Kwa hili la simu, Anne Makinda ameonewa..!

Kwa hili la simu, Anne Makinda ameonewa..!

maggid kila kitu kina mwanzo na mwisho wake, na hata huyo mnyonge ipo siku atazinduka na kudai haki yake na hapo ndipo nchi itakua haikariki, ukija angalia chanzo cha yote ni upuuzi unaofanyika na watu walio pewa mamlaka
Na katika hili kinachonisikitisha zaidi ni ukweli kuwa, anayeumia ni mwananchi mnyonge aliyetuma sms ya matusi kwa Anne Makinda. Na sasa wanadakwa mmoja baada ya mwingine kwa vile namba zao zimesajiliwa. Hawa wanyonge watafunguliwa mashtaka na kuna watakaoingia gerezani. Kama kijana yule mwanajeshi wa Arusha, ambaye akiwa kwenye sare ya jeshi alionyesha alama ya Chadema akiwa kwenye picha na viongozi wa Chadema. Naye yuko jela sasa. Wakati haya yakiwatokea wanyonge , waheshimiwa wenye kutaja namba za simu za waheshimiwa wenzao hadharani, wataendelea ' kusakata-rhumba' - Kwa Raha Zao!

Maggid
 
Mjengwa nani kakupa mamlaka ya kuhukumu eti wamekosea kutoa namba? napata mashaka ya namna unavyotumia kalamu yako kuhujumu juhudi za ukombozi wa haki na demokrasia ya kweli
Mbona MWAKYEMBE alitoa namba
yake hajatukanwa? huyo ni utumwa wake ndo unampelekea MATUSI pamoja na
kuwa si vema kutumia lugha ya matusi kumrekebisha mtu ila nae APATE
funzo kama kuna viongozi wengi wametoa no zao na hawatukanwi yeye kwa
nini anatukanwa?.
 
Ndugu zangu,
kuna ambao hamjanielewa. Hoja yangu ya msingi ni kuwa, yale mazingira yaliyopelekea simu ya Spika na Naibu wake kutolewa hadharani yamechangia pia kuwapa wakati mgumu wahusika maana kuna waliotumia fursa hiyo vibaya na kupiga au kutuma jumbe za matusi kama wahusika ( Makinda na Ndugai) walivyolalamika. Kuna wakati tuache ushabiki wetu wa kisiasa na tuje kwenye hali halisi.

Mkuu maggid naomba nipingane na wewe.. Kwanza ninaomba uelewe hakuna litakalofanyika bila ya kuwa na "opposite force" kama wanielewa.. Mfano zipo namba za dharura za kupiga polisi na zimamoto kukiwa na shida.. Ila unafahamu wanavyolalamika wanavyopigiwa simu ovyo na raia wasio na matatizo yeyote..! Lakini bado huduma za dharura zinaendelea kwa mafanikio makubwa.. Kwa hiyo hiyo ya kusema namba imetumika vibaya haina mashiko..

Halafu hujaona kauli ya Katibu wa bunge.. huyu ambae anataka kuzuia bunge kuonyeshwa live alivyosema kuhusu sakata la kutoa namba za simu za spika na naibu wake..? Amesema Chadema kutoa namba za spika na naibu wake sio kosa.. Kosa liko kwa alietukana.. na sheria ichukue mkondo wake kama kuna msg ya matusi kwao..

Inawezekana nilikuwa ninasoma makala zako but kwa mnyumbulisho huu ninaanza kupata shaka kama huwa unaandika makala bila ya kuwa influenced..
 
KUMBE MAGGID NAYE MSHENZI HIVI, yani akili yake inaonyesha kuwa makinda ndio ameonewa lakn ndungai hajaonewa. Kuna tofaut gan kat ya alichofanyiwa ndungai na makinda? Kwa ndungai hawez sumbuliwa na wanawake wanao amini kuwa wabunge wanapesa? Unatumia masaburi kufikiri? Kama ni swala la kuweka namba hadharani, basi bunge ndiyo lina makosa kwa kuweka namba za wabunge wote kwenye website yao
 
Kumbukeni ule usemi "asiyefunzwa na mamaye hufunzwa na walimwengu"
 
Maggid usiishi dunia ya kusadikika kama simulizi za Shaaban Robert!!

Hao ndio wananchi ambao mfumo unaowakilishwa na Anne makinda na mwezie bungeni unawakarahisha kwa kanuni wasizozielewa!

Hao ndio watanzania ambao mfumo wa CCM unakataa kuwapa elimu bora na elimu ya uraia. hao ndio wananchi ambao hawaelewi kwa nini wawakilishi wao wazibwe midomo wasizungumze mambo ambayo wanaona yana maslahi kwao, hao ndio wananchi ambao wanamuona Anne makinda kwamba anatumika kuilinda serikali licha ya madudu lukuki yanayofanywa na serikali ya CCM.

