Kutangazwa Arusha kuwa jiji

Kutangazwa Arusha kuwa jiji

Mndokanyi

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2012
Posts
629
Reaction score
119
Mh Raisi J. Kikwete anategemewa kutangaza rasmi Arusha kuwa jiji. Jambo lililonishtua ni kwamba tamko hilo litafanywa rasmi kwa kukata utepe pale mnara wa mwenge kulikofanyika uzinduzi wa Azimio la Arusha.Sasa ndugu JF baada ya uzinduzi huo,mnara huu utakuwa na kumbukumbu ya kitu gani?!,Azimio la Arusha au kumbukumbu ya Arusha kutangazwa kuwa jiji?!
 
Utaendelea kuitwa mnara wa mwenge.
 
Arusha inakuwa jiji kwa mara ya pili? Mkapa ndiye aliyepandisha hadhi Arusha na kuwa jiji (more than 7 yrs ago).
 
Sijui ni criteria gani zinatumika kuuita mji jiji huko Tanzania. Manake hata kamji ninachoishi tuko wachache lakini kanaitwa Garden city, Kule Long island. Miji na vijiji vyote bongo ni majiji
 
Wakati wa mkapa wanasema kuna vigezo ilikuwa haijakidhi.
 
Anyway,kwanini kwa Arusha imekuwa so special? Mbeya,Tanga,Mwanza ilikuwa hivi? Politics?
 
Anyway,kwanini kwa Arusha imekuwa so special? Mbeya,Tanga,Mwanza ilikuwa hivi? Politics?
Hilo swali nimemuuliza journalist mmoja nguli mpaka sasa hajanipa jibu lolote. Mi nakumbuka ilipopandishwa Mwanza sikusikia kama kulikuwa na hafla yoyote, na hata baadae Tanga na Mbeya sasa sijui Arusha ina nini la maana mpaka ufanyike uzinduzi?
 
ARUSHA don't deserve to be city, migomba mpaka mjini
 
Sijui ni criteria gani zinatumika kuuita mji jiji huko Tanzania. Manake hata kamji ninachoishi tuko wachache lakini kanaitwa Garden city, Kule Long island. Miji na vijiji vyote bongo ni majiji

mkuu SHERRIF ARPAIO sijui wametumia vigezo gani kwa Arusha
bado arusha miundombinu iko hovyo barabara za kuingia mji huu ni mbili tuu ukiifunga barabara ya Moshi Arusha na barabara ya Sokoine huu mji hutoki
Mita mia mbili kutoka barabara ya Moshi Arusha katika ule ukanda wa halmashauri ya Jiji ni nyumba za udongo
kati kati ya jiji lenyewe bado kuna nyumba za zamani zilizoezekwa kwa madebe na zinaendelea kuwepo katikati ya hapo atakapofanyia uzinduzi wenyewe
 
Last edited by a moderator:
Si ilishawahi kua jiji hii? Mbona walivoivua ujiji hawakutangaza?

Tetesi: Fungu lililotengwa kwa ajili ya afla ya kutangaza Arusha kua jiji ni Tsh........ Nakutania
 
Arusha ilishakuwa jiji hata kabla ya mbeya.

Mkeshaji Arusha ilipewa hadhi ya jiji lini na Mbeya ikapata lini? Usidanganye watu bwana. Arusha haikuitangulia Mbeya kupata hadhi ya jiji. Mbeya ilitanguliwa na Mwanza.
 
Last edited by a moderator:
Sijui ni criteria gani zinatumika kuuita mji jiji huko Tanzania. Manake hata kamji ninachoishi tuko wachache lakini kanaitwa Garden city, Kule Long island. Miji na vijiji vyote bongo ni majiji

Kaka SHERRIF ARPAIO kwani huko wanatumia criteria gani? Unataka mji ufanane na London ndipo uitwe jiji? Kila nchi ina vigezo vyake.
 
Last edited by a moderator:
Hizi Kamikaze na attempts za kuchefua watu wa arusha wakidhani wataweza washawishi wawapende zitazaa kitu kibaya sana.Kikwete hajui watu wa arusha by nature ni watu wa vita.Wamasai, waarusha, wameru, na wa mikoa ya jirani si watu salama sana.

CCM imeshapewa kisogo basi wakubalike yaishe waweke nguvu kwingine,kila move wafanyayo inaonekana wazi kujawa dhuluma na hivyo kuishia kuwa chukizo.
 
ARUSHA don't deserve to be city, migomba mpaka mjini
Migomba haitakaa iiishe ,itatoweka ila itarudi wenye pesa wakianza merger viwanja kibao uswahili na kupata eneo kubwa lenye garden watarudisha migomba tena. Minazi nayo ilikuwa haitakiwi mjini ila baadaye ilirudi ktk sehemu maridadi.Kahawa siku hizi zinaoteshwa ktk garden za nyumba nyingi sana Arusha.
 
Kwa Arusha kutangazwa kuwa jiji na ona ni haraka tu! Mji wa Arusha una changamoto nyingi ambazo wange zishughulikia kabla ya kutangazwa kuwa jiji.
Changa moto kama!
1 barabara hili ni tatizo kubwa hata zilizopo ni nyembamba sana, kwakweli huu mji una hitaji barabara za kutosha ni haibu kusema Arusha ni jiji labda kwa mtu ambaye ajawai kuishi au kupita Arusha anaweza asishangae!
Japo miundo mbinu si kigezo pekee lakini kwa hili kuna udhaifu sana!
Kwakweli ni bora nguvu nyingi zingeelekezwa kwenye kuuboresha mji huo, sijajua hiyo haraka ni ya nini?

Ukweli lazima usemwe Arusha bado huku ni kujifariji, lakini pamoja na vitega uchumi vingi vilivyoko hasa utalii nashangaa mji wa Arusha kuwa na miundo mbinu hafifu!
 
that's problem for receiving AID from USA and Uropean coutry
 
Back
Top Bottom