Embu tutafakari kidogo

Embu tutafakari kidogo

Thecoder

JF-Expert Member
Joined
Aug 10, 2015
Posts
2,380
Reaction score
6,142
Ukivuliwa tabaka zote za kumbukumbu ulizozikusanya kwa miaka mingi, ni kitu gani hasa kitabaki kukufanya uwe wewe?

Embu tafakari kwa kina hapa…
Huenda unachokiita akili si chochote zaidi ya maktaba ya mabaki ya jana iliyojificha ndani ya ubongo wako.

Maana mwanadamu haishi kwa kile anachokijua sasa, bali kwa kivuli cha yale yaliyokwisha pita.

Angalia, elimu yako ni marejeo ya kale,

Lugha yako ni mwangwi wa sauti zilizotamkwa kabla yako, Mwendo wako, maamuzi yako, hofu zako, imani zako na hata namna unavyoitazama dunia, vyote vimefungwa kwenye masanduku ya historia yaliyohifadhiwa kichwani mwako.

Ndiyo maana jamii humuita mtu huyu mwenye akili na mwingine asiye na akili kwa kupima ukubwa wa hazina ya marejeo aliyobeba.

Angalia hapa…
Daktari huitwa bingwa kwa sababu amehifadhi simulizi za magonjwa yaliyopita.

Mwanasheria hushinda kesi kwa sababu ameweza kuvuta kivuli cha hukumu za jana na kuzileta leo.

Na ushahidi wenyewe ni nini kama si mabaki ya jambo lililokwisha kufanyika muda uliopita?

Kwa kifupi ni kwamba hakuna hoja inayokubalika bila kupewa kaburi la zamani ili iweze kulalia.

Ndio maana ukisema jambo ambalo halijawahi kutokea, dunia hukutazama kama mwendawazimu. Lakini ukisema jambo ambalo lilishawahi kutokea, hata kama ni la kipuuzi, watu hulipa heshima fulani kwa sababu lina historia.

Ndiyo maana dunia yote inaonekana kana kwamba haiishi kuanzia sasa kwenda mbele, bali inaishi ndani ya makumbusho ya mambo yaliyopita na sasa. Kwasababu kila mfumo umejengwa juu ya ibada ya jana.

Leo hii mtu akikwambia ametoka sehemu unayoifahamu, hutaki kumuamini mpaka akupe alama za kale unazozijua zipo kwenye eneo hilo, akizitoa kwa namna sahihi, unaamini vinginevyo huwezi muamini.

Na hapo ndipo siri kubwa ilipojificha, ya kwamba binadamu haamini ukweli hadi uwe ule unaofanana na kumbukumbu zake au zozote zile za kale.

Na kwa sababu hiyo, sayansi nayo si kitu kingine isipokuwa historia iliyokataa kufa.
Historia ya kawaida huzikwa kwenye jana.

Lakini sayansi ni historia inayojirudia kwa nidhamu maalum hadi watu waiite sheria.

Mfano, mvua ilinyesha jana, ikarudia leo, ikitarajiwa kesho ndio tunasema kuna mfumo wa kisayansi unaoweza kuelezea mvua, kutokana na kujirudia rudia kwa tabia zile zile Kila mvua inapotaka kunyesha, lakini msingi wake bado ni ule ule, kumbukumbu ya yaliyopita.

Ila dunia ikikutana na jambo lisilo na mizizi kwenye jana. Kwa mfano, ugonjwa ambao hauna mfano wowote uliowahi kuwepo, usio na pattern, usiorudia tabia, usiokubali kuhifadhiwa kwenye rekodi.
Ndipo utaona namna akili zote zitakavyosimama pasinakujua wapi waanzie na wapi wamalizie.

Kwa sababu uwezo wa mwanadamu haujazoea kuumba kutoka mwanzo, ila umezoea kurejea kutoka kwenye kile ambacho tayari kilishakuwepo.

Hata AI mnayoihofia leo, haifanyi kazi kwa kuona kesho bali inavuta vipande vya jana na kuvipanga upya ila yenyewe hufanya kwa kasi kubwa kuliko mwanadamu.

Kwahiyo, future ndiyo eneo pekee ambalo akili hushindwa kutawala, ndiyo maana kesho hubaki kuwa fumbo na jana hubaki kuwa mwalimu na kipimo cha werevu.

