Kwa hili, Dr. Slaa wewe ni 'Mdini' pia!

Kwa hili, Dr. Slaa wewe ni 'Mdini' pia!

Status
Not open for further replies.
Kwanza hakuna ubishi kwamba Dk Slaa ni mdini kama alivyo mtu mwingine kwa sababu amewahi kutumikia dini kwa ahadi kabla hajaamua kusaliti na kurudi uraiani nadhani kwa lengo la kuwatumikisha.

Pili, hakuna ubishi kwamba gazeti la Tanzania daima ni kampeni meneja wa CHADEMA na tatu hakuma ubishi kwamba kuna wimbi kubwa la masuala ya udini.
Ushauri wangu:
Kama kweli hawa viongozi wanataka kututawala na kuongoza nchi hii waache huu ujinga wa kupandikiza udini miongoni mwa watanzania.

Tunajua sana kwamba wewe ni diwani wa igoma uliyekiri kupewa fedha na CCM ili kusambaratisha chama chako cha zamani na kumvua umeya aliyekuwa meya kwa njia ya chadema
Tunakujua sasa hivi unasema unakula sahani moja na wenje kuhakikisha hasimami kwenye uchaguzi ujao
tunakujua sana upo mtaandaoni kuiangusha chadema kwa njia zozote kwa hiyo unayoyasema kuhusu Dr Slaa uliyemtukana sana huko nyuma hatushangai, lakini unakiri kuwa kuna udini sasa tuyazungumze haya matatizo na tuseme chanzo chake ndipo tutakapoweza kuyaondoa wote tunajua KIkwete aliingia madarakani kupitia misikiti na kuwabambikia wagombea wenzake kwamba ni wadini sasa tatizo limeota mizizi tupambane kuliondoa
 
Hilo gazeti la kufungia vitumbua na maandazi lisipofungiwa sasa litakuja kusababisha machafuko katika nchi yetu.
Ni vyema Serikali ikaliona hili mapema.
Mwanahalisi pia lilikua linaleta mafuko?
 
Mtu ambaye ni mdini ni yule ambaye anatumia dini fulani kupata kitu fulani, anatumia nafasi aliyonayo kuwapendelea watu wa dini fulani, anatumia uwezo wake/nafasi yake kuwadhulumu watu wa dini fulani au anafanya mobilization za kijamii kwa misingi ya upendeleo au ubaguzi wa kidini.Mtu yeyote mwenye tabia hizi ni mdini bila kujali ni nani. Wala mdini si mtu anaye kemea tabia miongoni mwa hizo zilizotajwa hapo juu.Kila anayedhani yeye ni mtu mwema na wakupigia mfano; na awe wa kwanza kujiepusha na tabia tajwa hapo juu.

kwa hiyo unamtetea dr slaa kuwa amekemea? yeye ana mamlaka gani ya kukemea wakati yeye mwenyewe ni mtuhumiwa?
 
Kama ambavyo mods wataufunga huu uzi punde, vivyo hivyo gazeti la Tanzania Daima linatakiwa liwekwe kwenye watch list.
 
kwa hiyo CDM ikichukua nchi ndo waislam watafukuzwa? khaaaa. sina imani na dr slaa na sina imani na machadema wote. chama gani cha kibaguzi hiki

Uzuri hii propaganda iliyoenezwa na mwenyekiti wa CCM Mh Jakaya KIkwete imemurudia mwenyewe taifa sasa linaangaliwa kama taifa lenye kurutubisha magaidi wa kidini mpaka sasa tunahamisha dhambi kuwasakizia wamerekani Kikwete analohili na chama chake wewe angalia juzi imesemwa tuuache kusema mambo ya uchochezi nape anasema chadema ni chama cha magaidi sasa kikutana na chama chama magaidi na majangiri CCM ndipo nchi inapolipuka,haitawaliki na hakuna tena utawala wa sheria fujo tupu zilizoasisiwa na MACCM
 
Dr Slaa bora ungekaa kimya kuliko kuendelea kujidhalilisha na kauli zako.

Ueleweki mara useme ulishinda uchaguzi usalama wa taifa wakaiba kura.

Kwa kukusaidia tu JK toka aingie madarakani misikiti anayokwenda ni ya Bakwata ambayo haina waumini wengi.

Huwezi kumkuta JK kwenye misikiti mikubwa hapa Dar kama Kichangani, Mtambani, Idrisa, Mtoro.

Labda tuambie misikiti gani alikuwa anafanya udini, halafu una uhakika gani kuwa Waislam wote walimpigia JK.

Ngoja nikuletee vile vipeperushi vilivyokuwa vinasambazwa MISIKITINI kwamba WAISLAMu wamuchague JK kwasababu ni Musilamu mwenzao. Aibu yako.