Makinda anapokandamiza hoja za wawakilishi wao basi hasira zao lazima zitaelekezwa mahali fulani na hapo mahali ni kwa Spika ambaye ndiye mwakilishi wa mfumo kandamizi wa wawakilishi wao.

Maggid usisahau kwamba wananchi wengi wanamuona Makinda kama mtu aliyepewa nafasi ya uspika ili kumuengua Mzee wa kasi na viwango; Sam Sitta ambaye katika macho ya wananchi wengi wanamkumbuka kama alikuwa spika bora kwa kuweka uwiano katika bunge la zama za vyama vingi tofauti na Makinda ambaye anaonekana kuwa na hangover ya chama kimoja na ajenda kuu ya kulinda uoza wa serikali ya CCM kukidhi matakwa ya waliompa kazi ya uspika.

Maggid do not be self righteous; wananchi wanaona na wanajua kilicho chema na kisichowafaa, usiwahukumu haraka; jaribu kutafakari hasira hizo zinatokana na nini?!


Let the people vent their anger; what goes around;comes around
 
Busara miongoni kwa viongozi wa Chadema imekosekana, wao wanafikiri kwa matumbo

Majid Mjengwa na Mafilili,

Nasikitishwa na mawazo yenu finyu! Hivi kosa la Wabunge wa CHADEMA ni kuwapa Wananchi/Watanzania namba za simu za Anne Makinda na Job Ndugai au kuwahamasisha wawapigie simu??? Maana namba za wabunge wote kuanzia Spika,Naibu wake, PM na Mawaziri wote mbona ziko kwenye Website ya BUNGE???Mtu yeyote anaweza kuingia kwenye mtandao wa BUNGE na akasoma namba ya Mbunge yeyote na akaweza kumtwangia simu au sms!!!Kama namba za Wabunge ni siri basi waziondoe kwenye Website kama wanavyotaka kuondoa TV Live Broadcasting!!!

Halafu Bwana Majid, kwanini wewe ume-single out Makinda peke yake???Je,unataka kutuambia Job Ndugai yeye hakutumiwa sms za kutukanwa???Mbona KAMWENE unataka kuanzisha hali Tribalism biasing???Maana kwa mtu akisoma katika ya mistari kuna kaharufu ka ukabila hapa......kuna ka-ukamwene na ka-uiringa ringa hapa!!!

Maana kama ungelikuwa fair ungeli-generalise kwamba Makinda na Ndugai wameonewa! Lakini wa kwetu unapoleta habari za Oh,sijui Makinda kaonewa sana mimi napata taabu kidogo hapa! Ok, tuseme basi kwa vile huyu dada yako ni Mwanamke, sawa. Lakini hiki si ndicho wanachokipigania hawa mama na dada zetu kwamba WANAWEZA hata vitu vya wanaume???Sasa unaposema kaonewa ni vipi????Kwanza yeye kama Spika ndiye AMEWAONEA WATANZANIA KWA KUZIKATAA HOJA ZA MSINGI NA MUHIMU ZILIZOWASILISHWA NA WABUNGE WALIOTUMWA NA WATANZANIA WENYEWE KWENDA KUZIWASILISHA BUNGENI. Makinda na Ndugai lazima wabebe lawama hizi hawana cha kujitetea hapa!!!Wafanye wafanyavyo historia itwahukumu na Teknolojia itaendelea kuwaumbua taraaatibuu pamoja na kutaka kuzuia matangazo ya TV Live!!!!

Pamoja na ubaguzi ulioonyesha kwenye hili bado Makinda na Ndugai wanastahili malipo haya ya sms za kuwataka wajiuzulu. Nakumbuka vizuri sana siku ile Wabunge wote wa CDM waliosoma namba za Makinda na Ndugai kwa Wananchi waliohudhuria mkutano ilikuwa kwa ajili ya KUWATAKA wajiuzulu na si kutukanwa!!!!
Sijasikia Job Ndugai yeye kapokea sms ngapi za kumtaka ajiuzulu au matusi. Tumesikia Polisi wanafanya uchunguzi katika sms hizi, tusubiri.

Bado jambo hili litaendelea kuleta utata na kuibua na mambo mengine ya nyuma. Tunakumbuka wakti wa Uchaguzi 2010 kuna sms zilikuwa zikitumwa kwa viongozi wa CDM hasa mgombea Urais Dr.Slaa za kumtukana na kumdhalilisha pamoja na swala hilo kufikishwa Policcm mpaka kesho hatujasikia watu wamekamatwa kutokana na kadhia hiyo.Itakuwa ni kichekesho sana kwa Jeshi letu la Policcm kama kweli wataweza kuwakamata hao watu zaidi ya 400 waliotuma sms kwa Makinda achilia mbali Ndugai!!