Ukifaulu mtihani kwa A zote, huenda hukua na akili kuliko wengine bali huenda ulikuwa na uwezo mkubwa zaidi wa kubeba mizoga ya taarifa za zamani kichwani mwako na hii ikafanya ukaitwa genius kwa sababu uliweza kukariri historia kwa usahihi mkubwa kuliko waliokaa pembeni yako.

Na hapa ndipo dunia ilipojenga mfumo wake wa ulinzi.

Kwamba, ukileta hoja isiyo na kumbukumbu ya zamani, wenye dini watakuambia unakufuru ikiwa imelenga upande huo na ukileta mbele ya wasomi, watakuambia thibitisha.

Na kuthibitisha huko maana yake ni nini?
Wanataka urudi jana ukatafute ushahidi.

Ukishindwa kufanya hivyo, hoja yako hufa kabla hata haijasikilizwa.

Ndiyo maana watu wengi hurudi kwa hiari ndani ya gereza la kawaida la fikra, gereza la historia. Kwa sababu huko hakuna pingamizi na ni sehemu salama ya akili zinazohitaji kivuli cha jana ili ziweze kupumua.

Lakini swali ambalo wengi hawathubutu kujiuliza ni hili…
Je, ni nani aliyeufuma mfumo huu wa kuabudu yaliyopita?

Kwa nini dunia inaonekana kana kwamba inaruhusu kujua kile kilichokwisha kuwepo pekee, na inazuia kufikiri kuhusu kile ambacho hakijawahi kuwepo?

Kana kwamba kuna ukuta usioonekana unaozuia akili kuvuka mipaka ya historia, na dunia pamoja na mifumo yake yote hufanya juu chini kuulinda ukuta huo usionekane.

Na huenda ndio maana hakuna jipya chini ya jua, na si kwa sababu mambo mapya hayawezi kutokea, hapana, bali kwa sababu akili nyingi zimefungwa ndani ya maktaba ya jana kiasi kwamba haziwezi kutambua kile ambacho hakina kumbukumbu.

Imani yangu inaniambia sisi ni bora ya zaidi ya hivi tulivyo, ila ni vile tumefungwa kwenye eneo ambalo halitupi mwanya wa kuona zaidi ya vile ambavyo tunalazimishwa tuvione.

Ndio maana nasema, ukifutiwa kila ulilowahi kujifunza, kila uso uliowahi kuuona, kila neno ulilowahi kusikia… usingebaki na akili bali ungebaki na utupu unaohitaji kufundishwa historia upya ili uweze kuruhusiwa kuishi tena ndani ya mfumo wa dunia kwasababu akili unayohisi uko nayo huna bali imetengenezwa na kuwa shaped kinamna ile dunia inataka iwe.
 
ukiangalia weather ni zile zile maisha tunayoishi ukisoma historia ya watu wa zamani sana kama watu wa Messepotamia utaona ni maisha yale yale mpaka tech walizotumia ni kama tunacopy kwao, mzunguka wa jua unakuwa unatabirika sababu ni una pattern

Ni kama vile kila kitu kinasabibishwa na kitu nyuma yake, ulimwengu wa vitu unaojirudia hakuna mwanzo wala mwisho sababu mwanzo umetokana na mwisho na mwisho umetokana na mwanzo, Big Cycle ya maisha, Ma buddha walijua hizi ishu ndio maana min -me anawakubali sana
 
Alafu Thecoder kuna ile hali nyingine ya ajabu huwa inatokea mfano umewaza kitu fulani hujatoa wala kusikia sehemu yoyote ile halafu baada ya muda unakuta hilo wazo kuna mtu alishawahi kulizungumzia zamani kidogo,

My take ni kama vile kila information ya ulimwengu mzima umekuwa incoded kwenye akili zetu hivyo ni sisi tu kutoa hzo taarifa, kuna watu wanajua jinsi ya tap in kwenye akili zao na kutoa hzo info
Sababu kama kila kitu kimetokana na the same matter na energy hivyo ile connection bado ipo
 
Ukivuliwa tabaka zote za kumbukumbu ulizozikusanya kwa miaka mingi, ni kitu gani hasa kitabaki kukufanya uwe wewe?

Embu tafakari kwa kina hapa…
Huenda unachokiita akili si chochote zaidi ya maktaba ya mabaki ya jana iliyojificha ndani ya ubongo wako.

Maana mwanadamu haishi kwa kile anachokijua sasa, bali kwa kivuli cha yale yaliyokwisha pita.

Angalia, elimu yako ni marejeo ya kale,

Lugha yako ni mwangwi wa sauti zilizotamkwa kabla yako, Mwendo wako, maamuzi yako, hofu zako, imani zako na hata namna unavyoitazama dunia, vyote vimefungwa kwenye masanduku ya historia yaliyohifadhiwa kichwani mwako.

