohusika na afya pamoja na wadau wa sekta ya afya.
Utambulisho
Nirejee kwa kujitambulisha kuwa kwa miaka kadhaa kama raia ,mwanaJF,mdau wa maswala ya siasa,mdau wa maswala yanayolalamikiwa na wananchi ,mdau wa Sera mbalimbali za nchi ,mdau katika sekta ya afya ,mdau wa bima ya afya kwa wote,mdau wa afya ya msingi kwa wote,mdau korofi wa kuona Tanzania inajitegemea katika maswala ya afya lakini pia mzalendo asiye na simila inapokuja suala la uhuru kamili wa Tanzania bila msaada wa walami.

#MWANZO WA HOJA YANGU#
Wakati tunapata uhuru mwalimu Nyerere alitupa muelekeo wa kupambana na maadui watatu muhimu ikiwemo Ujinga,maradhi na umasikini.
Hadi leo bado kama nchi tunayo dira,mipango na mikakati dhidi ya maadui hawa watatu.
Kwa kiasi kikubwa Serikali ,viongozi wa siasa na jamii wameshirikiana na wananchi katika kukabiliana na maadui hawa kwa ufanisi mkubwa na KAZI INAENDELEA.
Nikijikita katika adui maradhi ni wazi kuwa kumekuwepo na Mabadiliko muhimu mbalimbali yaliyoashiria utekekezaji wenye matokeo.Zaidi tumejionea utekekezaji mkubwa wa kimatokeo hususani katika kipindi cha miaka 7 ya hivi karibuni japo mabadiliko hayo hayana msingi au egemeo la kisiasa(kisera) ...nasema hivi kwa kuwa bado tuna sera ya afya ya mwaka 2007 mwezi juni.
Kwa muktadha huu tunaweza kuwa tumepiga hatua kubwa bila kuwa na idhini au baraka za kisera.
Aidha natambua kuwa Tuna sheria iliyoanzisha mfuko wa bima ya afya ya Taifa (NHIF) kama sikosei ilianza 1999 na marekebisho yaliyofanyika mara kwa mara.Kama nikirejea sawasawa mojawapo ya majukumu ya chombo hiki (kumbukumbu zangu tu zinaniambia niliwahi kusoma sehemu) ni kusimamia utekelezaji wa bima ya afya kwa wote.
Pia niseme kwa maoni yangu kuwa moja ya jukumu la NHIF la kuikuza bima ya afya kwa wote lilishindwa kutekelezwa hadi tukafikia hatua ya wadau wengine au vyombo vingine kuingilia kati.

Nirejee kuipongeza Serikali chini ya Wizara ya Afya na OR TAMISEMI kufikia hatua kubwa ambayo imepelekea kuwa na Sheria ya bima ya afya kwa wote hivi karibuni ambayo inasubiri kutengenezewa kanuni.

#VURUGU ZA NHIF KWA SASA#
Wakati wadau ,wizara za kisekta na za utekekezaji ,wanufaika na wananchi wakisubiri maekelekezo mujarabu ya utekelezaji wa sheria ya bima ya afya kwa wote naona NHIF wakijitoa ufahamu iwe kwa kupangwa au kwa kupotoka au vyovyote vile wakiibua sintofahamu katika jamii.yaani wameibuka na Price list ya huduma watakazogharamia kwa level mbalimbali za huduma bila kuwashirikisha wadau hususani wa afya na wanaotoa huduma za afya.
Kwangu mimi hii naona ni vurugu na pengine ni hujuma dhidi ya sheria hii iliyopita kwa shida na mashaka mengi.
kuna kipindi niliwalaumu waheshimiwa wabunge walivyokataa kuipitisha ila kwa sasa nawaelewa kwa nini walikuwa na mashaka!pengine walipata hisia chafu ya kutengwa kwa mwananchi wa kawaida katika utekelezwaji wa sheria hii.

