Ubabaishaji wa ofisi ya NIDA

Mr RoundAbout

Member
Oct 6, 2023
70
85
Ndugu wana bodi, nawasalimu na kuwatakia heri ya Sikukuu ya Noeli na Mwaka mpya 2024.

Ndugu za imenibidi niandike tu suala hili kwani ni zaidi ya mara 4 nimekutana na usumbufu sana katika ofisi za NIDA, Mimi mwenyewe nimehangaika sana kupata kitambulisho changu, yaani kifupi ofisi hii hawajitambui Nini wanachofanya. Iko hivi, Nina mdogo wangu ambaye anaishi South Africa, alizaliwa uingereza kipindi Mzee anafanya PhD kwani alikuwa mwalimu chuo kikuu Cha Dar es salaam, ana passport ya Tanzania hizi mpya aliichukulia ubalozi wa Afrika Kusini,, yaani ni raia wa Tanzania kabisa.

Sasa kaja kula Sikukuu nyumbani, akasema naye apate kitambulisho Cha Taifa maana ni haki yake. Tulienda ofisi mojawapo ya NIDA na fomu zetu zulizokamili. Tulipofika tukapokelewa kama kawaida na kupewa namba, tukaingia ofisi ya uhamiaji mdogo wangu akasainiwa fomu yake katika kipengele Cha Uraia na Afisa wa Uhamiaji baada ya kujiridhisha kuwa ni raia Kwa documents zote zipo. Baada ya hapo tukaambiwa tuende Kwa Maafisa wapiga picha wa NIDA, ndipo tukakutana na mambo ambayo yanashangaza, wakakataa kumpiga picha eti siyo.

Wakati watu wa Uhamiaji ndiyo wanaohusika na suala la uraia walikuwa wamesha mhudumia Kwa kuangalia nyaraka zake. Kimsingi inakera sana ofisi kama hii ya umma inakuwa na watumishi ambayo hawajitambui na hawajui nn Cha kufanya. Nilipokuwa pale nimeona wateja wengi tu wakijibiwa hovyo mpaka wengine kuamua kuondoka.

Nikahisi labda pengine ofisi hii imeshindwa kujisimamia ndiyo maana Mhe Rais, ameiunganisha na RITA, pengine Kwa ukubwa wa RITA itasaidia katika kuboresha huduma ya utoaji wa namba inayofanywa na NIDA.

Ndiyo hayo wanabodi, yaliyotukuta Watanzania wenzenu.
 
Pole mkuu, ilitakiwa isiwe shida kabisa kwa raia kupata kitambulisho, ndio maana hii NIDA,RITA ni kufutilia mbali, wizara ya ndani ndio wawe wahusika wa kutoa na kuratibu hizi IDs, police ilitakiwa iwe na wizara yake, uraia &immigrations hizi idara ndizo zitakua chini ya wizara ya mambo ya ndani, na mtoto anapozaliwa kokote hapa nchini ,mzazi asiruhusiwe kurudi nyumbani hadi awe na birth certificate ya mtoto wake, yaani unabridged certificate. Hii itaua longolongo zote ,kuomba passport unahitaji kuwa na ID book basi
 
Ndugu wana bodi, nawasalimu na kuwatakia heri ya Sikukuu ya Noeli na Mwaka mpya 2024.
Ndugu za imenibidi niandike tu suala hili kwani ni zaidi ya mara 4 nimekutana na usumbufu sana katika ofisi za NIDA, Mimi mwenyewe nimehangaika sana kupata kitambulisho changu, yaani kifupi ofisi hii hawajitambui Nini wanachofanya. Iko hivi, Nina mdogo wangu ambaye anaishi South Africa, alizaliwa uingereza kipindi Mzee anafanya PhD kwani alikuwa mwalimu chuo kikuu Cha Dar es salaam, ana passport ya Tanzania hizi mpya aliichukulia ubalozi wa Afrika Kusini,, yaani ni raia wa Tanzania kabisa. Sasa kaja kula Sikukuu nyumbani, akasema naye apate kitambulisho Cha Taifa maana ni haki yake. Tulienda ofisi mojawapo ya NIDA na fomu zetu zulizokamili. Tulipofika tukapokelewa kama kawaida na kupewa namba, tukaingia ofisi ya uhamiaji mdogo wangu akasainiwa fomu yake katika kipengele Cha Uraia na Afisa wa Uhamiaji baada ya kujiridhisha kuwa ni raia Kwa documents zote zipo. Baada ya hapo tukaambiwa tuende Kwa Maafisa wapiga picha wa NIDA, ndipo tukakutana na mambo ambayo yanashangaza, wakakataa kumpiga picha eti siyo. Wakati watu wa Uhamiaji ndiyo wanaohusika na suala la uraia walikuwa wamesha mhudumia Kwa kuangalia nyaraka zake. Kimsingi inakera sana ofisi kama hii ya umma inakuwa na watumishi ambayo hawajitambui na hawajui nn Cha kufanya. Nilipokuwa pale nimeona wateja wengi tu wakijibiwa hovyo mpaka wengine kuamua kuondoka.
Nikahisi labda pengine ofisi hii imeshindwa kujisimamia ndiyo maana Mhe Rais, ameiunganisha na RITA, pengine Kwa ukubwa wa RITA itasaidia katika kuboresha huduma ya utoaji wa namba inayofanywa na NIDA.
Ndiyo hayo wanabodi, yaliyotukuta Watanzania wenzenu.
Kwa kweli NIDA ni shida, hata hivi vitambulisho lukuki vimetoka sio Kwa sababu wamependa Bali shinikizo na hili Jambo la kuunganishwa na Rita.
Yaani mpaka unajiuliza hivi hawa watu ni Shule gani walizisoma.angalau wewe hapo umekutana na WA uhamiaji ambaye inaonekana anajielewa. Wengi bado hasa hivyo vitoto vya NIDA na maafisa usalama. Na ukitilia maanani siku hizi hakuna kitu chako kitaenda bila NIDA, na maofisa wenyewe ndio hawa.
 
Kwa kweli NIDA ni shida, hata hivi vitambulisho lukuki vimetoka sio Kwa sababu wamependa Bali shinikizo na hili Jambo la kuunganishwa na Rita.
Yaani mpaka unajiuliza hivi hawa watu ni Shule gani walizisoma.angalau wewe hapo umekutana na WA uhamiaji ambaye inaonekana anajielewa. Wengi bado hasa hivyo vitoto vya NIDA na maafisa usalama. Na ukitilia maanani siku hizi hakuna kitu chako kitaenda bila NIDA, na maofisa wenyewe ndio hawa.
Na inavyoonekana hata maboss wao ni wale wale tu, hawajielewi kbs kwani binti ametujibu hovyo sana yule mpaka tukamshangaa. Kweli hii ni Taasisi ya mchongo tu
 
Back
Top Bottom