Ndiyo maana jamii humuita mtu huyu mwenye akili na mwingine asiye na akili kwa kupima ukubwa wa hazina ya marejeo aliyobeba.

Angalia hapa…
Daktari huitwa bingwa kwa sababu amehifadhi simulizi za magonjwa yaliyopita.

Mwanasheria hushinda kesi kwa sababu ameweza kuvuta kivuli cha hukumu za jana na kuzileta leo.

Na ushahidi wenyewe ni nini kama si mabaki ya jambo lililokwisha kufanyika muda uliopita?

Kwa kifupi ni kwamba hakuna hoja inayokubalika bila kupewa kaburi la zamani ili iweze kulalia.

Ndio maana ukisema jambo ambalo halijawahi kutokea, dunia hukutazama kama mwendawazimu. Lakini ukisema jambo ambalo lilishawahi kutokea, hata kama ni la kipuuzi, watu hulipa heshima fulani kwa sababu lina historia.

Ndiyo maana dunia yote inaonekana kana kwamba haiishi kuanzia sasa kwenda mbele, bali inaishi ndani ya makumbusho ya mambo yaliyopita na sasa. Kwasababu kila mfumo umejengwa juu ya ibada ya jana.

Leo hii mtu akikwambia ametoka sehemu unayoifahamu, hutaki kumuamini mpaka akupe alama za kale unazozijua zipo kwenye eneo hilo, akizitoa kwa namna sahihi, unaamini vinginevyo huwezi muamini.

Na hapo ndipo siri kubwa ilipojificha, ya kwamba binadamu haamini ukweli hadi uwe ule unaofanana na kumbukumbu zake au zozote zile za kale.

Na kwa sababu hiyo, sayansi nayo si kitu kingine isipokuwa historia iliyokataa kufa.
Historia ya kawaida huzikwa kwenye jana.

Lakini sayansi ni historia inayojirudia kwa nidhamu maalum hadi watu waiite sheria.

Mfano, mvua ilinyesha jana, ikarudia leo, ikitarajiwa kesho ndio tunasema kuna mfumo wa kisayansi unaoweza kuelezea mvua, kutokana na kujirudia rudia kwa tabia zile zile Kila mvua inapotaka kunyesha, lakini msingi wake bado ni ule ule, kumbukumbu ya yaliyopita.

Ila dunia ikikutana na jambo lisilo na mizizi kwenye jana. Kwa mfano, ugonjwa ambao hauna mfano wowote uliowahi kuwepo, usio na pattern, usiorudia tabia, usiokubali kuhifadhiwa kwenye rekodi.
Ndipo utaona namna akili zote zitakavyosimama pasinakujua wapi waanzie na wapi wamalizie.

Kwa sababu uwezo wa mwanadamu haujazoea kuumba kutoka mwanzo, ila umezoea kurejea kutoka kwenye kile ambacho tayari kilishakuwepo.

Hata AI mnayoihofia leo, haifanyi kazi kwa kuona kesho bali inavuta vipande vya jana na kuvipanga upya ila yenyewe hufanya kwa kasi kubwa kuliko mwanadamu.

Kwahiyo, future ndiyo eneo pekee ambalo akili hushindwa kutawala, ndiyo maana kesho hubaki kuwa fumbo na jana hubaki kuwa mwalimu na kipimo cha werevu.

Ukifaulu mtihani kwa A zote, huenda hukua na akili kuliko wengine bali huenda ulikuwa na uwezo mkubwa zaidi wa kubeba mizoga ya taarifa za zamani kichwani mwako na hii ikafanya ukaitwa genius kwa sababu uliweza kukariri historia kwa usahihi mkubwa kuliko waliokaa pembeni yako.

Na hapa ndipo dunia ilipojenga mfumo wake wa ulinzi.

Kwamba, ukileta hoja isiyo na kumbukumbu ya zamani, wenye dini watakuambia unakufuru ikiwa imelenga upande huo na ukileta mbele ya wasomi, watakuambia thibitisha.

Na kuthibitisha huko maana yake ni nini?
Wanataka urudi jana ukatafute ushahidi.

Ukishindwa kufanya hivyo, hoja yako hufa kabla hata haijasikilizwa.

Ndiyo maana watu wengi hurudi kwa hiari ndani ya gereza la kawaida la fikra, gereza la historia. Kwa sababu huko hakuna pingamizi na ni sehemu salama ya akili zinazohitaji kivuli cha jana ili ziweze kupumua.