Halafu nitakuletee ule waraka wa Wakiristu na Waislamu uone tofauti yake. Waraka wa Waislamu ulihimiza wazi Waislamu kumchagua RAIS muislamu mwenzao, wakati ule wa Wakiristo ulisema achagulie RAIS mwenye maadili na mzalendo, bila kutaja jina wala dini ya mtu. Penye uongo ukweli hujitenga.

JK hasali tena hiyo misikiti ya Fundamentalists (wavaa mabomu) kwasababu anajua aliwandanganya kuwapatia MAHAKAMA YA KADHI. Anaogopa kupigwa vibao kama Alhaji Mwinyi. Get real dude!
 
kwa hiyo unamtetea dr slaa kuwa amekemea? yeye ana mamlaka gani ya kukemea wakati yeye mwenyewe ni mtuhumiwa?

Mtuhumiwa ni Jakaya kikwete ndani ya bunge,miongoni mwa taasisi na wananchi hata mkewe anafahamu mumewe ni mwanzilishi wa udini na mpaliliaji ili tu utukufu wake na mali zake ziweze kudumu daima unamsikia nitakabidhi nchi kwa mwana CCM manake atatumia njia yeyote ikiwemo kutumia dini
 
Mh udini udini tunaelekea wapi? Jadilini mambo ya msingi sio kueneza ushawishi usiofaa.
 
kwa hiyo unamtetea dr slaa kuwa amekemea? yeye ana mamlaka gani ya kukemea wakati yeye mwenyewe ni mtuhumiwa?
mfano kama mtu karipoti tukio la ujambazi katika kituo cha polisi na mimi na wewe ndio askari, tunachotakiwa kufanya cha kwanza ni kuhakikisha kama ripoti aliyotoa ni ya kweli na kama ni ya kweli tuishughulikie na kumpongeza kwa kuitoa na kama ya uongo tumkemee halafu baada ya hapo kama tunajua kuwa na yeye kuna mahali aliiba ndio tuanze kumshughulikia sasa; (hiyo ni kesi mpya) lakini sio mtu ana ripoti na kukemea tukio lisilofaa halafu badala ya sisi kupitia hatua stahiki, tunakimbilia kuangalia udhaifu wa mtoa taarifa eti ili iwe ndio sababu ya kuitupilia mbali taarifa yake.huu ni ushabiki usiosaidia kitu.
 
the more we talk about this saga the more it roots into us. most of the threads under such kind of posts drill out the hate, ignorance and most probably sarcasms. at least if we all do not agree about what these politicians bring to us, we should stand firm and say it as one thing because this outrage is of no joke when it burst out. we stand together regardless of our political affiliations against this saga!
 
Mmebugi; mnaambiwa ukweli na Dr. Slaa halafu mnaweke thread ya udini, sasa mdini nani?

Hili ndio tatizo linalotufanya sisi tuendelee kuwa wasindikizaji milele, Watawala na vijana wao hawataki kabisa kujadili chanzo cha matatizo
  • Wanataka tubadili matokeo ya form four hawataki tujadili chanzo cha failure
  • Wanatuonea huruma umaskini wetu ila wao na rais wao hawajui chanzo cha umaskini wetu
  • Na sasa wanataka kuutibu udini na hawataki tujadili chanzo. Hii yote ni kwa sababu wao ndio chanzo
 
Hakuna kupepesa macho mwanzilishi wa udini hapa nchini ni baba mweye nyumba!! huu ndio ukweli na ni lazima tuuseme!

Kura ya muislamu ni kwa muislamu..
 
Nchi zinazo ongongozwa kwa mfumo wa kidini duniani ni za Kislam tu, hizo ambazo ni za Kikrsito wala hata hayo maadili ya Kikristo sio lazima kiongozi awe nayo, nchi pia zinazo ongozwa kwa Kislam ndizo zinazoongoza kwa machafuko, kwa ufupi, huwezi kutofautisha fujo, chuki na mauaji na Uislam.

Hivi Al Asad si ni mwislam na nini anawafanya Waislamu wenzie? jumuia ya kimatifa kama Marekani ndizo ambazo zinajaribu kumshawishi Al Asad aache kufanya mauaji ya kikatili, mbaya zaidi Iran, nchi ambayo ndio mfano bora kwa Waislam duniani, ina support mauaji anayoyafanya Al Asad, narudia, huwezi kutofautisha chuki, fujo, mauaji na Uislam!

Naomba nikujibu kwa uungwana japo hukuchangia kiuungwana na hustahiki kufanyiwa uungwana.
Huwezi kutambua uislam unaelekeza nini kwa kumuangalia muislam anafanya nini, kama ambavyo ni kawaida pia kumkuta muumini anatenda kinyume kabisa na maelekezo ya imani anayojinasibisha nayo, hatuwezi ku-reflect mafundisho ya imani fulani kwa sababu tu ya matendo ya waumini wake. Huwezi ku-coment kwa ku-generalize kiasi hicho, huo ni ukosefu wa fikra. Ukitaka kidogo ueleweke kwenye hayo maneno yako yenye red; substitute neno "Uislam" uweke neno "waislam"

Kwa ushauri tu: Ukitaka kujua uislam kwa kuutendea haki, "usome uislam unafundisha nini na sio waislam wanafanya nini" utakuta ndani yake kuwa uislam ni mzuri sana kinyume na waislam wenyewe walivyo.
 
