Ninachoamini mimi kuwa binaadamu ni sawa na wanyama wengine,katika wanyama mwenye hisia sana mmoja wapo ni mbwa,kwa wale wafugaji mbwa wanaweza kuelewa nini naongea.
Mbwa ana uwezo wa kujua nani anakuja kukutembelea nyumbani kwako anaweza kujua kama anaekuja ni mtu mbaya au mzuri,kwa wale wahalifu wanaofuga mbwa wanatumia mbwa kujua kama askari anakuja sehemu waliyopo..
Kama mtakumbuka wakati wa "Tsunami" ule mtetemeko wa ardhi uliotokea chini ya bahari shehemu ya mashariki ya mbali,tetemko hilo lilisababisha mawimbi makubwa sana katika nchi mashariki ya mbali hasa Thailand...
Tembo na ndege na wanyama wengi walikimbilia sehemu za milima kabla "tsunami" kutokea, hii ilishanga wa watu sana,Wanyama waliweza kuona kama kutatokea kitu kibaya kabla hata hicho kitu hakijatokea..
Binaadamu tuna hisia kama za wanyama lakini uwezo unapishana, binaadamu wengine wana uwezo mkubwa wengine mdogo,wengine wanahitaji kukuzisha uwezo wao,wengine wanajitambua wana uwezo huo wengine hawajitambui kama wana uwezo huo
Nakubaliana na mengi uliyoelezea katika maandishi yako,japo kuwa naona kama mengine umezidisha kuweka chumvi kidogo,Binafsi ninao uwezo kam wako,kwa mambo fulani,mfano chochote ninachokitabiri kitatokea,nikisema mwezi au siku fulani nitapata kitu hichi basi nitapata ukweli sijui napata vipi lakini napata..
Chakushangaza mengi ya mambo ninayopata au yanayokuja kwangu kwanza yanaanza kama hisia au "vision" fulani,Mfano hivi sasa nina hisia kuwa mwakani lazima niendeshe gari ya Volvo cx 70,basi asilimia 95 nitakuwa na hiyo gari...
Nilikuwa hodari sana Darasani,mpaka nimemaliza elimu ya juu mimi nilikikuwa ni mtu wa pili kwa shule,nimeshukua shahada ulaya ambayo vile vile ilikuwa mfano kwa walimu,nina uwezo wa kuona kama kitu kibaya kitanitokea,nina uwezo wa kumjua mtu mzuri au mbaya,nina uwezo a kujua nini mtu anataka kuongea kabla hajaongea....nk
Kwa ufupi nimeamini nini unachojaribu kukieleza,ni "frustration" imekukumba hujui kwanini uko hivyo....lakini hicho nikipaji ambacho kila binaadamu anacho,sema wengi wetu hatujui vipi tukitumie.....