Lakini swali ambalo wengi hawathubutu kujiuliza ni hili…
Je, ni nani aliyeufuma mfumo huu wa kuabudu yaliyopita?

Kwa nini dunia inaonekana kana kwamba inaruhusu kujua kile kilichokwisha kuwepo pekee, na inazuia kufikiri kuhusu kile ambacho hakijawahi kuwepo?

Kana kwamba kuna ukuta usioonekana unaozuia akili kuvuka mipaka ya historia, na dunia pamoja na mifumo yake yote hufanya juu chini kuulinda ukuta huo usionekane.

Na huenda ndio maana hakuna jipya chini ya jua, na si kwa sababu mambo mapya hayawezi kutokea, hapana, bali kwa sababu akili nyingi zimefungwa ndani ya maktaba ya jana kiasi kwamba haziwezi kutambua kile ambacho hakina kumbukumbu.

Imani yangu inaniambia sisi ni bora ya zaidi ya hivi tulivyo, ila ni vile tumefungwa kwenye eneo ambalo halitupi mwanya wa kuona zaidi ya vile ambavyo tunalazimishwa tuvione.

Ndio maana nasema, ukifutiwa kila ulilowahi kujifunza, kila uso uliowahi kuuona, kila neno ulilowahi kusikia… usingebaki na akili bali ungebaki na utupu unaohitaji kufundishwa historia upya ili uweze kuruhusiwa kuishi tena ndani ya mfumo wa dunia kwasababu akili unayohisi uko nayo huna bali imetengenezwa na kuwa shaped kinamna ile dunia inataka iwe.
Lakini ukisema jambo ambalo lilishawahi kutokea, hata kama ni la kipuuzi, watu hulipa heshima fulani kwa sababu lina historia.
 
Alafu Thecoder kuna ile hali nyingine ya ajabu huwa inatokea mfano umewaza kitu fulani hujatoa wala kusikia sehemu yoyote ile halafu baada ya muda unakuta hilo wazo kuna mtu alishawahi kulizungumzia zamani kidogo,

My take ni kama vile kila information ya ulimwengu mzima umekuwa incoded kwenye akili zetu hivyo ni sisi tu kutoa hzo taarifa, kuna watu wanajua jinsi ya tap in kwenye akili zao na kutoa hzo info
Sababu kama kila kitu kimetokana na the same matter na energy hivyo ile connection bado ipo
Yeah, Dunia haijawahi umbwa mara mbili, so info huwa zipo kulingana na zama husika, ingawa justification ni nyingi katika pande zote za kidini na kisayansi ili kuzuia uhalisia ila nadhani tuko very powerful kuliko hivi tulivyo that's why ni kama universe imeamua kutuwekea mipaka fulani ili kutufanya tuweze kubaki kwenye boksi lile lile zama hadi zama.
 
ukiangalia weather ni zile zile maisha tunayoishi ukisoma historia ya watu wa zamani sana kama watu wa Messepotamia utaona ni maisha yale yale mpaka tech walizotumia ni kama tunacopy kwao, mzunguka wa jua unakuwa unatabirika sababu ni una pattern

Ni kama vile kila kitu kinasabibishwa na kitu nyuma yake, ulimwengu wa vitu unaojirudia hakuna mwanzo wala mwisho sababu mwanzo umetokana na mwisho na mwisho umetokana na mwanzo, Big Cycle ya maisha, Ma buddha walijua hizi ishu ndio maana min -me anawakubali sana
Hakuna kipya chochote chini ya jua coz kwa jinsi tulivyo huwa hatuumbi kuanzia mwanzo ila tunaumba juu ya uumbaji fulani ambao tayari ulishawahi kuwepo, so kilichopo sasa yawezekana kilishawahi kuwepo na hakitakua ndio mwisho wake bali kitaendelea kuwepo tena na tena... Angalia tu hata kwenye hali za kawaida kuna vitu vingi ambavyo vinapotea halafu ghafla unaviona vinarudi tena kwenye trend coz siku zote tupo kama hivyo.
 
