Kutoka Bungeni: Wabunge wapinga ongezeko la kodi ya uchakavu wa magari

Kutoka Bungeni jioni ya leo Wabunge wa CCM, Mh. Serukamba na Mh. Olesendeka wamepigania vikali hoja ya kupunguza muda wa awali kwa kodi ya uchakavu wa magari toka nje ya nchi toka miaka 10 iliyokuwa awali na kuwa miaka 8.

Wakitoa mapendekezo yao Mh. Olesendeka alisisitiza kwa kubakisha ongezeko hili Serikali itakuwa haijawatendea haki wananchi wake, kwa maana hiyo alikua anamuunga mkono moja kwa moja Mh. Serukamba hata ikampasa Mh. PM kusimama na kuondoa utata uliopo hata naye kuikubali hoja hiyo.

Nawasilisha!

mkuu wabunge wamekubalianaje katika hilo? wamerejesha miaka kumi au??
 
Kutoka Bungeni jioni ya leo Wabunge wa CCM, Mh. Serukamba na Mh. Olesendeka wamepigania vikali hoja ya kupunguza muda wa awali kwa kodi ya uchakavu wa magari toka nje ya nchi toka miaka 10 iliyokuwa awali na kuwa miaka 8.

Wakitoa mapendekezo yao Mh. Olesendeka alisisitiza kwa kubakisha ongezeko hili Serikali itakuwa haijawatendea haki wananchi wake, kwa maana hiyo alikua anamuunga mkono moja kwa moja Mh. Serukamba hata ikampasa Mh. PM kusimama na kuondoa utata uliopo hata naye kuikubali hoja hiyo.

Nawasilisha!

Tatizo ni fomula inayotumika kukokotoa kodi na wala si umri wa gari. Ki-IST used unakinunua Japani kwa dola 2000 kama shs 3mil na ushee lakini kodi yake milioni 6. Wanachotetea wabunge hata hawakijui. TRA wanatumia depreciation method kukokotoa kodi ya gari. Wanaangalia likiwa jipya liliuzwa/lingeuzwa shs ngapi halafu wanatoa kiasi cha asilimia fulani kila mwaka. Thamani itakayobaki ndio msingi wa kodi unayolipa. Hivyo ukinunua la hivi karibuni depreciation cost inakuwa ndogo na thamani baki (residual value) inakuwa kubwa kodi yake ni kimbembe vilevile. Walichoweka TRA NI KUHAKIKISHA UNALIPA KODI KUPITA MAELEZO. Kwa hivyo vyovyote utakavyo kimbilia tofauti itakuwa ndongo sana. Usipolipa penalti ya gari ya zamani unalipa thamani kubwa ya gari ambayo ni karibia mpya. Ambao hamkutoroka vipindi vya hesabu darasani mtanielewa. Olesendeka na mwenzake walitakiwa kujua hilo ili wafahamu wamtetee mwananchi kwa kipengere gani.

Nawasilisha!
 
Hata wangefanya miaka 12 na zaidi ingekuwa poa..ila lamsingi wangeangalia milleage..ime-run milleage ngapi? Gari haichakai kwa kukaa muda mrefu bali kwa kutembea muda umbali mwingi. Unakuta gari inakidhi kigezo cha miaka 10 au 8 lakini imekwenda km zaidi ya lakimoja..wakati ambapo unaikuta gari ina miaka zaidi ya kumi(12 au zaidi) lakini imekwenda km 30elfu au hata 60elfu.. je hapo ipi ina ubora? ya miaka 8 au 12?
Lamsingi wange-limit kwenye milleage na sio umri wa gari.
Hata hivyo nawapongeza waliotetea miaka 10 ibaki.
 
Tatizo ni fomula inayotumika kukokotoa kodi na wala si umri wa gari. Ki-IST used unakinunua Japani kwa dola 2000 kama shs 3mil na ushee lakini kodi yake milioni 6. Wanachotetea wabunge hata hawakijui. TRA wanatumia depreciation method kukokotoa kodi ya gari. Wanaangalia likiwa jipya liliuzwa/lingeuzwa shs ngapi halafu wanatoa kiasi cha asilimia fulani kila mwaka. Thamani itakayobaki ndio msingi wa kodi unayolipa. Hivyo ukinunua la hivi karibuni depreciation cost inakuwa ndogo na thamani baki (residual value) inakuwa kubwa kodi yake ni kimbembe vilevile. Walichoweka TRA NI KUHAKIKISHA UNALIPA KODI KUPITA MAELEZO. Kwa hivyo vyovyote utakavyo kimbilia tofauti itakuwa ndongo sana. Usipolipa penalti ya gari ya zamani unalipa thamani kubwa ya gari ambayo ni karibia mpya. Ambao hamkutoroka vipindi vya hesabu darasani mtanielewa. Olesendeka na mwenzake walitakiwa kujua hilo ili wafahamu wamtetee mwananchi kwa kipengere gani.

Nawasilisha!

Mkuu kununua gari ya 2003 na kununua gari ya 2005 kuna tofauti ya about 3 millioni kama unanunua Vits. Nimetumia calculator ya tra.

Miaka ikibaki 10 ni nafuu kwa mwananchi wa kawaida.
 
Mkuu kununua gari ya 2003 na kununua gari ya 2005 kuna tofauti ya about 3 millioni kama unanunua Vits. Nimetumia calculator ya tra.

Miaka ikibaki 10 ni nafuu kwa mwananchi wa kawaida.
Muelewe salisalum,
Ukinunua Gari ya karibuni utalambwa bei kubwa kwani assumption ya TRA ni kua haija-depreciate sana so bado mpyampya.

Na ukinunua ya zamani nayo utachapwa kodi za kutosha tu,
Kwani umeleta Gari chakavu.

So unakabwa kotekote bila kujali kua kuitumia napo unakabwa bei za mafuta!!!
 
Hapa mimi sina usemi maana nilitoroka darasa la hesabu shuleni mara mwalimu wangu wa hesabu alipofariki. teh teh teh te
 
nafikiri hoja zetu tulizozibandika humu huwa wanazisoma..........

Social media zimeibuka kuwa na authority ya aina yake kiasi kwamba politicians wana-cite humu ku-argue mambo yao. Si mara moja serikali imewahi kukana tuhuma bila kusema chanzo, lakini chanzo hicho kinatoka humu JF. Pia nimewasikia wanasiasa wengine wakilaumu JF, na wengine wakijigamba kama ni wanachama humu akiwemo Mh Job Ndugai akijaribu kuthibitisha umakini wake kwa jamii kuwa huwa anaangalia JF. Usisahau kuchangia JF inedelee kuimarika.

Kinachonichekesha na kunifurahisha zaidi, si mara moja nimewahi kuna magazeti yakichukua articles na hoja za humu JF na kuziandikia kama makala au news, na ku-claim authority bila ku-aknowledge JF.
 
Jamani hivi ndio kweli vijihouse allowance wanaanza kuzifyeka PAYE, mbona hawa watu hawana huruma?
 
Ubora wagari haupimwi kwa mileage.Gari yaweza kuwa imeclock 200,000 mileage lakini engine ikawa bado iko safi kuliko hata gari iliyotembea mileage 70,000. Kingine ni kwamba TRA watapoteza sana kutoza kodi kwa kutumia kigezo cha mileage,kwani mileage zote manual au digital zote zinachakachulika bila tatizo.
 
Idadi ya miaka tutakayodumu kuwa soko la wengine kwa bidhaa zao mpya na mitumba, ni sawa sawa na miaka ambayo uchumi wetu utadumu kuwa duni. Fikiria ni miaka mingapi hiyo.
Nimeikumbuka sana hoja ya huyu mkuu;
[h=2]Thursday, January 5, 2012[/h][h=3]Tanzania Yangu.....Na mikakati thabiti ya "kuua kilicho chake"[/h]

