"Tulipoamua kupandisha Tozo za Miamala tulikuwa tuna lengo zuri tu ila tulipoanza kusikia Kelele za Wananchi basi Serikali tukaona kwakuwa tunawajali Wananchi wetu tuingilie kati na sasa nimeunda Kamati ili kuliangalia hili na itakuja na majibu muda si mrefu" Rais Samia.
Hasira yangu na Uchungu wangu zaidi haipo katika Kauli nzima bali ni hilo neno tu la 'Kelele' ambalo Mimi nalitafsiri kama vile Rais 'ametudharau' mno na kwamba anataka Watanzania tuwe ni Watu wa kukubali tu kila Kitu ambacho Serikali inaamua.
Kama ni kweli Mheshimiwa Rais Samia alilisema hili neno la 'Kelele' kama alivyonukuliwa popote pale alipo ajue kuwa binafsi 'amenikera' japo huenda Watanzania wengi wakawa 'wameridhika' nalo.
Watu wa Mkoa wa Mara (Musoma) ambao ndiyo 'Mashujaa' wa nchi hii ya Tanzania kuambiwa tuna 'Kelele' ni Kosa Kubwa mno na Dharau japo kwa Watu Washamba wao neno hili huenda wakalifurahia zaidi.
Tata mraaah sijui anawachukuliaje?Yaani Mwanamke kabisa anatuambia Wanamume wa Kikurya, Kizanaki,Kijita na Kijaluo kutoka Mkoani Mara kuwa tuna 'Kelele' Kwake? Hivi Bi Mkubwa hapa alipitiwa tu au alidhamiria?
Nakufahamu kwa muda mrefu humu jukwaani, najua aina yako ya uandishi, imekaa kimasihara sihara but unafikisha UJUMBE, twende mbele na diskasheni kakaNimeandika tu hivyo Mkoa wa Mara ( Musoma ) na Kuwatania hao Watani zangu Wapendwa ( Wajomba na Mashangazi ) kama sehemu tu ya 'Kuunogesha' Uzi ili hata kama tunalijadili hili la Kuambiwa ni Wapiga 'Kelele' lakini pia 'tunapoozana' kwa Kutaniana na Kuchangamshana hapa na pale.
Labda kiswahili cha KIZANZIBAR mkuu.Neno sahihi ambalo lingetumika badala ya kelele ni "malalamiko". Kelele ni sauti ambazo hazina mpangilio na mara nyingi ni za kupuuzwa.
Naandika wapiga kelele hapa JF.
Ninashukuru kwa Kulijua hili kwa Utuo.Nakufahamu kwa muda mrefu humu jukwaani, najua aina yako ya uandishi, imekaa kimasihara sihara but unafikisha UJUMBE, twende mbele na diskasheni kaka
Yupo kama yezebeli mke wa ahabuKuna Mwandamizi Mmoja kutoka Zanzibar na ambaye kafanya nae Kazi Serikalini na mpaka katika Bunge la Katiba alikuwa nae aliniambia kuwa 'Mama' ana 'Dharau' sana na maneno ya 'Karaha' nikamkatalia ila sasa nayashuhudia Mwenyewe ' mubashara' kabisa.
Sasa Mura nakushauri usikae karibu na panga, unaweza kumgecha yeyote na hiyo silaha yakoNikiwa kama mwana Mkoa wa Mara ( Musoma ) hili neno la Kuambiwa tuna 'Kelele' tena na Mwanamke limeniumiza na kunipandisha sana Hasira zangu za 'Kichuri' Mkuu.
Au ataambiwa na yeye aende kitunda akauuze mayai kwenye Baiskeli Kama wa Wakulya wenzie huko kitunda!!Hili ndio neno. Na huo ndio uanaume. Kama wewe ni wa mara bila kuingia barabarani. Humu unapiga kelele tu. Mwisho ataambiwa hamia burundi kwa kelele zako
Wamekura sasa wamevimbilwa wanaanza kutujambia kisha wanatulazimisha tucheke washenzi sana