Yeah, Dunia haijawahi umbwa mara mbili, so info huwa zipo kulingana na zama husika, ingawa justification ni nyingi katika pande zote za kidini na kisayansi ili kuzuia uhalisia ila nadhani tuko very powerful kuliko hivi tulivyo that's why ni kama universe imeamua kutuwekea mipaka fulani ili kutufanya tuweze kubaki kwenye boksi lile lile zama hadi zama.
we unahisi ni kipi kinatuzuia kufika potential yetu ni elimu au nishati tuliyonayo bado ni ndogo maana kama uki view ulimwengu ki tech ni kama quantum computer kubwa yenye nguvu hivyo kama tukiwa na nishati kubwa tutakuwa na uwezo wa kutengeneza vitu vikubwa na ku match uwezo na ulimwengu
 
we unahisi ni kipi kinatuzuia kufika potential yetu ni elimu au nishati tuliyonayo bado ni ndogo maana kama uki view ulimwengu ki tech ni kama quantum computer kubwa yenye nguvu hivyo kama tukiwa na nishati kubwa tutakuwa na uwezo wa kutengeneza vitu vikubwa na ku match uwezo na ulimwengu
Nadhani ni ulimwengu tu wenyewe ndio uko hivyo kwa maana hata elimu iliyopo na maamuzi ya ulimwengu wenyewe, sometimes huwa nafikiria labda ni kwa namna ile ile ya wewe ukiwa na nyumba yako kubwa then ukaweka utaratibu fulani wa namna ya watu wanavyopaswa kuishi kwenye nyumba hiyo, chumba kipi wafungue na chumba kipi wasifungue, walala saa ngapi na waamke saa ngapi, wengi wakifanikiwa kuingia kwenye mfumo wako watakua wanawakumbusha hata wale wachache ambao watakua wanapingana na sheria husika hadi nao kujikuta wanaingia kwenye mfumo ule ule ambao wewe umeuweka
 
Nadhani ni ulimwengu tu wenyewe ndio uko hivyo kwa maana hata elimu iliyopo na maamuzi ya ulimwengu wenyewe, sometimes huwa nafikiria labda ni kwa namna ile ile ya wewe ukiwa na nyumba yako kubwa then ukaweka utaratibu fulani wa namna ya watu wanavyopaswa kuishi kwenye nyumba hiyo, chumba kipi wafungue na chumba kipi wasifungue, walala saa ngapi na waamke saa ngapi, wengi wakifanikiwa kuingia kwenye mfumo wako watakua wanawakumbusha hata wale wachache ambao watakua wanapingana na sheria husika hadi nao kujikuta wanaingia kwenye mfumo ule ule ambao wewe umeuweka
Kisha unatengeneza necessity ya watu kuishi kwenye nyumba yako hakuna kuhama na hakuna kujua ulijengaje hyo nyumba incase mtu atataka kutengeneza nyumba yake.

Sababu ingredient kubwa ni dark energy ndio haijulikani, hivyo kama future scientist wakigundua dark energy ni nini na.kwa sasa wanaweza ku manifest matter japokuwa bado ni quantum scale na inakaa muda mfupi, ila wakiweza unafikiri wataweza kutengeza man made celestial body au hayo ni mambo ya nature hatutafika huko tuache mikononi kwa Nature tu
 
Kisha unatengeneza necessity ya watu kuishi kwenye nyumba yako hakuna kuhama na hakuna kujua ulijengaje hyo nyumba incase mtu atataka kutengeneza nyumba yake.

Sababu ingredient kubwa ni dark energy ndio haijulikani, hivyo kama future scientist wakigundua dark energy ni nini na.kwa sasa wanaweza ku manifest matter japokuwa bado ni quantum scale na inakaa muda mfupi, ila wakiweza unafikiri wataweza kutengeza man made celestial body au hayo ni mambo ya nature hatutafika huko tuache mikononi kwa Nature tu
Yeah yaani wewe ndio unaamua kipi kiwepo na kipi kisiwepo na kipi kijulikane kipi kisijulikane... Kuna ile hadithi ya sodoma na gomola ila pia kuna ile hadithi ya wana wa Mungu kuzaa na wana wa Adam, ila pia kuna ile hadithi ya mnara wa Babel, hizi hadithi zote ukizisoma vizuri utaona ni kama wingi wa maarifa ambao ulitokea hizo zama ndio ambao ulipelekea dunia iende kwenye mabadiliko ya lazima kwa maana nyingine ni kwamba inajifanyia reset ili ianze upya, and if so basi ni ngumu kufikia level iliyobeyond na limit iliyowekwa na universe yenyewe, but Mimi binafsi natamani kuona hiyo ikifanikiwa ili tuweze kuona after hapo muitikio gani ambao universe itatupatia😅
 