#MAONI NA USHAURI WANGU KWA NHIF/WIZARA YA KISEKTA#
-Kwanza kabisa NHIF ijiondoshe na kujiepusha kimkakati (strategic retreate) katika utekelezaji wa mchakato wa bima ya afya kwa wote.NHIF ijiweke kama mdau anayetakiwa kupangwa na kupangiwa katika utekelezaji wa sheria hii mpya...sio kwa ubaya bali kwa maslahi mapana ya wanufaika wote.
-Utungaji wa kanuni na mchakato wake usimamiwe na wizara ya Afya kwa kushirikisha kikamilifu Ofisi ya Rais Tamisemi, Ofisi ya Waziri Mkuu,Wizara mtambuka,Mikoa na Halmashauri ,sekta binafsi ,bunge na jamii kwa ujumla.
Hapa namaanisha USHIRIKISHAJI KAMILIFU na sio semina za kisanii.
-NHIF isitishe michakato yake ya price list inayotarajiwa kuanza mwezi januari 2024 ambayo inakiuka mikataba waliyoingia na watoa huduma ...hii inaangazia na kuakisi maswala ya kibajeti na kisheria ya taasisi mbalimbali ambazo ziliingia mikataba na NHIF.
-Wadau wote wanaohusika waratibiwe kuandaa mapendekezo (yawe kimaandishi) ili yawasilishwe kwa wizara ya afya ili kuunda kanuni za utekelezaji wa sheria ya bima ya afya.
-Ni vyema na ikibidi wizara ya Afya ipeleke bungeni kanuni hizo kwa maridhiano kamilifu ya utekekezaji.
-Wizara ya Afya itambue kuwa Afya kwa kiasi kikubwa inaanzia ngazi ya jamii,zahanati,vituo vya afya ,hospitali za wilaya ..halafu ndio hospitali za mikoa,kanda na kitaifa.wadau muhimu wa afya wapo ngazi ya msingi na sio ngazi ya rufaa.wananchi na wagonjwa zaidi ya 80% wanaanzia au wanafaidika na afya ya msingi na sio vinginevyo.

Heri ya Krismasi na mwaka mpya.

KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA!!!
Pili usijaribu hata sikumoja kumtetea mtoa huduma kama wewe ni mmoja wa uanachama wa bima yeyote ile. Yeye analengo la kupata faida kupitia afya yako, kwake yeye afya yako ni biashara ndio maana bima zote zinacontrol za hali ya juu kuzidi hata social insurance yaani NHIF. Business oriented insurance usijeiombea ikupate, 50,400/= ni consultation fee ya Bugando ndio umpe halafu akutibie the whole year, thubutu. Hii vita ni bora mwanachama akaiangalia tu, ukiingilia atakayeumia ni wewe, mwenzako anataka pesa nyingi kupitia ugonjwa wako. Atakurudisha hata mara 50 hospitali na akupe dawa ambazo dose yake ni za miezi 3 ila wewe umetumia miaka 2 mfululizo. Baada ya hapo ni dialysis kuelekea kifo chako.
 
Pili usijaribu hata sikumoja kumtetea mtoa huduma kama wewe ni mmoja wa uanachama wa bima yeyote ile. Yeye analengo la kupata faida kupitia afya yako, kwake yeye afya yako ni biashara ndio maana bima zote zinacontrol za hali ya juu kuzidi hata social insurance yaani NHIF. Business oriented insurance usijeiombea ikupate, 50,400/= ni consultation fee ya Bugando ndio umpe halafu akutibie the whole year, thubutu. Hii vita ni bora mwanachama akaiangalia tu, ukiingilia atakayeumia ni wewe, mwenzako anataka pesa nyingi kupitia ugonjwa wako. Atakurudisha hata mara 50 hospitali na akupe dawa ambazo dose yake ni za miezi 3 ila wewe umetumia miaka 2 mfululizo. Baada ya hapo ni dialysis kuelekea kifo chako.
Usichanganye mada mbili hapa...mtoa huduma ni mdau muhimu sana kutetewa na kushirikishwa kikamilifu na sio kisanii.
NHIF haipaswi kupoka mamlaka ya regulatory authorities nyingine.
As of now kulikuwa kuna haja na kiherehere gani cha kuja na mabadiliko haya wakati tukisubiri utekelezaji wa bima ya afya kwa wote?
Nitakupa mfano mdogo tu....
sababu ya kutotambua huduma ya kibingwa ngazi ya Zahanati ni ipi??yaani zahanati ya kule ukerewe ikimualika Janabi kwenda kuwaona wastaafu waliopo kijijini wenye kadi za bima ya Afya kituo husika hakilipwi na NHIF!!!Hii ndio universal health care?kwa muktadha wa mabadiliko haya daktari bingwa wa macho akienda(na kits zake) kumfanyia upasuaji mstaafu aliopo wilayani procedure hiyo hailipwi na NHIF.
unafahamu gharama ya kumtoa mgonjwa Tandahimba na kumpeleka Muhimbili japo tu kufanyiwa operesheni ya kuondosha tezidume?
Mabadiliko haya mmepanga na nani au watu wa wapi?

dunderhead.
 