Tatizo huwa tuna BWETEKA na kila moja hupenda dini yake..hiyo ni haki yako.. Lakini kuna TAIFA na uzalendo kwanza.
Masilahi ya nchi yako iwe mbele baadaye hayo mengine kama yana ulazima yatafuata.

Kiroho safi chukua "LIKE"
 
Tanzania waislam hawazidi 40% according to tbc je kikwete kashindaje kama waislam wachache kuliko wakristo?
 
Ndugu Kibe, kwanza nikuombe radhi kuwa nitatumia maneno mengine ambayo yanweza yakakukera lakini ni afadhali yakukerer lakini yanasaidia kutokulisha Taifa kasa ya uadui.

>Kwanza style uliyoitumia kuleta uzi wako imekuwa imejaa chuki kuliko kuliko kuleta mshikamano wa kweli baina ya Watanzania. Umetumia maneno ambayo yamejaa shari na chuki.

>Uzi wako umekosa vigezo/viashiria vya udini. Kwanza ungetuambia Dr.Slaa wakati anamtuhumu JK kuwa mdini amefanya hivyo bila kuorodhesha walau viashiria/ vigezo vinavyomfanya JK kuwa mdini? Na mdini wa dini gani hiyo? Na kama gazeti tajwa halitaja viashiria ambavyo Dr.Slaa amevitaja basi ungeacha kuleta uzi huu au kama wameviorodhesha lakini wewe hukuvileta kajipange upya uje na uzi mwingine.

>Tatu, ni kutumia gazeti kumhukumu Dr.Slaa na kuunga unga vitu ili uonyeshe Dr.Slaa ndiye mdini. Kwanza sidhani kama Dr.Slaa ndiye kalituma gazeti kuandika yaliyoandikwa. Mhariri anao uhuru wa kuandika alivyoona inafaa. Hukuwepo eno la tukio ili kushuhudia kile unachosema.

>Waraka wa Wakatholiki-Kwanza huo haukuwa waraka wa maaskofu bali wa wanazuoni wa Kikatholiki na Wiaslamu na wasiokuwa Waislamu walioamua kuusoma vizuri bila jicho la chuki na husuda wanakubali ulikuwa informative na haukuwa na chembe ya udini. Hakuna mahali alipotajwa Dr.Slaa wala CDM kwenye nyaraka hizo. Hapo lazima uwe mkweli wa dhamira yako na hapo watu watakusoma na kukuelewa lakini ukilazimisha unachotokitaka kiwe kama unavyotaka hata ujumbe wako uliotaka kuutoa kwa hadhira yako unakuwa umewekewa doa

>Ushuhuda wa macho na masikio yako kuwa ulimwona Dr.Slaa akiomba kura kwa kutumia kanisa, nakuomba umwogope Mungu wako. Andika vyovyote unavyotaka lakini usiandike kitu halafu ukaombwa ushahidi ukaishia kusema nilukuwa na mbwa wangu. Ninajua kwa asilimia 100 Dr.Slaa hakuwahi kupiga kampeini kanisani. Na ni kanisani gani hilo mbona hulitaji? Halafu neno Kanisa jamani ni pana mno na lazima uliheshimu unapokuwa unalitumia neno hilo na uende deeper kuelezea una maana gani kwenye matumizi yako. Kama ambavyo hupendi dini yako, dhehebu lako na viongozi wako wa dini wadhihakiwe na wewe usiwe mwepesi kutumia vibaya taasisi za dini za watu na viongozi wao
 
huyu mzee mimi huwa simwelewi sijui kama ni uzee au ni kutapatapa make kila anachofanya anakosea.
 
Tatizo huwa tuna BWETEKA na kila moja hupenda dini yake..hiyo ni haki yako.. Lakini kuna TAIFA na uzalendo kwanza.
Masilahi ya nchi yako iwe mbele baadaye hayo mengine kama yana ulazima yatafuata.

Mbona 2005 Askofu Kilaini alitamka kwamba Kikwete ni chaguo na Mungu, CCM na wapambe wakachekelea na hakuna aliyekemea udini?! CCM 2005 alisema CUF ni chama cha kidini. Je CUF ni wadini? Nani aliweka ilani ya Mahakama ya Kadhi mwaka 2005 ambayo ilianzisha fukuto la udini hapa nchini? CCM ndiyo imepandikiza mbegu ya udini na sasa inavuna ilichopanda. Kwa kimombo CCM's "chicken has come home to roost!"
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom