Kutumia Dola ni kukosa hoja?

Kutumia Dola ni kukosa hoja?

jmushi1

Platinum Member
Joined
Nov 2, 2007
Posts
26,375
Reaction score
25,453
Wanajamvi, hivi kutumia dola dhidi ya wapinzani wako siyo dalili za kuishiwa na hoja kwenye taifa linalojinadi kufuata mfumo wa kidemokrasia?

Sidhani kama ni sahihi kumfananisha Trump na siasa zetu kwenye suala la matumizi ya dola. Hakuna usawa wa mifano hiyo hata chembe!

Mambo mengi ambayo yanafanywa na dola ya Tanzania dhidi ya upinzani yana ufanano gani na yale anayoyafanya Trump na serikali yake dhidi ya chama pinzani cha Democrats?

Hakuna kufanana hata kidogo, kwanza wagombea wote kuna wakati inafikia wanapewa ulinzi “secret services” ambao ndo wako specialized kwenye usalama wa viongozi hao bila ya kujali chama anachotokea.

Kikubwa kinachofanyika, ni kuwahakikishia ulinzi wakati wanamwaga sera zao kwa wananchi. Tena akitokea anayevuruga mkutano anabebwa juu juu kama karatasi na kutupwa nje. Sasa huku kwetu dola ndo inasimamia ukandamizwaji wa haki, uvunjifu wa sheria na ukiukwaji wa katiba ya nchi yetu halafu katibu mkuu wa ccm ambaye ni professor anaongea maneno kama vile ni mipasho?

Mbunge wa chama chochote cha upinzani marekani anaweza kupigwa risasi mahali popote pale iwe ndani ama nje ya marekani(achilia mbali kwenye maeneo ya bunge kama Lissu), na dola isitumike kufanya uchunguzi? Unaifananisha marekani na Tanzania kwenye utu wa kuthaminiana wenyewe kwa wenyewe? Au mkuu alizungumzia matumizi ya dola kivipi? Anajitia upofu? Ama ni ulevi wa madaraka?

Viongozi ump wanaweza kuthubutu kuzivamia studio za CNN pamoja na kuziita “fake news” kila uchwao? Yaliyotokea cloudsvideo si zipo? Hivyo ndivyo namna ya kutumia dola kubaki madarakani ama ni udikteta?

Mifano iko mingi sana! Lakini kwa kifupi kauli hiyo ya katibu mkuu wa ccm inadhihirisha ukweli kwamba serikali inayotumia dola ili iweze kubaki madarakani, basi imeishiwa na hoja za kuwashawishi watanzania kuweza kuwachagua.

Dola kazi yake kwenye demokrasia, ni kusimamia uwanja sawa wa kila upande uweze kuziwakilisha hoja zake kwa wananchi bila bughudha yoyote ile! Na siyo kutumika na chama kimoja. Hilo likitokea, tunaweza kusema ni udikteta!

Pia nashauri kuwepo na midahalo ili wananchi tuweze kujiridhisha na siyo kupachikiwa viongozi tu bila kusikia uwezo wao wa kusimamia hoja.

Rais ni nembo ya kwanza na mwakilishi wa kwanza kwa Taifa hata nje ya nchi.

Ukimpata rais ambaye hajui mdahalo, kuna uwezekano akawa katili. Ndo maana hatuoni mijadala ya bunge live ili wananchi tuwe proud kuhusu demokrasia yetu na kuona mchango wetu kwa Taifa kupitia wawakilishi wetu nk.

Tungekuwa na midahalo ya wazi na mfumo mzuri, aliyoyahoji Ben Saanane yangeshapatiwa majibu kabla ya mtu kuingia ikulu na Ben kutekwa na kupoteza maisha yake.
 
Maneno aliyoyatamka katibu mkuu wa ccm ambaye na yeye kiukweli ulinzi wake ni mkubwa kupitiliza kwa maoni yangu, nadhani baada ya waziri mkuu(nimeshawahi kushuhudia msafara wake), yanaonyesha ulevi mbwa wa madaraka!
 
Ni kweli Mwl. Nyerere alikuwa katili kweli kwa sababu hakupenda midahalo na wapinzani wake ndio maana aliamua kufuta vyama vingi na kwenye nafasi ya Urais akawa anaweka kivuli kishindane naye!

Rais wa Urusi, Vladimir Putin anapenda sana midahalo lakini kama ukitaka kumjua zaidi, ingia kwenye anga zake!

Rais Kagame mpaka anapewa uwanja wa midahalo kwenye vyuo kama George Washington University lakini jaribu kuingia kwenye anga zake utapata jibu sahihi!

Hoja ya msingi ni kuwa, kupenda midahalo sio kigezo cha kiongozi kutokuwa katili na kutopenda midahalo sio kigezo cha kuonyesha kiongozi atakuwa katili!

