Kwa CV hii kuna pointi kweli huko Arumeru

Kwa CV hii kuna pointi kweli huko Arumeru

Vipi ya profesa maji marefu na jah people aliyenazo atumwagie hapa katika huu uzi.
 
Wenye CV nzuri ni wepi, na wamefanya nini na hizo CV zao kama si aibu tupu na hawana michango kwa jamii ya kitanzania?
 
chadema imejaliwa vipaji vya vijana wasomi Vicent anapwaya sana kwenye elimu ni kama tu jina la Nyerere linamuokoa
 
Huyo Vicent anaonekana ni mtu wa matusi tupu kwa sababu CV yake tu inaonyesha amesoma shule tatu (3) msingi ambazo zote zipo hapo hapo Musoma Mjini inaonekana hana nidhamu.

Nikiunganisha na thread uliyoanzisha kule it tells all..... mlianza na jina la Nyerere, sasa CV yake na nidhamu yake skuli...

Ukichoka kufikiri jua una tatizo kubwa
 
Kuna aina nne za elimu. 1) formal education ambayo tunapata shuleni 2) Informal education ambayo tunapata kupitia maisha ya kila siku 3) Seminar/ au workshop hizi hutolewa kuhusu jambo fulani na huwa za mda mfupi. 4) discipleship/ apprenticeship education ambayo tunapata kutokana na kufuatana na mwalimu mfano ni kwenye magereji, watu wanajifunza kwa kuona jinsi fundi mkuu anategengeneza magari. Wanafunzi wa Yesu na Muhamad walijifunza kupitia njia hii. Siku zote aina ya nne ya elimu ndiyo hasa kile kinachopaswa kuitwa elimu. Ukikumbua akina Socrates, Plato na Aristotle walivyogeuza ulimwengu wa walsafa ilikuwa ni kwa njia hii. Socrates alikuwa mwanafunzi wa Academu ambaye alikuwa mtu wa kwanza kugundua mtihani. Hii ndiyo maana hata leo shule nyingi huchukua jina la academy kama heshima ya Academus. Academu alimfundisha Socrates kwa njia ya utume yaani discipleship. Socrates nay alimfundisha Plato kwa njia hiyo hiyo. Naye Plato alifanya vivyo hivyo kwa Aristotle gwiji wa falsafa.
Je mnaposema Nyerere hakusoma mnamaanisha kwamba hajapitia katika elimu zote hizo. Mbona mnakosa weledi? Je hawa maprofesa wanaojikomba kwa kiingereza kibovu kwenye tv wanafaida gani kwa nchi hii? Je akina Chenge, Lowasa na Rostam walisoma Cambrige wanafaida gani kama kila siku wanahusishwa na ufisadi?
Elimu si darasani tu, elimu ni kila mahali! Kama Nyerere angefanya jambo la kipumbavu, tungesema hajaelimika lakini si kwa kuangalia vyeti bali kuangalia nyanja zote.
Tafuteni hekima katika maamuzi ya mambo haya. Acheni kuvamia mambo, bila kufikiri kwa kina.
Mungu ibariki Tanzania.
 
pima maendeleo ya halmashauri ya manispaa ya mji wa musoma anayoongoza huyu jamaa na maendeleo ya majimbo yanyoongozwa na wasomi (maprofesa, madokta na hata wenye masters zao) kisha utuambie ni yupi mwenye ahueni. Kuwa na elimu kubwa isiyo na manufaa kwa unaowawakilisha au kuwa na elimu ya wastani na kuwasaidia waliokuchagua kuwa mwakilishi wao?
 
Mkapa ni mwizi na muuaji.mwalimu kipindi kile hakua na mafua wala kichomi,walimkuta mzee wa watu yupo zake shambani anapalilia,sasa kwakua mwalimu alikua na tabia ya kufanya checkup ya afya yake mara kwa mara na ilikua ni muda mrefu hakuawahi kufanya huo uchunguzi wa afya yake akaona si vibaya ngoja akacheki.kumbe limkapa limesgafanya mambo yake huko ndio yakawa yaliyokua,kwanza laana lile limtu ndio maana haishi kupigwa na mkewe kila kukicha na kusaidiwa kazi za chumbani,jitu sura mbaya kama mdudu vile.mbona na usomi wake hakuna alilofanya zaidi yakuuza viwanda na raslimali zote za nchi?mkapa ndie mtu wa kwanza kuimajisi ikulu kwani aligeuza kuwa pango la biashara na wanyanganyi,alikua anafanya biashara kitu ambacho mwalimu alikipiga vita kuliko vitu vyote,ukwepaji kodi mkubwa ulianzia kwa mkapa na ufisadi wote wakutisha,epa,meremeta,mchuchuma ,majengo pacha na madudu mengine yote.bora huyu mnae mwita hakusoma alakini anatetea haki za wanyonge na kusimama katika ukweli.wakowapi wasomi kina balali,mramba,chenge,karamagi,rostam na hao mnao amini ni wasomi,wamelifikisha wapi tanzania ya sasa au mnaongozwa na ushabiki tu.nyerere ni msomi mara mia ya mkapa msomi mwizi na muuaji.
 