Usichanganye mada mbili hapa...mtoa huduma ni mdau muhimu sana kutetewa na kushirikishwa kikamilifu na sio kisanii.
NHIF haipaswi kupoka mamlaka ya regulatory authorities nyingine.
As of now kulikuwa kuna haja na kiherehere gani cha kuja na mabadiliko haya wakati tukisubiri utekelezaji wa bima ya afya kwa wote?
Nitakupa mfano mdogo tu....
sababu ya kutotambua huduma ya kibingwa ngazi ya Zahanati ni ipi??yaani zahanati ya kule ukerewe ikimualika Janabi kwenda kuwaona wastaafu waliopo kijijini wenye kadi za bima ya Afya kituo husika hakilipwi na NHIF!!!Hii ndio universal health care?kwa muktadha wa mabadiliko haya daktari bingwa wa macho akienda(na kits zake) kumfanyia upasuaji mstaafu aliopo wilayani procedure hiyo hailipwi na NHIF.
unafahamu gharama ya kumtoa mgonjwa Tandahimba na kumpeleka Muhimbili japo tu kufanyiwa operesheni ya kuondosha tezidume?
Mabadiliko haya mmepanga na nani au watu wa wapi?

dunderhead.
Boss unaijua miongozo yote ya afya, ukishaisoma IKAMA ndio utajua bado afya huijui. Chief, daktari kabla ya kuwa daktari bingwa anaanza na MD, services anazotoa zote prof Kahamba akiwa Tandahimba ni as a GP not a specialist. Job description ya specialist na list of resources with investigations to be carried out at district level yaani hospitali za wilaya kutokana na muongozo wa maabara (tafuta upo) ni GP level sio specialist level ndio maana kwa muongozo wa watumishi wa afya (IKAMA) daktari bingwa hatambuliki hospitali za wilaya kushuka ngazi ya chini. Miongozo hiyo haikutungwa na NHIF bali wizara ya afya. Pia kitita hichi cha mafao hutolewa na maamuzi ya wizara sio NHIF maana hiyo taasisi ipo chini ya wizara ya afya. Afya sio mihemuko, inamiongozo ambayo nikikutajia hutaiweza ijua mpaka kesho.
 
Boss unaijua miongozo yote ya afya, ukishaisoma IKAMA ndio utajua bado afya huijui. Chief, daktari kabla ya kuwa daktari bingwa anaanza na MD, services anazotoa zote prof Kahamba akiwa Tandahimba ni as a GP not a specialist. Job description ya specialist na list of resources with investigations to be carried out at district level yaani hospitali za wilaya kutokana na muongozo wa maabara (tafuta upo) ni GP level sio specialist level ndio maana kwa muongozo wa watumishi wa afya (IKAMA) daktari bingwa hatambuliki hospitali za wilaya kushuka ngazi ya chini. Miongozo hiyo haikutungwa na NHIF bali wizara ya afya. Pia kitita hichi cha mafao hutolewa na maamuzi ya wizara sio NHIF maana hiyo taasisi ipo chini ya wizara ya afya. Afya sio mihemuko, inamiongozo ambayo nikikutajia hutaiweza ijua mpaka kesho.
Swali langu ni namna gani mwanatandahimba mstaafu wa wizara ya afya atapata huduma essential ya kibingwa akiwa Tandahimba??unajua ni gharama kiasi gani zinamkabili mteja huyu kuja dar?
Zahanati mpya na vituo vipya vya afya na hospitali za kisasa za wilaya zinashusha vipi huduma ikiwemo za kibingwa karibu na mwananchi?
Haya ndio maswali ambayo katoto kalichotoka medical school na kukimbilia kwenye viyoyozi vya ofisi za NHIF hakawezi kuyajibu.ndio maana nasisitiza watulie pembeni wapangiwe na kupangwa
 
Sijui ni kipi kimewahi kufanyika kikafanikiwa!

Umeme tabu, Maji tabu, hospitali huduma tabu, barabara tabu n.k.
 
