Kusubiri marekebisho ya Taarifa za NIDA kwa zaidi ya miezi mitatu ni uzembe wa Mamlaka

BigTall

JF-Expert Member
Mar 9, 2022
422
1,049
Watanzania tunaofanya marekebisho ya Taarifa za Kitambulisho cha NIDA kuna mlolongo mrefu na gharama kubwa lakini bado pia taarifa hazirekebishwi kwa zaidi ya miezi mitatu.

Wengi tunafahamu kuwa kuwa na kitambisho cha Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) ni jambo muhimu na linarahisisha shughuli nyingi kwenye kazi mbalimbali pamoja na masuala ya masomo na hata binafsi.

Kwanza kabisa ukitaka kurekebisha taarifa binafsi za kitambulisho au zilizopo NIDA unatakiwa kujipanga kisaikolojia kutokana na kesho utakazozipata za usumbufu pamoja na kujiandaa kiuchumi kwa kuwa utalazimika ‘kutoboka’ mfukoni ili kupata kitu.

Mfano nijitolee mfano mimi binafsi, nilipohitaji kurekebisha taarifa nilitumia kiasi cha Tsh. 20,000 kwa ajili ya Hati ya Kiapo (Deep Poll), Tsh. 33,000 kwa ajili ya kulipia kwenye katika Ofisi ya Msajili, nikatangaza katika Gazeti la Serikali 20,000, nilipokamilisha hapo nikalipia Tsh. 20,000 kwenye ofisi zao za NIDA.

Jumla ilikuwa Shilingi 93,000 lakini hapo bado kuna gharama za nenda rudi, njoo kesho, nenga kule, rudi huku.

Baada ya kukamilisha hayo ndipo unaanza mchakato wa kusubiri muda wa marekebisho hayo.

Nina zaidi ya miezi mitatu sijafanyiwa marekebisho.

Mfano kuna Wanafunzi wa Mwaka wa Kwanza wanao ripoti vyuoni na ili usajiliwe unatakiwa uwe na NIDA au taarifa zao ziendane pamoja na zile zilizopo kwenye nyaraka zake nyingine.

Asilimia kubwa ya Wanafunzi wanaohitaji kufanyiwa mabadiliko kwenye NIDA ili yaendane sawa na taarifa zilizopo kwenye nyaraka zao wanazowasilisha chuo, wamekuwa wakiitia katika wakati mgumu.

Wito wangu kwa Serikali ya Tanzania na Mamlaka yenyewe ya NIDA, katika Dunia ya sasa ambayo kuna maendeleo makubwa ya Teknolojia, kweli unalazimika kusubiri miezi mitatu kufanyiwa marekebisho ya taarifa za NIDA hata kama ukiwa na kila kitu? Hii si sawa, tuko nyuma sana.
 
Watanzania tunaofanya marekebisho ya Taarifa za Kitambulisho cha NIDA kuna mlolongo mrefu na gharama kubwa lakini bado pia taarifa hazirekebishwi kwa zaidi ya miezi mitatu.

Wengi tunafahamu kuwa kuwa na kitambisho cha Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) ni jambo muhimu na linarahisisha shughuli nyingi kwenye kazi mbalimbali pamoja na masuala ya masomo na hata binafsi.

Kwanza kabisa ukitaka kurekebisha taarifa binafsi za kitambulisho au zilizopo NIDA unatakiwa kujipanga kisaikolojia kutokana na kesho utakazozipata za usumbufu pamoja na kujiandaa kiuchumi kwa kuwa utalazimika ‘kutoboka’ mfukoni ili kupata kitu.

Mfano nijitolee mfano mimi binafsi, nilipohitaji kurekebisha taarifa nilitumia kiasi cha Tsh. 20,000 kwa ajili ya Hati ya Kiapo (Deep Poll), Tsh. 33,000 kwa ajili ya kulipia kwenye katika Ofisi ya Msajili, nikatangaza katika Gazeti la Serikali 20,000, nilipokamilisha hapo nikalipia Tsh. 20,000 kwenye ofisi zao za NIDA.

Jumla ilikuwa Shilingi 93,000 lakini hapo bado kuna gharama za nenda rudi, njoo kesho, nenga kule, rudi huku.

Baada ya kukamilisha hayo ndipo unaanza mchakato wa kusubiri muda wa marekebisho hayo.

