Minjingu Jingu
Senior Member
- Nov 2, 2023
- 116
- 480
Iliniumiza sana msichana tumeanza naye mahusiano siku tatu tu akaniambia ana changamoto anahitaji tsh 150,000. Nikamwambia sina yote nina Tsh 100,000 nikamtumia. Hakusema hata amepokea, akanyamaza tu.
Ikabidi nimpigie simu kujua kama amepokea au laah, akapokea simu nikamuuliza "umeona kuna pesa kidogo nimekutumia Tsh. 100,000", akasema "Nimeona." Nikasubiri hata aseme asante hakusema, akaniambia, "Nipo natafuta hiyo 50,000 kwa rafiki zangu waniongezee maana nilitaka tsh 150,000 na nilikuambia hivyo."
Nikasema sawa nisamehe sikuwa nayo yote, akanijibu "Basi baadaye." Nikaingia kwenye menu yangu ya Tigo Pesa nikaomba kuirudisha ile pesa, nashukuru haikuchelewa sana ikarudishwa, nikamshukuru Mungu.
Nikamtumia mama yangu Tsh. 20,000 nikanyamaza. Akapiga simu dk hiyo hiyo akishukuru sana na kunitakia mibaraka mingi mingi, nikamwambia mama hiyo kidogo, akasema hapana hakuna pesa kidogo, akashukuru na kuniombea pale nilipopungua parudishwe.
Basi alivyokata tu simu nikammalizia na ile nyingine 80,000, akanipigia simu tena this time nikamwambia mama naingia kwenye kikao, nashukuru Mungu akubariki.
Niliona angenishukuru sana mpaka nakuwa najisikia vibaya. Siku zote mama yangu yupo hivyo umtumie 10,000 ya voucher umtumie 200,000 ya matumizi shukrani zake zipo pale pale. Nikawaza sana kuwa hawa wanawake wa sasa hivi wanakwama wapi kuwa that much cold?
Yule msichana mpumbavu akanipigia simu kuwa mbona tena ile pesa nimeichukua, nikamwambia niliona ni ndogo sana nimeichukua nimemtumia mama, yeye asubiri nikipata nyingi nitamtumia, nikakata simu.
Mpaka leo hatuna tena mawasiliano, nime-mblock.
Ikabidi nimpigie simu kujua kama amepokea au laah, akapokea simu nikamuuliza "umeona kuna pesa kidogo nimekutumia Tsh. 100,000", akasema "Nimeona." Nikasubiri hata aseme asante hakusema, akaniambia, "Nipo natafuta hiyo 50,000 kwa rafiki zangu waniongezee maana nilitaka tsh 150,000 na nilikuambia hivyo."
Nikasema sawa nisamehe sikuwa nayo yote, akanijibu "Basi baadaye." Nikaingia kwenye menu yangu ya Tigo Pesa nikaomba kuirudisha ile pesa, nashukuru haikuchelewa sana ikarudishwa, nikamshukuru Mungu.
Nikamtumia mama yangu Tsh. 20,000 nikanyamaza. Akapiga simu dk hiyo hiyo akishukuru sana na kunitakia mibaraka mingi mingi, nikamwambia mama hiyo kidogo, akasema hapana hakuna pesa kidogo, akashukuru na kuniombea pale nilipopungua parudishwe.
Basi alivyokata tu simu nikammalizia na ile nyingine 80,000, akanipigia simu tena this time nikamwambia mama naingia kwenye kikao, nashukuru Mungu akubariki.
Niliona angenishukuru sana mpaka nakuwa najisikia vibaya. Siku zote mama yangu yupo hivyo umtumie 10,000 ya voucher umtumie 200,000 ya matumizi shukrani zake zipo pale pale. Nikawaza sana kuwa hawa wanawake wa sasa hivi wanakwama wapi kuwa that much cold?
Yule msichana mpumbavu akanipigia simu kuwa mbona tena ile pesa nimeichukua, nikamwambia niliona ni ndogo sana nimeichukua nimemtumia mama, yeye asubiri nikipata nyingi nitamtumia, nikakata simu.
Mpaka leo hatuna tena mawasiliano, nime-mblock.