Ni ukweli kuwa siasa za Tanzania simefungamanishwa sio na na dola pekee bali hata taasisi zingine muhimu za kijamii ndio maana unasikia kuwa Tanzania ni nchi mojawapo Afrika ambayo ina amani kwa muda mrefu.

Mwl. Nyerere aliposema, ''Rais wa Tanzania anaweza kutoka chama chochote cha siasa lakini Rais bora atatoka CCM'' alikuwa na maana pana sana kwa watu wanaojua siasa za Tanzania!
 
CCM kwenye ulingo sawa bila msaada wa vyombo vya ulinzi hawana chao. Ndo mana kila uchwao wanaishia kujipendekeza na kujiunganusha kimkakati vyombo vya dola ili viwahakikishie kubaki madarakani.
 
Midahalo inapima uwezo wa kujieleza kwa kiongozi anayekusudia kuomba nafasi kubwa za uongozi,na lengo ni kujua na kutambua uwezo wa huyo kiongozi tarajiwa kwenye mambo mbalimbali ya kidunia ili ikitokea amepewa nafasi ya kuongea kwenye mikutano ya kimataifa asibabaike au kuogopa mikutano ya kimataifa.

Ni aibu kwa nchi kuwa na kiongozi parochial kwenye mambo ya kidunia maana Rais ni nembo ya Taifa akiwa empty minded ni sawa na kuwa nchi na wananchi wake ni empty minded pia
 
1583507466927.png
 
Statements za katibu wa CCM zinaonyesha ukakasi kwa demokrasia yetu!!

Ati mwenye dola atumie dola yake kujiwekea uzio wa kisiasa dhidi ya wenzake..hii hoja haikubaliki kabisa.
 
Mimi ninachojua ,Bashiru alikuwa anaiongelea dola(serikali) na sio vyombo vya dola (polisi n.k). Mafanikio ya serikali ndio uhakika Wa chama chenye madaraka kuendelea kutawala kwa kuwa serikali ndio dola inayochaguliwa na watu.
 
MsemajiUkweli,
Out of point mifano yako yote unatolea wakati tukiwa chini ya chama kimoja. Wewe unatoa mfano wa Russia ambao nao irrelevant hapa given Putin ni dictator. Sasa kutokana na kauli yako hii, labda katibu mkuu wa ccm angesema tuko chini ya dictatorship kuliko kufananisha siasa zetu na zile za Trump.

Kuhusu midahalo, hilo nalisimamia bila kuyumba, mifano yako ni irrelevant again, labda useme ccm ni chama cha kifashisti maana ndivyo ambavyo hutumia dola kubakia madarakani badala ya hoja.

Sisi wananchi kama wadau ni lazima tusikie uwezo wako wa kukabiliana kwa hoja. Ukiwa huwezi hoja, unabakia kwenye vihoja. Mfano kutumia dola nk.
 
Maneno aliyoyatamka katibu mkuu wa ccm ambaye na yeye kiukweli ulinzi wake ni mkubwa kupitiliza kwa maoni yangu, nadhani baada ya waziri mkuu(nimeshawahi kushuhudia msafara wake), yanaonyesha ulevi mbwa wa madaraka!
2316889_FB_IMG_1582491848963.jpg
 
Hivi hawa watu hawanaga washauri? Ina maana CCM wote hawana akili? Hata kama kweli intention yao ni kutumia dola je yawezekana vipi mtu timamu akalizungumza hilo katika media? SMH
Ndo ulevi mbwa huo wa madaraka mkuu. Hata uongozi wa taifa kama la Tanzania ni suala la kujitolea. Lakini sisi kwetu ni suala la kunufaika kwa kila namna na vyote vinavyoletwa na madaraka, hence ulevi mbwa.
 
Mkuu niliwahi kushuhudia msafara wa huyu jamaa! Kwanza nilidhani ni kiongozi mkubwa wa serikali, kuja kuona ni yeye katibu mkuu wa ccm nilishangazwa sana. Nadhani yeye anafahamu kile kitu kinaitwa “chama kushika hatamu”, anapewa ulinzi kwa namna ambayo inaonyesha kuwa mfumo tulio nao siyo mzuri. Yeye mwenyewe nadhani anashangaa kuona anaishi kama yuko peponi na wakati kazi ya uprofesa pengine ilikuwa ngumu zaidi.

ccm haifai hata kwa kurumangia.
 
Statements za katibu wa CCM zinaonyesha ukakasi kwa demokrasia yetu!!

Ati mwenye dola atumie dola yake kujiwekea uzio wa kisiasa dhidi ya wenzake..hii hoja haikubaliki kabisa.
Hii ni uthibitisho kwamba tunahitaji overhauling.
 
Back
Top Bottom