Ms Judith
JF-Expert Member
- Dec 24, 2010
- 2,563
- 936
Wapendwa,
Kama nilivyowaahidi ndio namaliza mazungumzo na rafiki yangu kutoka Eritrea kuhusu "babu" wa huko kwao na shughuli zake. Kimsingi hatofautiani sana na babu wetu huyu wa TZ. Mambo ya "babu" wa Eritrea kwa mujibu wa huyu rafiki ni kuwa:
1.
Alijulikana kwa jina la Armalakha na alikuwa muinjilisti na mhubiri hodari katika nchi za Ethiopia na Eritrea hata kabla Eritrea haijajitenga kutoka Ethiopia.
2.
Aliwahi kuingia katika migogoro kadhaa na makanisa ya kikatoliki na orthodoxy (amabyo ndiyo makubwa na yanaheshimika sana nchini humo) ya Eritrea na Ethiopia kwa sababu makanisa hayo yalipinga utaratibu wa tiba yake kwa kuhusianisha uganga wake na mafundisho ya biblia.
3.
Mwaka 1996 alianza kudai kuwa mungu amemuotesha mchanganyiko wa madawa asilia ambayo huyachanganya na kuyachemsha na kasha maji yake kuwanywesha wagonjwa wake na makapi ya maji yake kuwafungia wagonjwa wake kwenye mkono wa kuume na kuuning'iniza mkono huo kama POP. Hiyo ni baada ya kusema mungu kamtokea katika ndoto na kumfunulia kuwa maradhi yote yanayowasumbua watu yako tumboni na hutokea mwilini kupitia mkono wa kuume.
4.
Watu wa kwanza kunywa dawa zake walikuwa wakiongea kwa lugha za ajabu na yeye akawa anadai ndizo lugha mpya zilizotabiriwa na nabii Yoeli!
5.
Alidai anatibu magonjwa makuu kama kansa, ukimwi, kisukari na kutoa mapepo ya aina zote kwa dawa zake hizo!
6.
Alidai mungu kamwagiza atibu kwa Nakfa 8/- tu (nakfa ni sarafu ya Eritrea na nakfa moja ni sawa na senti kama 30 za USD)
7.
Alipata umaarufu mkubwa sana na wa ghafla sambamba na kutajirika sana katika kipindi kifupi sana na kulikuwa na shuhuda nyingi sana kuwa watu wengi walipona maradhi yao kwa muda mfupi sana na kimiujiza japo hospitali za Ethiopia na Eritrea hazikuwahi kuthibitisha uponyaji wake hata mara moja!
8.
kutokana na uhasama ulioibika baada ya Eritrea kujitenga na Ethiopia (baada ya eritrea kujitangazia uhuru), alituhumiwa kuwa alikuwa wakala wa intelijensia ya Ethiopia (yaani alikuwa anaipatia serikali ya Ethiopia taarifa za siri za kijasusi) na kufuatia kuandamwa sana na vyombo vya dola aliuawa kwa kupigwa risasi June mwaka 2006.
Hayo ndiyo niliyopata kwa rafiki yangu huyu.
Wapendwa tusiache kuzijaribu kila roho ili tujiridhishe kuwa zimetokana na Mungu. Neno la mungu ni taa na mwangaza wa maisha yetu, liyumulikie kila tuendapo. Amina.
Nawatakia tafakari njema
Glory to God
Kama nilivyowaahidi ndio namaliza mazungumzo na rafiki yangu kutoka Eritrea kuhusu "babu" wa huko kwao na shughuli zake. Kimsingi hatofautiani sana na babu wetu huyu wa TZ. Mambo ya "babu" wa Eritrea kwa mujibu wa huyu rafiki ni kuwa:
1.
Alijulikana kwa jina la Armalakha na alikuwa muinjilisti na mhubiri hodari katika nchi za Ethiopia na Eritrea hata kabla Eritrea haijajitenga kutoka Ethiopia.
2.
Aliwahi kuingia katika migogoro kadhaa na makanisa ya kikatoliki na orthodoxy (amabyo ndiyo makubwa na yanaheshimika sana nchini humo) ya Eritrea na Ethiopia kwa sababu makanisa hayo yalipinga utaratibu wa tiba yake kwa kuhusianisha uganga wake na mafundisho ya biblia.
3.
Mwaka 1996 alianza kudai kuwa mungu amemuotesha mchanganyiko wa madawa asilia ambayo huyachanganya na kuyachemsha na kasha maji yake kuwanywesha wagonjwa wake na makapi ya maji yake kuwafungia wagonjwa wake kwenye mkono wa kuume na kuuning'iniza mkono huo kama POP. Hiyo ni baada ya kusema mungu kamtokea katika ndoto na kumfunulia kuwa maradhi yote yanayowasumbua watu yako tumboni na hutokea mwilini kupitia mkono wa kuume.
4.
Watu wa kwanza kunywa dawa zake walikuwa wakiongea kwa lugha za ajabu na yeye akawa anadai ndizo lugha mpya zilizotabiriwa na nabii Yoeli!
5.
Alidai anatibu magonjwa makuu kama kansa, ukimwi, kisukari na kutoa mapepo ya aina zote kwa dawa zake hizo!
6.
Alidai mungu kamwagiza atibu kwa Nakfa 8/- tu (nakfa ni sarafu ya Eritrea na nakfa moja ni sawa na senti kama 30 za USD)
7.
Alipata umaarufu mkubwa sana na wa ghafla sambamba na kutajirika sana katika kipindi kifupi sana na kulikuwa na shuhuda nyingi sana kuwa watu wengi walipona maradhi yao kwa muda mfupi sana na kimiujiza japo hospitali za Ethiopia na Eritrea hazikuwahi kuthibitisha uponyaji wake hata mara moja!
8.
kutokana na uhasama ulioibika baada ya Eritrea kujitenga na Ethiopia (baada ya eritrea kujitangazia uhuru), alituhumiwa kuwa alikuwa wakala wa intelijensia ya Ethiopia (yaani alikuwa anaipatia serikali ya Ethiopia taarifa za siri za kijasusi) na kufuatia kuandamwa sana na vyombo vya dola aliuawa kwa kupigwa risasi June mwaka 2006.
Hayo ndiyo niliyopata kwa rafiki yangu huyu.
Wapendwa tusiache kuzijaribu kila roho ili tujiridhishe kuwa zimetokana na Mungu. Neno la mungu ni taa na mwangaza wa maisha yetu, liyumulikie kila tuendapo. Amina.
Nawatakia tafakari njema
Glory to God