Kuwepo au Kutokuwepo; wote wapo

Kuwepo au Kutokuwepo; wote wapo

Huyu aliyepo hii leo ndiye asiye kuwepo badae na asiye kuwepo ndiye aliyepo. Hiki unachokiona leo siyo hicho walichokiona waliokuwepo, lakini ndiyo hicho kilichopo, ambacho kila aliyekuwepo, anayekuwepo na atakaye kuwepo anacho.

Wewe upo kwasababu wao walikuwepo na kwasababu walikuwepo na wewe upo na hivyo wote mpo.

Ukisema kwa sababu walikuwepo hivyo hawapo sasa maana yake na wewe haukuwepo na haupo sasa. Kama unasema walikuwepo, lakini sasa hawapo maana yake wewe pia hukuwepo ndiyo sababu unaona hawapo.

Ukiwa mwanadamu tayari umekuwepo na hivyo haiwezekani kwamba hautakuwepo.

Mtu aliyepo anawezaje kusema hayupo angali yupo? Vivyohivyo kwa aliyekuwepo atawezaje kutokuwepo? Aliyekuwepo ndiye aliyepo nae atakuwepo. Vivyohivyo kwa aliyepo ndiye yupo na atakuwepo.

Kama huyo hayupo maana yake na wewe haupo, lakini kama wewe upo na yeye yupo. Unawezaje kusema, yeye hayupo, lakini wewe upo?

Kama mtu huzaliwa na aliye kuwepo na yeye huyo anaezaliwa huwapo nae akisha kuwapo huzaa atakae kuwepo. Sasa ni nani kati hawa anaeweza kudai huyu hayupo?

Hivyo hakuna awezae kuwepo kama aliyekuwepo, aliyepo na atakayekuwepo hajaweza kuwepo na hivyo aliyekuwepo yupo, atakuwepo na kwasababu yupo nasi tupo.
Hizo po zimetufanya tusielewe
 
Ni kwamba aliyekwisha kuwepo hato weza kuwa hayupo tena na kwa vile alikuzaa wewe nawe pia ulikuwepo naye katika uwepo wake, hivyo basi hakuna asiye kuwepo aliyekwisha kuwepo.
 
Kama mtu huzaliwa na aliye kuwepo na yeye huyo anaezaliwa huwapo nae akisha kuwapo huzaa atakae kuwepo. Sasa ni nani kati hawa anaeweza kudai huyu hayupo?

Hivyo hakuna awezae kuwepo kama aliyekuwepo, aliyepo na atakayekuwepo hajaweza kuwepo na hivyo aliyekuwepo yupo, atakuwepo na kwasababu yupo nasi tupo. [emoji848][emoji848][emoji848][emoji848][emoji848][emoji115][emoji115][emoji115][emoji115][emoji144][emoji144][emoji144][emoji144][emoji144]
Pia ile siku na saa isiyojulikana ikiwadia basi nasi hatuto kuepo tena.
 
Is this all about reincarnation?? Kufa na kuzaliwa kama kiumbe/mtu mwingine??
Someone??
 
Asante nundu-, kwa andiko zuri lenye kufikirisha.
Maisha yanatawaliwa na
Uwepo.
Bila Uwepo hakuna maisha, ndio maana huyu Mungu wa Ibrahim Issaka na Yakobo ailiyeumba Uwepo yeye ndiye asili ya Uwepo.

Musa alipomwuliza
" Wewe unayejiita Mungu Jina lako unaitwa Nani kwa Jina ? "

Akajibu Mimi naitwa
NIKO AMBAYO NIKO.