Mwaka 2008, Tanzania ilitajwa kama nchi ya 78 katika nchi bora za kufanya biashara ulimwenguni. Kwa mujibu wa matandao wa Forbes unaojihusisha na habari za Mapato na Biashara, takwimu zilizotolewa mwaka huo zilionesha kuwa Tanzania ilikuwa imepanda nafasi 26 toka ile iliyokuwa nayo mwaka 2007 (ya 104) na kwa mwaka huo (2008) ilikuwa nafasi moja juu ya China iliyoshuka nafasi mbili toka mwaka uliopita.
Ripoti ya mwaka 2008 ilionesha kuwa ukuaji wa viwanda, madini hasa Dhahabu, mabadiliko ya mfumo wa kibenki na uwekezaji, michango ya wahisani pamoja na sera madhubuti za uchumi ni kati ya vigezo vilivyoiweka Tanzania katika nafasi hiyo. Lakini pia miundombinu chakavu imekuwa kikwazo katika uwekezaji na ukuaji wa uchumi kwa ujumla. Mwaka uliomalizika umeshuhudia Tanzania ikishika nafasi ya 108, ikiwa ni nafasi 6 chini ya ilivyokuwa mwaka 2010. Na kwa mwaka jana, wenzetu ambao tulikuwa juu yao kwa nafasi moja mwaka 2008, (namaanisha China) sasa wanashikilia nafasi ya 82.
Botswana ndiyo nchi bora zaidi kwa biashara barani Afrika (kwa mujibu wa mtandao wa Forbes) na inashikilia nafasi ya 55 duniani. Kwa upande wa Majirani zetu, Kenya ni ya 103, Uganda ni ya 105.
Bado yaonekana kuwa nchii yangu (inayosemekana kuwa katika asilimia 10 zenye uhitaji zaidi, ama wenyewe wanaita maskini) inategemea zaidi misaada ya nje ilhali inatumia asilimia nne (4%) ya eneo lote la nchi.
Miundombinu chakavu katika kukwamua uchumi inaonekana kuwa kikwazo kingine kinachoikwamisha nchi ambayo tayari inashikilia rekodi ya kupokea fungu kubwa zaidi kutoka Millennium Challenge Compact (MCC) lenye thamani ya dola milioni 698.
LAKINI NI NANI MCHAWI WA MAENDELEO YETU?
NAWAZA.......
Hivi kama serikali (ambayo naamini ina magari mengi sana) ingeweka ulazima wa magari yote kununua matairi kwenye viwanda vya ndani kama General Tyre, VINGEKUFA? Ama watasema matairi yaliyokuwa yakitengenezwa Arusha hayakukidhi ubora wa barabara na hali ya Tanzania?
general%2Btyre%2Bpic.jpg
Hivi kama serikali ingeweka mkakati madhubuti na kuamua kutumia magari yanayotengenezwa na kiwanda cha jeshi cha NYUMBU katika idara na ofisi zake zooote nchini, tusingepunguza uagizaji wa magari? Ama watasema MAGARI YA NYUMBU HAYAKO KATIKA KIWANGO CHA TANZANIA ukilinganisha na magari yatokayo Marekani / Japan / China?
Hivi wabunge wetu na sare zote zinazofadhiliwa / kudhaminiwa na serikali zingekuwa ni kutoka viwanda vya ndani kama URAFIKI vingekufa?​
bush%2Bin%2Btanzania.jpg
Hivi serikali ingeamua kutumia (japo asilimia kubwa ya) saruji ya nyumbani, nondo za nyumbani na mafundi wa nyumbani kujenga "vikwangua anga" vyote vya nyumbani, ajira ingekuwa katika kiwangi ilichopo?
Dar+Es+Salaam+Mwl+Nyerere+Pension+Tower.JPG
Ni wakati ambao naamini "wenye uerevu" wa mambo watajitokeza na kunyambua mambo haya yanayoelezwa na hawa "wataalam" wa uchumi wa dunia, ama wajitokeze kuwapinga na kujenga hoja za ki-uchumi wa Tanzania na / ama Afrika na kisha kutueleza ni kwanini tupo tulipo, na ni vipi tunaweza kusonga mbele zaidi (kama kuna uwezekano).
Lakini nawaza namna tunavyoweza kusonga mbele kiuchumi ikiwa HATUTHAMINI KILICHO CHETU?​
Ni vipi tutaendeleza VAZI LA TAIFA iwapo mBunge asiyevaa SUTI haonekani kuvaa kiheshima ndani ya Bunge la Tanzania? Hata suti tunasikia kuwa wazivaazo wanazitoa nje ya nchi (kama WIKILEAKS ilikuwa sahihi). Tutawezaje kuendeleza uzalishaji wa magari ya nyumbu ikiwa yale waliyotengeneza miaka hiyo hayajapata mteja na wala kupata nafasi ya kuonyeshwa na kunadiwa (zaidi ya siku ya maigizo ya uhuru)?
Ni vipi kiwanda kama General Tyre kingeshindana na viwanda vya nje iwapo maelfu ama malaki ya magari ya serikali yanatumia matairi yaliyoagizwa nje?
 
Hii ni kweli kabisa, ingawa wengi hawajui hili

Tatizo ni fomula inayotumika kukokotoa kodi na wala si umri wa gari. Ki-IST used unakinunua Japani kwa dola 2000 kama shs 3mil na ushee lakini kodi yake milioni 6. Wanachotetea wabunge hata hawakijui. TRA wanatumia depreciation method kukokotoa kodi ya gari. Wanaangalia likiwa jipya liliuzwa/lingeuzwa shs ngapi halafu wanatoa kiasi cha asilimia fulani kila mwaka. Thamani itakayobaki ndio msingi wa kodi unayolipa. Hivyo ukinunua la hivi karibuni depreciation cost inakuwa ndogo na thamani baki (residual value) inakuwa kubwa kodi yake ni kimbembe vilevile. Walichoweka TRA NI KUHAKIKISHA UNALIPA KODI KUPITA MAELEZO. Kwa hivyo vyovyote utakavyo kimbilia tofauti itakuwa ndongo sana. Usipolipa penalti ya gari ya zamani unalipa thamani kubwa ya gari ambayo ni karibia mpya. Ambao hamkutoroka vipindi vya hesabu darasani mtanielewa. Olesendeka na mwenzake walitakiwa kujua hilo ili wafahamu wamtetee mwananchi kwa kipengere gani.