Nina zaidi ya miezi mitatu sijafanyiwa marekebisho.

Mfano kuna Wanafunzi wa Mwaka wa Kwanza wanao ripoti vyuoni na ili usajiliwe unatakiwa uwe na NIDA au taarifa zao ziendane pamoja na zile zilizopo kwenye nyaraka zake nyingine.

Asilimia kubwa ya Wanafunzi wanaohitaji kufanyiwa mabadiliko kwenye NIDA ili yaendane sawa na taarifa zilizopo kwenye nyaraka zao wanazowasilisha chuo, wamekuwa wakiitia katika wakati mgumu.

Wito wangu kwa Serikali ya Tanzania na Mamlaka yenyewe ya NIDA, katika Dunia ya sasa ambayo kuna maendeleo makubwa ya Teknolojia, kweli unalazimika kusubiri miezi mitatu kufanyiwa marekebisho ya taarifa za NIDA hata kama ukiwa na kila kitu? Hii si sawa, tuko nyuma sana.
Mdau naamini pia kama tungekuwa mbele kama usemavyo ungekuwa makini kuweka taarifa zako vizuri. Ni aibu pia kwa msomi kuwa na nyaraka zinazokinzana kila mara na kuwatupia lawama wengine kwa nakosa yako mwenyewe. Sidhani kama ni sahihi kubadilisha kirahisi hivyo taarifa kwenye kanzidata inayochukuliwa kuwa ya Taifa. Huu umakini na usasa pia tuuweke kwenye umakini wa taarifa zetu. Tunaelekea kwenye integration ya Africa Mashariki ambapo hata maswala ya ajira tutakuwa tunagombania. Tuwe makini tunaosema kuwa ni wasomi kuweka taarifa sahihi.
 
Mdau naamini pia kama tungekuwa mbele kama usemavyo ungekuwa makini kuweka taarifa zako vizuri. Ni aibu pia kwa msomi kuwa na nyaraka zinazokinzana kila mara na kuwatupia lawama wengine kwa nakosa yako mwenyewe. Sidhani kama ni sahihi kubadilisha kirahisi hivyo taarifa kwenye kanzidata inayochukuliwa kuwa ya Taifa. Huu umakini na usasa pia tuuweke kwenye umakini wa taarifa zetu. Tunaelekea kwenye integration ya Africa Mashariki ambapo hata maswala ya ajira tutakuwa tunagombania. Tuwe makini tunaosema kuwa ni wasomi kuweka taarifa sahihi.
Mimi naweza sema zaidi ya asilimia 70 ya watu ambao taarifa zao zinamakosa Kwenye kitambulisho cha NIDA chanzo ni hao hao maafisa wa NIDA. Utakuta mwananchi kajaza fomu yake vizur kabisaa na Kwa umakini lakin wao haraka haraka zao na kukosa umakini wanakosea kujaza taarifa kwenye mfumo. Na hii imewakuta wengi hasa kipindi NIDA inaandikishwa mtaani, Kwa kuwa mwananchi hupati mda wa kuhakiki taarifa zako kma zimejazwa sahihi unakuta kugundua hilo baada ya Namba au kitambulisho kutoka. Nina jamaa zangu kadha walikutwa na kadhia hii moja kazaliwa mwaka 1995 NIDA imetoka 1955 , mwingine anaitwa EMMANUEL NIDA imetoka EMMANU
 
Mdau naamini pia kama tungekuwa mbele kama usemavyo ungekuwa makini kuweka taarifa zako vizuri. Ni aibu pia kwa msomi kuwa na nyaraka zinazokinzana kila mara na kuwatupia lawama wengine kwa nakosa yako mwenyewe. Sidhani kama ni sahihi kubadilisha kirahisi hivyo taarifa kwenye kanzidata inayochukuliwa kuwa ya Taifa. Huu umakini na usasa pia tuuweke kwenye umakini wa taarifa zetu. Tunaelekea kwenye integration ya Africa Mashariki ambapo hata maswala ya ajira tutakuwa tunagombania. Tuwe makini tunaosema kuwa ni wasomi kuweka taarifa sahihi.
Hata kama alikosea haiwapi uhalali wa kusubirisha mtu miezi mitatu.
 
Back
Top Bottom