Hizi zitakuwa salamu nzuri sana kwa Makinda na Ndugai kuwajulisha kuwa viti walivyokalia wamepewa na Watanzania ambao wamewapa ridhaa ya kuingia Bungeni ili kwenda kutetea maslahi ya Watanzania lakini wanafanya kinyume chake. Wakumbuke kuwa wao ni watumishi wa Wananchi na siyo CCM!!!!!
 
Hivi kwanini mashabiki wa chadema wanapenda sana matusi?
una uhakika gani kama ni chadema???? tangu uingie kwenye siasa akili zimemeyeyuka...
Na katika hili kinachonisikitisha zaidi ni ukweli kuwa, anayeumia ni mwananchi mnyonge aliyetuma sms ya matusi kwa Anne Makinda. Na sasa wanadakwa mmoja baada ya mwingine kwa vile namba zao zimesajiliwa. Hawa wanyonge watafunguliwa mashtaka na kuna watakaoingia gerezani. Kama kijana yule mwanajeshi wa Arusha, ambaye akiwa kwenye sare ya jeshi alionyesha alama ya Chadema akiwa kwenye picha na viongozi wa Chadema. Naye yuko jela sasa. Wakati haya yakiwatokea wanyonge , waheshimiwa wenye kutaja namba za simu za waheshimiwa wenzao hadharani, wataendelea ' kusakata-rhumba' - Kwa Raha Zao!

Maggid

inasikitisha sana mtu mzima kutokuwa na akili....aisee wewe jamaa huwa ni mnafiki sana.....
 
Wikolo,
Asante sana,
Hata kama viongozi wa Chadema hawakuwaeleza watu wamtukane au wamdhalilishe Spika Anne Makinda, lakini, akili ya kawaida tu inakuambia, kuwa baada ya namba hiyo ya mkononi kutolewa, Spika Makinda asitarajie sms za kumtakia " Happy Valentine Day!".

Hoja yangu ya msingi ni kuwa kuna njia nyingine za kistaraabu zaidi na zenye kulinda faragha ya mtu za kuwasilisha malalamiko. Ikumbukwe pia, kuwa Anne Makinda anawakilisha taasisi ya Bunge. Sasa namba binafsi ya mkononi kutolewa hadharani yaweza kuwa usumbufu mkubwa kwake. Ni mtazamo wangu tu.

Kwa hiyo angetumiwa Happy Valentine Day ingekuwa sawa!!!!!!???
 
Mkuu Majid akili ya kawaida inapimwaje? Sijaona ona unacholalamikia kaka. Mimi nadhani picha waliyopata spika na naibu wake iwe fundisho kuwa utendaji wao ni mbovu. Tena wawashukuru CDM kwa kufanikisha wao kuona jamii inavowaona. Kama na ishara hizi hawataziona tusingependa yakitokea makubwa zaidi (Hatuombei) wasikimbilie huruma ya uma kama wanavofanya. Wananchi tumechoka kuburuzwa.
 
Maggid, Haya yote wakati mwingine yanasababishwa na hao wahanga wahusika(kama Makinda). Ubabe,ulevi wa madaraka na kutosikia lolote unaloshauriwa hata kama ni jema kwa vile wewe una madaraka ya mwisho ni hatari sana kwako wewe mwenyewe.
Walichofanya viongozi wa Chadema ni kumpatia ujumbe kuwa kama tusemacho sisi ambao tumetumwa na waliotuchagua unakidharau basi ngoja upate ujumbe toka kwao directly.
Nina hakika hata kama wametusiwa( ingawa kila mtu anatafsiri yake kwa tusi) lazima watakuwa wamepokea ujmbe mwingi wenye kuonyesha hisia sahihi kuhusu wakifanyacho na ushauri mzuri tuu wafanye nini.
Mbona wewe unatoa makala zako hapa za kuelimisha na unaungwa mkono sana na wengine wanakukosoa tena kwa lugha chafu na hujaacha kuandika? Kwa sababu unajua unadili na watu yote yapo.
Watende kulingana na kanuni na busara za kiuongozi kama haya yatawatokea,na wataifurahia kazi yao ya utumishi wa umma uliotukuka sio ukibaraka dhidi ya wananchi wanyonge.
Naweza sema kama kuna malalamiko toka kwa Makinda na Ndugai basi Chadema zoezi hili wamefanikiwa maana ujumbe umefika toka kwa wenye Bunge ( wananchi)

I could not have said it better
 
Hivi uthibitisho wa kwamba spika ametumiwa sms za matusi ni nani hasa anao? Au ni aina nyingine tu hii ya propaganda tunaletewa? Watu kadhaa wamekuja hapa jamvini na kusema spika ametumiwa sms za kumdhalilisha na wakati huo huo, hakuna hata sms moja ambayo imeonyeshwa walau kama mfano.