Kuna ile hadithi ya sodoma na gomola ila pia kuna ile hadithi ya wana wa Mungu kuzaa na wana wa Adam, ila pia kuna ile hadithi ya mnara wa Babel, hizi hadithi zote ukizisoma vizuri utaona ni kama wingi wa maarifa ambao ulitokea hizo zama ndio ambao ulipelekea dunia iende kwenye mabadiliko ya lazima
Dah! Kama ina ukweli ndani yake
Mimi binafsi natamani kuona hiyo ikifanikiwa ili tuweze kuona after hapo muitikio gani ambao universe itatupatia
Mi pia ningependa sana kuona hivyo
 
Dah! Kama ina ukweli ndani yake

Mi pia ningependa sana kuona hivyo
Yeah hayo maandiko yote yanaelezea waziwazi ya kwamba hizo nyakati zote ni nyakati ambazo Dunia ilipitia mabadiliko makubwa ya uelewa wa mambo miongoni mwa watu.

Watu walikua wanafanya vitu ambavyo vilikua beyond limitations ambazo ulimwengu wenyewe umejiwekea ili kujilinda.

And now pia tupo kwenye kipindi kikubwa cha mabadiliko watu wako very open-minded ila pia wako huru kushare bila kuhofia kama ambavyo ilikua hapo awali kwasababu kuna kauhuru fulani ka ndani watu wako nacho.

Fikra nyingi zamani zilikua zinamezwa kwenye kivuli cha Imani, hasa zile zinazohusiana na maswala ya uumbaji wa mtu, vitu na ulimwengu kwa ujumla so watu walikua hawajipi uhuru wa kuacha akili zao zielekee huko kama ambavyo hivi sasa ilivyo.

Ndio maana utaona watu wanagawa vizazi kwa zama na kwa jinsi inavyoonekana kizazi kilizoanzia miaka ya 2000 ndio kizazi ambacho kipo huru zaidi ya vizazi vilivyotangulia, ni kizazi ambacho hakifuati sheria kwa lazima, ni kizazi ambacho kinapenda kujaribu maonyo yaani vile vitu ambavyo watu husema ni mwiko or dhambi wao ndio wanapita navyo ili waone venye inakua, so hii ni dalili moja wapo ya kukuonesha kwamba ni kizazi ambacho kipo huru sana kifikra.

Lakini hapo hapo kwakua ndio tunaelekea huko basi universe yenyewe imeamua kujilinda kwa kumake sure uhuru wa fikra uliopo hauwezi kuwa huru katika namna ya ukomavu kwa maana Kila kitu kipo simplified so badala ya wewe kuukomaza ubongo wako kifikra unaiachia AI ikusaidie kufikiria na vitu kama hivyo.

Kwahiyo kila zama za mabadiliko yenye athari ya moja kwa moja au yatakayokuwa na athari ya moja kwa moja kwenye universe lazima kuwe na defensive mechanism ya kuendelea kukufanya ubaki pale pale, so hakuna jambo lolote la bahati mbaya au la maamuzi binafsi au la ongezeko la akili zilizopo duniani, linaloweza kutokea pasipo universe yenyewe kuamua na endapo itaamua ujue ni katika mlengo huo wa defensive au pumbazo.
 
Yeah hayo maandiko yote yanaelezea waziwazi ya kwamba hizo nyakati zote ni nyakati ambazo Dunia ilipitia mabadiliko makubwa ya uelewa wa mambo miongoni mwa watu.

Watu walikua wanafanya vitu ambavyo vilikua beyond limitations ambazo ulimwengu wenyewe umejiwekea ili kujilinda.

And now pia tupo kwenye kipindi kikubwa cha mabadiliko watu wako very open-minded ila pia wako huru kushare bila kuhofia kama ambavyo ilikua hapo awali kwasababu kuna kauhuru fulani ka ndani watu wako nacho.

Fikra nyingi zamani zilikua zinamezwa kwenye kivuli cha Imani, hasa zile zinazohusiana na maswala ya uumbaji wa mtu, vitu na ulimwengu kwa ujumla so watu walikua hawajipi uhuru wa kuacha akili zao zielekee huko kama ambavyo hivi sasa ilivyo.

Ndio maana utaona watu wanagawa vizazi kwa zama na kwa jinsi inavyoonekana kizazi kilizoanzia miaka ya 2000 ndio kizazi ambacho kipo huru zaidi ya vizazi vilivyotangulia, ni kizazi ambacho hakifuati sheria kwa lazima, ni kizazi ambacho kinapenda kujaribu maonyo yaani vile vitu ambavyo watu husema ni mwiko or dhambi wao ndio wanapita navyo ili waone venye inakua, so hii ni dalili moja wapo ya kukuonesha kwamba ni kizazi ambacho kipo huru sana kifikra.