Nawasilisha!
 
Ashakum si matusi, Nimegundua hii serikali ni ya viazi vitupu
Hapo dar kuna yale magari ya budege na wenzie ya kuzoa taka. yani yale yalitakiwa yawe hayatembei barabarani tena. Sasa badala ya kupambana na watu kama hawa, eti wanatulazimishia kununua magari mapya. nchi hii ya vituko.
eti wanapunguza ajali, wakati mawaziri wao na wabunge wanapata ajali kila siku na ma V8 yao mapya.

Leo Dr. Mgimwa kajishushia hadhi pamoja na swala la vocha za simu. naona magamba yameanza kumuharibu sasa.
 
Waziri wa fedha amewaacha hoi wabunge na Wtz waliokuwa wakimsikliza wakati akitoa
Sababu za kupunguza muda magari yaliyotumika kuingizwa nchini,mwanzo serikali
ilipendekeza iwe miaka minane na kuendelea,waziri alipobanwa kuhusu kwanini
iwe miaka minane akajibu tunawasaidia wananji magari makukuu yanatumia mafuta mengi
Pia spare zake ni gharama!!!! Wabunge wakaangua miguno serukamba akasema suala
la gharama ni la mtu binafisi akaungwa mkono na wabunge wengine.

Mtoto wa mkulima naye akaja na longolongo eti wamefanya vile ili kuwalinda wtz na ajari Wabunge wakazomea ikabidi aufyate wakaondoa mswada uchwara na sasa imebaki
Miaka kumi Kama kawa.

Haya magamba yamejisahau kabisa km wabongo wanahali ngumu na hawawezi kumudu
Kununua magari mapya?

Imetokea leo ktk Bunge la Tanzania.

imebaki kivipi wakati watu washalipa uchakavu ? Au tutarudishiwa hela zetu?
 
Mmh! Walikuwa wapi siku zote? Kwanza binafsi naona wangeangalia hali halisi ya gari sio umri kwani kuna magari ya miaka 20 lakini hali yake huwa ni nzuri sana. Binafsi naona hii kodi ni ya kuzuia watu wenye kipato cha chini tusiwe na magari. Sioni mantiki yake. Wanatukamua tu na wafanya biashara wakubwa ambao ndio wanatakiwa kulipa kodi wakiwa hawalipi inavyostahili. Mungu wetu atatusaidia tutalipa tu kwani gari ni muhimu sana kwa maisha ya mwanadamu na uwezo wa kununua jipya wengi wetu hatuna.
Kutoka Bungeni jioni ya leo Wabunge wa CCM, Mh. Serukamba na Mh. Olesendeka wamepigania vikali hoja ya kupunguza muda wa awali kwa kodi ya uchakavu wa magari toka nje ya nchi toka miaka 10 iliyokuwa awali na kuwa miaka 8.

Wakitoa mapendekezo yao Mh. Olesendeka alisisitiza kwa kubakisha ongezeko hili Serikali itakuwa haijawatendea haki wananchi wake, kwa maana hiyo alikua anamuunga mkono moja kwa moja Mh. Serukamba hata ikampasa Mh. PM kusimama na kuondoa utata uliopo hata naye kuikubali hoja hiyo.

Nawasilisha!
 
Muelewe salisalum,
Ukinunua Gari ya karibuni utalambwa bei kubwa kwani assumption ya TRA ni kua haija-depreciate sana so bado mpyampya.

Na ukinunua ya zamani nayo utachapwa kodi za kutosha tu,
Kwani umeleta Gari chakavu.

So unakabwa kotekote bila kujali kua kuitumia napo unakabwa bei za mafuta!!!

Argument ya kukabwa kote kote ambayo salisalum ameitoa nimeielewa. Ila si kweli kuwa hamna nafuu. Miaka ikibaki 10, una uwezo wa kuleta vits ya 2003 ambapo hutachargiwa dumping charge! You will save 3 mil tofauti na kama utaleta gari ya 2005 kwa sheria ya miaka nane ili kukwepa dumping charge. Nafuu ipo.

Kuhusu kutumia depreciation method. I think TRA wanakwepa kutumia bei uliyonunuliwa coz there have been cases za udanganyifu wa bei halisi ya gari.
 
Back
Top Bottom