Afadhali ya Vince Nyerere ana form 4, kuna Livingstone Lusinde na Prof Maji Marefu Ngonyani wameishia darasa la saba tu.

Huyu jamaa Nyerere anatekeleza vizuri sana kazi yake pale Musoma mjini. Ni vizuri kuwa na elimu kubwa kwani hakuna mbadala wa elimu katika dunia ya sasa but tumeona watu kibao wana madigrii ya kumwaga lakini buree kabisa, mfano ni Prof Kapuya au Jumanne Maghembe au Dr Shukuru Kawambwa. Andrew Chenge ana Masters ya sheria, angalia shule ya marehemu Dr Balali...
Vince Nyerere anaimudu vilivyo kazi yake ya ubunge wa Musoma mjini na anawashirikisha katika maamuzi mbalimbali wananchi wake, licha ya kuwa elimu yake ni ya chini ukilinganisha na wengine. Na Elimu kuwa ya kiwango kidogo kulinganisha na wengine haizuii kusema ukweli kama mtu KAMUUA BABA YAKO
 
Mi nna CV kali lakini siajwahi pewa hata uenyekiti wa kitongoji!!!
huyu jamaa pia alikuwa hajawahi kusikika katika siasa za nchi hii kwa sababu inawezekana aliamini nchi imejaa wasomi na watasaidia kutatua (au kujaribu) matatizo yaliyopo.
Miaka inapita na idadi ya wasomi wanazidi kuongezeka kwa kiwango cha juu na umasikini na matatizo yakiongezeka pia, na ndio jamaa ameamua kuingia ulingoni.

Ni mambo mangapi yanaamuliwa utadhani wafanya maamuzi ni watoto wa darasa la pili!? au naye aandike elimu ya bandia kama wafanyavyo wengine!? Ndio maana mimi pia sikujua kama huyu bwana ni Form IV maana delivery capacity yake inawazidi sana hao wasomi. Kikibwa alicho nacho ndicho kile ambacho wengi tunakitafuta na hatujakipata ...KUSEMA UKWELI!

 
mzee elimu ni vyeti au uelewa.

unaweza ukanipa elimu ya zuma
Siyo lazima awe na degree ila hii imezidi angekuwa hata vyeti vya veta angalau kuongezea ongezea. Unajua tuache ushabiki humu JF kumteua Form 4 tena ambaye hatujui kama alifaulu kidato hicho kuwa kampeni meneja ni kututukana watanzania. Lakini tusishangae MBOWE anahitaji watu wa aina hii ili iwe rahisi kumnyenyekea na kupiga magoti. Vicent, Sugu, Lema ni aina ya watu wanao mfaa sana mmafya huyu. Hivi akina Halima mdee elimu zao wanatumiwaje na Chama?
 
Watu wangu wanapotea kwa kukosa maarifa!! Hivi maarifa yanapatikanaje?
 
Msiwe wazandiki na mambumbumbu wa kujua vitu. Kuna watu wamesoma saaaaaaaana lakini hawezi hata kusimama mbele za watu kusema chochote. Kidato cha nne cha VN sio kigezo! Kigezo ana uwezo gani wa kuongoza na kujenga hoja zenye tija kwa jamii! Zamani tulikuwa tunapelekwa pale Kivukoni! Mnakumbuka? Tunaenda kufundishwa propaganda pale.
Kumbuka uongozi ni kipaji na sio kiwango cha elimu!
 
Wenye CV nzuri ni wepi, na wamefanya nini na hizo CV zao kama si aibu tupu na hawana michango kwa jamii ya kitanzania?
Nampenda kijana maana hajadanganya popote,hana vyeti ila ana uwezo waulize akina profesa flani nini walifanyia Taifa?zaidi ya kuiba?
 
Tutegemee matusi matupu sikujua kama jamaa ana elimu ya form 4 alikuwa wapi kujiendeleza

Lakini usisahau kuwa Mhessgimiwa Rais Jk alimtimua marehemu Balali kwa kutokufanya kazi sivyo pamoja na elimu yake
 
Vicent amenajisi elimu kumpa ukampeni meneja Arumeru kama chadema watashinda wategemee CCM kukata rufaa kwa maneno yake likiwemo la Mkapa alimuua Nyerere.

Naona uko busy kupiga porojo kama lilivyo jina lako! Nani alisema ili uwatumikie wananchi lazima uwe na PHD?
 
Back
Top Bottom