Lakini hapo hapo kwakua ndio tunaelekea huko basi universe yenyewe imeamua kujilinda kwa kumake sure uhuru wa fikra uliopo hauwezi kuwa huru katika namna ya ukomavu kwa maana Kila kitu kipo simplified so badala ya wewe kuukomaza ubongo wako kifikra unaiachia AI ikusaidie kufikiria na vitu kama hivyo.

Kwahiyo kila zama za mabadiliko yenye athari ya moja kwa moja au yatakayokuwa na athari ya moja kwa moja kwenye universe lazima kuwe na defensive mechanism ya kuendelea kukufanya ubaki pale pale, so hakuna jambo lolote la bahati mbaya au la maamuzi binafsi au la ongezeko la akili zilizopo duniani, linaloweza kutokea pasipo universe yenyewe kuamua na endapo itaamua ujue ni katika mlengo huo wa defensive au pumbazo.
Kwa hyo hatuko mbali na tukio la kungamiza
Ila nahisi this time itakuwa tofauti kidogo
 
Ukivuliwa tabaka zote za kumbukumbu ulizozikusanya kwa miaka mingi, ni kitu gani hasa kitabaki kukufanya uwe wewe?

Embu tafakari kwa kina hapa…
Huenda unachokiita akili si chochote zaidi ya maktaba ya mabaki ya jana iliyojificha ndani ya ubongo wako.

Maana mwanadamu haishi kwa kile anachokijua sasa, bali kwa kivuli cha yale yaliyokwisha pita.

Angalia, elimu yako ni marejeo ya kale,

Lugha yako ni mwangwi wa sauti zilizotamkwa kabla yako, Mwendo wako, maamuzi yako, hofu zako, imani zako na hata namna unavyoitazama dunia, vyote vimefungwa kwenye masanduku ya historia yaliyohifadhiwa kichwani mwako.

Ndiyo maana jamii humuita mtu huyu mwenye akili na mwingine asiye na akili kwa kupima ukubwa wa hazina ya marejeo aliyobeba.

Angalia hapa…
Daktari huitwa bingwa kwa sababu amehifadhi simulizi za magonjwa yaliyopita.

Mwanasheria hushinda kesi kwa sababu ameweza kuvuta kivuli cha hukumu za jana na kuzileta leo.

Na ushahidi wenyewe ni nini kama si mabaki ya jambo lililokwisha kufanyika muda uliopita?

Kwa kifupi ni kwamba hakuna hoja inayokubalika bila kupewa kaburi la zamani ili iweze kulalia.

Ndio maana ukisema jambo ambalo halijawahi kutokea, dunia hukutazama kama mwendawazimu. Lakini ukisema jambo ambalo lilishawahi kutokea, hata kama ni la kipuuzi, watu hulipa heshima fulani kwa sababu lina historia.

Ndiyo maana dunia yote inaonekana kana kwamba haiishi kuanzia sasa kwenda mbele, bali inaishi ndani ya makumbusho ya mambo yaliyopita na sasa. Kwasababu kila mfumo umejengwa juu ya ibada ya jana.

Leo hii mtu akikwambia ametoka sehemu unayoifahamu, hutaki kumuamini mpaka akupe alama za kale unazozijua zipo kwenye eneo hilo, akizitoa kwa namna sahihi, unaamini vinginevyo huwezi muamini.

Na hapo ndipo siri kubwa ilipojificha, ya kwamba binadamu haamini ukweli hadi uwe ule unaofanana na kumbukumbu zake au zozote zile za kale.

Na kwa sababu hiyo, sayansi nayo si kitu kingine isipokuwa historia iliyokataa kufa.
Historia ya kawaida huzikwa kwenye jana.

Lakini sayansi ni historia inayojirudia kwa nidhamu maalum hadi watu waiite sheria.

Mfano, mvua ilinyesha jana, ikarudia leo, ikitarajiwa kesho ndio tunasema kuna mfumo wa kisayansi unaoweza kuelezea mvua, kutokana na kujirudia rudia kwa tabia zile zile Kila mvua inapotaka kunyesha, lakini msingi wake bado ni ule ule, kumbukumbu ya yaliyopita.