Sehemu nyingine anajitambulisha Kama
MIMI NDIYE,
KABLA YA IBRAHIMU MIMI NIKO,
ALFA NA OMEGA yaani mwanzo na Mwisho.
BWANA WA MILELE
NK.
Nirudi kwa sisi Binadamu,
Binadamu pia wamerithishwa tabia ya ya UWEPO na Mungu.
Ila wao sio Alfa kwakuwa Wana mwanzo pale walipoumbwa.
Nikianza na kimwili hasa kwa sisi Waafrika, toka Adamu wetu azaliwe pale na kuishia pale Oduvai Gorge, ameendelaea kuishia hadi leo kwani bado damu yake unaishi hadi sasa ambayo ndio sisi.
Ni kosa Mwanadamu kujibu SIPO, au HATUPO.
Mtu anakuuliza kwenye simu uko wapi unajibu SIPO, hili nikosa.
Ukiulizwa uko wapi jibu
Niko Mjini au Kazini au Shambani au Nyumbani au sema ukweli nipo Guest House. NK.
Nirudi Kiroho, tunasoma Mungu alipomwumba Mwanadamu akampukizia Pumzi ya Uhai.
Hii Pumzi ya Mungu ya Uhai ni kitu cha thamani Sana sana kuliko MWILI. Hii ndiyo inayoitwa Roho inayojitambulisha Kama Nafsi.
Ukisikia watu wanasafiri kwa kumeditate ndiyo wanaitumia hii Pumzi ambayo ndo Uhai wenyewe kimwili wanauacha kitandani.
Yesu Kristo alipata kuwaambia wafuasi wake
"Msiwaogope wanawaua mwili bali mwogopeni mwenye uwezo wa kuiua Roho.
Na anasema pia

" Mtu aniaminiye Mimi hata akifa ataishi "
"Asiyeniamini hakika atakufa"
yaani Roho yake itauwawa na aliyeitengeneza.
Hapa analenga maisha ya umilele ya Kiroho.

Sehemu nyingine Yesu anasema,
"Waacheni Wafu wakawazike Wafu wao"
Kwani hao maisha yao yanakikomo pale wanapozikwa na kufa Kiroho.
Na akajitapa mahali kwa kusema,
Mimi NDIYE,
NJIA, KWELI NA UZIMA.
Hili pia ni Jina la Mungu.
Na hakuna kiumbe kilichokanusha hii sifa aliyojitapa Yesu Kristo, wala kuiga kujiita hivyo hadi hii leo.
ASANTE SANA.

Hivyo mleta nundu, mada hongera Sana kwa kuleta mada very Philosophic and Real.
 
Kwa kifupi ni kwamba, nothing comes 0ut of nothing, kwa kibongo, kama sijakosea ni" hakuna kitokeacho bila sababu"
 
Nafikiri ni ithabati ya wana sayansi wa middle ages..
And i think they were right..!!
 
Yes bro...!![emoji106][emoji106]
Bro, nimekimbia kwa muda kule nilipouliza, idhabati alizotumia Nuhu, kama ndio ilikua Mwanzo wa idhabati wanazotumia injinia wetu wa sasa, yaani sikutegemea watu wanavyo respond..[emoji23][emoji23]
Ila nimepata jibu kwa nini wanafunzi wana feli universties nyingi..[emoji41][emoji41]
 
Kama mtu huzaliwa na aliye kuwepo na yeye huyo anaezaliwa huwapo nae akisha kuwapo huzaa atakae kuwepo. Sasa ni nani kati hawa anaeweza kudai huyu hayupo?

Hivyo hakuna awezae kuwepo kama aliyekuwepo, aliyepo na atakayekuwepo hajaweza kuwepo na hivyo aliyekuwepo yupo, atakuwepo na kwasababu yupo nasi tupo. [emoji848][emoji848][emoji848][emoji848][emoji848][emoji115][emoji115][emoji115][emoji115][emoji144][emoji144][emoji144][emoji144][emoji144]
Daah afadhali kidogo nimepata mwanga
 
Umeandika vyema sana.
Kufafanua maana ya nilichoandika. Kwanza kwa mtazamo wa kisayansi.
Kisayansi kila mtu aliezaliwa anarithi asilimia 50 ya chembechembe za mwili (DNA) kutoka kwa wazazi wake: watangulizi wake.
Hii maana yake ni kwamba, watoto hufanana kwa namna mbili na wazazi au watangulizi wao.
Kwanza,ni kwa namna ya maumbile: mwili. Ukitazama watoto na kisha ukatazama watangulizi wao (wazazi) utaona na kugundua wanafanana kimwili: maumbo na viungo.
Pili, ni kwa namna ya mwenendo au tabia na matendo. Wachunguze watoto, haiwezekani wakafanya matendo ambayo wazazi au watangulizi wao hawakuyafanya. Kwa mfano kama watangulizi (wazazi) walikuwa walevi, washerati, washirikina, wezi, wapole, wema au wachangamufu, watapatikana watoto wenye tabia hizo.
Kwa sababu hii (DNA) hatuoni waliokuwepo hawapo, tunao na wanaendelea kuwepo.
Aisee, shule kubwa hii
 
Back
Top Bottom