Mkuu Maggid, kikubwa hapa ni uadilifu wa mtu anayeshika nafasi hiyo bila kuangalia jinsia yake,chama chake,elimu yake na kigezo chochote kinginecho. Watu watende haki kama wanavyopaswa kulingana na majukumu yao. Sipingani na wewe kwa sababu ulichokitoa hapa ni maoni yako na yanapaswa kuheshimiwa kama yalivyo, lakini hebu na wewe basi jaribu kuheshimu mawazo ya viongozi wa chadema walioona kwamba kugawa namba za viongozi hao kwa wananchi ingeweza kusaidia kuongeza mbinyo kwa watu hao kutenda haki. Viongozi wa chadema hawakuwaeleza watu wamtukane au kumdhalilisha spika na naibu wake.
Mkuu umenena.Swali lingine kwa Maggid,je wakati Spika anatuonea Watanzania wote kasoro hao wachache walioko Serikalini kwa kutunyima fursa ya kutoa maoni yetu kupitia Wabunge au Wawakilishi wetu ulijisikiaje?.
 
Maggid ni dhahiri ya kuwa unahubiri usichokiamini ila unachochewa na tamaa ya kutaka kupewa ukuu wa wilaya kama ilivyokuwa Novatus Makunga. Maggid sioni sababu ya kumuhurumia Makinda ambaye akiamua kujiuzulu hatapata hasara yoyote wala madhara yoyote zaidi ya kupongezwa na hao hao waliomtumia sms 400, akina mama wa Dar es salaam ambao wana shida ya maji kwa nini Maggid usiwaone huruma akina mama hao? Umuone huruma Makinda ambaye ametaka mwenyewe kuwa speaker na anaweza kuepuka kadhia hiyo? Akina mama wa Dar hawawezi kuepuka kadhia ya ukosefu wa maji kwa sababu Makinda na Ndugai wamekataa hoja ya Mnyika. Specker Makinda anastahili kuona hasira za wananchi kidogo na kuzionja hasira hizo amelewa sifa za waliomuka hapo kwenye kiti na kumuambia kila kipo sawa. Pili, Maggid, namba za speaker zipo hadharani kwenye tovuti ya bunge utazipata. Maggid, Mwakyembe alitangaza namba zake na hakuna mtu aliyemtusi wala kumbughudhi watu wanafahamu haki zao na wanamjua anayedhohofisha harakati zao.
 
Maggid, Ama hujaelewa msingi wa hoja ya chadema ama una huruma sana na viongozi wa ccm. Nitakuuliza maswali machache;
Hivi nani anaumia zaidi kati ya Watu wanaokufa ktk nchii hii kutokana na matatizo ambayo yangeweza kutatuliwa na Bunge lakini Bunge linabanwa na spika Makinda na maumivi ya Anna makinda kupitia meseji? Hivi watu wanaokosa maji huku Dar huku Spika amezima hoja ya mnyika wakikusoma unadhani wanakuelewa kweli?

Ushauri wako kwa viongozi wa chadema wa kukusanya msg na sauti ni mzuri. Hata hivyo, kwa ushauri wangu ungepeleka msg hiyo hiyo kwa Rais Kikwete ambaye anakusanya kodi ili aendeshe zoezi hilo. Chadema hawana fedha za kufanya kazi hiyo.
 
Yeye pia hajawatendea haki watanzania hivyo ajirekebishe kwanza yeye
 
kwani wewe unaugulia nini? au hamnazo nini? kama hata achia ngazi basi hayo aliyo yapata ni madogo kunamakubwa yanakuja, sasa kwasababu wewe ni mnafki basi utaendelea kutetea upuuzi, na ikiwezekana ukaombe kazi ya utezi kwa huyo bi-kiloboto.


Wikolo,
Asante sana,
Hata kama viongozi wa Chadema hawakuwaeleza watu wamtukane au wamdhalilishe Spika Anne Makinda, lakini, akili ya kawaida tu inakuambia, kuwa baada ya namba hiyo ya mkononi kutolewa, Spika Makinda asitarajie sms za kumtakia " Happy Valentine Day!".

Hoja yangu ya msingi ni kuwa kuna njia nyingine za kistaraabu zaidi na zenye kulinda faragha ya mtu za kuwasilisha malalamiko. Ikumbukwe pia, kuwa Anne Makinda anawakilisha taasisi ya Bunge. Sasa namba binafsi ya mkononi kutolewa hadharani yaweza kuwa usumbufu mkubwa kwake. Ni mtazamo wangu tu.
 
Back
Top Bottom