Ila dunia ikikutana na jambo lisilo na mizizi kwenye jana. Kwa mfano, ugonjwa ambao hauna mfano wowote uliowahi kuwepo, usio na pattern, usiorudia tabia, usiokubali kuhifadhiwa kwenye rekodi.
Ndipo utaona namna akili zote zitakavyosimama pasinakujua wapi waanzie na wapi wamalizie.

Kwa sababu uwezo wa mwanadamu haujazoea kuumba kutoka mwanzo, ila umezoea kurejea kutoka kwenye kile ambacho tayari kilishakuwepo.

Hata AI mnayoihofia leo, haifanyi kazi kwa kuona kesho bali inavuta vipande vya jana na kuvipanga upya ila yenyewe hufanya kwa kasi kubwa kuliko mwanadamu.

Kwahiyo, future ndiyo eneo pekee ambalo akili hushindwa kutawala, ndiyo maana kesho hubaki kuwa fumbo na jana hubaki kuwa mwalimu na kipimo cha werevu.

Ukifaulu mtihani kwa A zote, huenda hukua na akili kuliko wengine bali huenda ulikuwa na uwezo mkubwa zaidi wa kubeba mizoga ya taarifa za zamani kichwani mwako na hii ikafanya ukaitwa genius kwa sababu uliweza kukariri historia kwa usahihi mkubwa kuliko waliokaa pembeni yako.

Na hapa ndipo dunia ilipojenga mfumo wake wa ulinzi.

Kwamba, ukileta hoja isiyo na kumbukumbu ya zamani, wenye dini watakuambia unakufuru ikiwa imelenga upande huo na ukileta mbele ya wasomi, watakuambia thibitisha.

Na kuthibitisha huko maana yake ni nini?
Wanataka urudi jana ukatafute ushahidi.

Ukishindwa kufanya hivyo, hoja yako hufa kabla hata haijasikilizwa.

Ndiyo maana watu wengi hurudi kwa hiari ndani ya gereza la kawaida la fikra, gereza la historia. Kwa sababu huko hakuna pingamizi na ni sehemu salama ya akili zinazohitaji kivuli cha jana ili ziweze kupumua.

Lakini swali ambalo wengi hawathubutu kujiuliza ni hili…
Je, ni nani aliyeufuma mfumo huu wa kuabudu yaliyopita?

Kwa nini dunia inaonekana kana kwamba inaruhusu kujua kile kilichokwisha kuwepo pekee, na inazuia kufikiri kuhusu kile ambacho hakijawahi kuwepo?

Kana kwamba kuna ukuta usioonekana unaozuia akili kuvuka mipaka ya historia, na dunia pamoja na mifumo yake yote hufanya juu chini kuulinda ukuta huo usionekane.

Na huenda ndio maana hakuna jipya chini ya jua, na si kwa sababu mambo mapya hayawezi kutokea, hapana, bali kwa sababu akili nyingi zimefungwa ndani ya maktaba ya jana kiasi kwamba haziwezi kutambua kile ambacho hakina kumbukumbu.

Imani yangu inaniambia sisi ni bora ya zaidi ya hivi tulivyo, ila ni vile tumefungwa kwenye eneo ambalo halitupi mwanya wa kuona zaidi ya vile ambavyo tunalazimishwa tuvione.

Ndio maana nasema, ukifutiwa kila ulilowahi kujifunza, kila uso uliowahi kuuona, kila neno ulilowahi kusikia… usingebaki na akili bali ungebaki na utupu unaohitaji kufundishwa historia upya ili uweze kuruhusiwa kuishi tena ndani ya mfumo wa dunia kwasababu akili unayohisi uko nayo huna bali imetengenezwa na kuwa shaped kinamna ile dunia inataka iwe.
Umeandikwa vitu vingi sana ngoja niwahi chini kutoa comment

Anyways..... mimi nitabakia na kende zangu mbili tu.
 
Kwa hyo hatuko mbali na tukio la kungamiza
Ila nahisi this time itakuwa tofauti kidogo
Ni ngumu kusema tupo mbali au karibu ila ni kweli kuna mabadiliko ya uhuru wa kifikra yapo, tena makubwa sana ila shida iliyopo ni ukomavu tu.

Kwasababu kimsingi mabadiliko makubwa hayategemei uhuru wa kifikra pekee ila yanategema sana na ukomavu uliopo kwenye fikra hizo zilizo huru.

Now upo huru ila huwezi kuchakata mambo wewe binafsi mwisho unaangukia kwenye usaidizi ambao usaidizi huo unakurudisha kwenye patterns zile zile za past.
 
Back
Top Bottom