kioju
JF-Expert Member
- Apr 28, 2014
- 804
- 271
Padre alihubiri huwezi kutubu dhambi zako kama wewe mwenyewe hujasamehe waliokutenda/kuumiza kwa kutokutubu dhambi zako unakuwa umejenga ukuta na mungu wako kwa kuwa na dhambi unakuwa umemuasi mungu wako kwa kuishi kwako katika dhambi kuna-invite majanga mengi katika maisha yako personally,majanga hayo yaweza kuwa magonjwa,umasikini,failures,mikosi Lakini hata katika kuishi kwako ukiwa si mwenye dhambi yaani kwa kuishi ukiwa hujavunja amri zote kumi za mungu bado dhambi zilizotendwa na generation nne za nyuma yako bado zinaweza kutesa,muulize baba yako au wazee kama kuna madhabahu walizo abudu huko nyuma Haya yalikuwa maudhui ya somo la leo.
Niko kwenye mid forties,nimelelewa kwenye ukatoliki sawia,natimiza wajibu wangu kama mkatoliki,natenda dhambi ndio, nawajibika kutubu na huwa natubu.Kwa mara ya kwanza leo katika maisha yangu ya dini nimekutana na mahubiri hayo hapo,padre alikuwa anaquote vitabu tofauti kusupport his arguments.Nimemkubali na nimekubali kitu ambacho for the last few years nilikuwa sijalikubali kusamehe
My ex alinitenda kutendwa ambako namshukuru mungu alinipa ujasiri wa kutokulipiza kisasi,for a year nilienda kukabidhi silaha polisi kwa sababu shetani alikuwa ananiteka,ningeweza kufanya kitu kibaya.Nilimwacha mke wangu,nili-move on,sikuwahi kumsamehe ila nilikwa najaribu kusahau.Kila nilipofikiria kile alichonifanyia tumbo lilikuwa linatetemeka.Baada ya mahubiri ya leo nilipata muda wa kutubu,nimemsamehe my ex,kutoka moyoni.
Our divorce was one of the messiest divorce ambazo huwezi kufikiria,yaani hata arrangements za kuwaona watoto,kulipia school fees ni through our solicitors.Nimempigia simu leo my lawyer ili aweke appointment na lawyer wa my ex ili waweze kutukutanisha nimwambie kwamba nimemsamehe kama ambavyo nimetubu leo kanisani.
Wana MMU naomba tushare hii topic ya KUSAMEHE.Je umashatendwa/umizwa kiasi cha kushindwa kusamehe?Sio kuumizwa kwenye ndoa/mapenzi tu,hapana hata maisha ya kawaida,ulidhulumiwa na mtu/watu,kuna mtu/watu walikatisha ndoto zako za maisha.Yaani yale mambo mabaya uliyofanyiwa na mtu/watu kiasi ukikumbuka au ukimuona mtu/watu waliokutenda unasikia moyo kukuenda mbio au tumbo kukuuma.Je uliwasamehe/utawasamehe?.Bila kusameheana tutakuwa tunajenga kweli taifa lenye maadili na lenye kumpendeza mungu kuazia kwenye familia au mtu mmoja mmoja au familia na familia?
cc @Kaunga The Boss Karucee snowhite Sikonge Kongosho
Mkuu uzi ni mzur lak umeuchafua kwa kumshushia hadhi Mungu kwa kuandka mungu
Ukishaandka mungu ktk tafsir ya biblia unabdlisha maana kabisa huyo anakua ni yule jamaa ibilisi lakin ukishasema Mungu hapo ndo unampa hadhi yake hasa huyo aliyetuumba
Tujitahdin kukumbka hlo
Pia kama umekwazka kwa hlo bhasi rejea uzi wako hapo juu
Ubarikiwe sana