Swali langu ni namna gani mwanatandahimba mstaafu wa wizara ya afya atapata huduma essential ya kibingwa akiwa Tandahimba??unajua ni gharama kiasi gani zinamkabili mteja huyu kuja dar?
Zahanati mpya na vituo vipya vya afya na hospitali za kisasa za wilaya zinashusha vipi huduma ikiwemo za kibingwa karibu na mwananchi?
Haya ndio maswali ambayo katoto kalichotoka medical school na kukimbilia kwenye viyoyozi vya ofisi za NHIF hakawezi kuyajibu.ndio maana nasisitiza watulie pembeni wapangiwe na kupangwa
Sasa swala lako linakuwa directed directly kwa waziri wa afya maana yeye ndio muhusika mkuu wa wizara husika. NHIF ni mlipaji wa huduma za huduma zilizotolewa na mtu wa afya na si elimu yake. Kwampaka sasa serikari imejenga zahanati, vituo vya afya na hospitali za wilaya hizo ni first step na vyote hivyo zipo chini ya wizara ya afya ila hazijafikia hatua kutoa huduma za kibingwa kule hivyo no specialized procedures au surgeries daktari bingwa atazifanya kule, yeye anafanya huduma ya MD ndio maana mwisho wa siku anamleta mgonjwa Muhimbili kwa matibabu hamtibii kule. Nikukumbushe NHIF inalipa huduma zilizotolewa na si elimu yako huwezi fanya craniotomy kule wala prostatectomy . Sasa wewe umetoa huduma ya normal Medical doctor, unataka ulipwe as a specialist in what sense kwasababu ya elimu yako, hebu tumia akili sasa, amekuja akamuexamine mgonjwa akamrefer mgonjwa as a normal MD does, hakumtibu unataka alipwe as a specialist why?? Nhif ndio isogeze huduma za afya just by misuse of funds wakati kinachotolewa sio huduma za kibingwa.
Pili shika naujue outreach services zikifanywa lengo ni msaada sio mapato, hivyo zikipangwa kufanya zinakuwa zimejigharamikia kila kitu hadi daktari pesa yake ya kumlipa. Sisi sio wakwanza kufanya outreach services, wapo Amref flying doctors wapo World vision na wengineo. Ushawahi sikia wanahitaji gharama za serikari kugharamikiwa in what sense enhee wasio na bima hawapati hiyo service basi hiyo sio outreach ni kitu kingine. Jua hili, kila kitu cha afya kinamuongozo wake na NHIF ni mlipaji wa huduma sio zaidi ya hapo hajapewa mamlaka zaidi ya hayo vingine ni wizara ya afya unachoshindwa kuelewa nikipi hasa.
 
Sasa swala lako linakuwa directed directly kwa waziri wa afya maana yeye ndio muhusika mkuu wa wizara husika. NHIF ni mlipaji wa huduma za huduma zilizotolewa na mtu wa afya na si elimu yake. Kwampaka sasa serikari imejenga zahanati, vituo vya afya na hospitali za wilaya hizo ni first step na vyote hivyo zipo chini ya wizara ya afya ila hazijafikia hatua kutoa huduma za kibingwa kule hivyo no specialized procedures au surgeries daktari bingwa atazifanya kule, yeye anafanya huduma ya MD ndio maana mwisho wa siku anamleta mgonjwa Muhimbili kwa matibabu hamtibii kule. Nikukumbushe NHIF inalipa huduma zilizotolewa na si elimu yako huwezi fanya craniotomy kule wala prostatectomy . Sasa wewe umetoa huduma ya normal Medical doctor, unataka ulipwe as a specialist in what sense kwasababu ya elimu yako, hebu tumia akili sasa, amekuja akamuexamine mgonjwa akamrefer mgonjwa as a normal MD does, hakumtibu unataka alipwe as a specialist why?? Nhif ndio isogeze huduma za afya just by misuse of funds wakati kinachotolewa sio huduma za kibingwa.
Pili shika naujue outreach services zikifanywa lengo ni msaada sio mapato, hivyo zikipangwa kufanya zinakuwa zimejigharamikia kila kitu hadi daktari pesa yake ya kumlipa. Sisi sio wakwanza kufanya outreach services, wapo Amref flying doctors wapo World vision na wengineo. Ushawahi sikia wanahitaji gharama za serikari kugharamikiwa in what sense enhee wasio na bima hawapati hiyo service basi hiyo sio outreach ni kitu kingine. Jua hili, kila kitu cha afya kinamuongozo wake na NHIF ni mlipaji wa huduma sio zaidi ya hapo hajapewa mamlaka zaidi ya hayo vingine ni wizara ya afya unachoshindwa kuelewa nikipi hasa.
yaani NHIF Muharibu halafu unataka tumuulize waziri?Kasome zaidi kuhusu universal health care.
Pia kawaulize zaidi wazoefu juu ya mahitaji essential ya huduma za kibingwa.
Muhimbili inaweza kuwahudumia watanzania wote wenye uhitaji?
...unadhani mjamzito aliopo kikonga huko pwani ndani ndani hastahili huduma ya kibingwa akiwa kikonga hadi afike Muhimbili?
 
Back
Top Bottom