Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 58,636
- 220,349
Wengi wetu hatuelewi matatizo katika jamii inayotuzunguka. Si lazima uwe tajiri ili uweze kuisaidia jamii. Kidogo ulichonacho kinaweza kubadilisha maisha ya mtu.
Nilikuwa ninaangalia African Channel siku moja, nilimuona baba mmoja Mnigeria ni tajiri anayeishi Marekani. Huyu tajiri biashara yake ilianzia kwenye mafuta Nigeria lakini sasa hivi ana vitega uchumi vingi vikubwa Marekani.
Anasomesha wanafunzi 20 kila mwaka kutoka Nigeria wasio na scholarship. Anawalipia tuition fees na accommodation mpaka wamalize shule.
Unaweza kununua kilo 10 za sukari kuwasaidia wasiojiweza. Kama hutaki ujulikane unaweza kumpa Imam, Paroko au mchungaji.
Kuna kisa nilikutana nacho Arusha. Chalii mmoja wa Mererani alimjengea mjane nyumba self contained umeme na maji na akamwambia mama usinipe asante ila niingize kwenye sala zako za kila siku kwa Mungu. Ni baada ya kusikia mama anafukuzwa kwenye nyumba kwa kukosa kodi.
Unapotoa usitegemee asante, fanya hayo kwa kumshukuru Mungu kwa kile alichokupa. Christmas inakuja, kuna familia haziwazi hata sikukuu itakuwaje matatizo ni mengi. Kuziwezesha familia hizi kula mlo wa sikukuu si jambo dogo. Fikiria.
Nilikuwa ninaangalia African Channel siku moja, nilimuona baba mmoja Mnigeria ni tajiri anayeishi Marekani. Huyu tajiri biashara yake ilianzia kwenye mafuta Nigeria lakini sasa hivi ana vitega uchumi vingi vikubwa Marekani.
Anasomesha wanafunzi 20 kila mwaka kutoka Nigeria wasio na scholarship. Anawalipia tuition fees na accommodation mpaka wamalize shule.
Unaweza kununua kilo 10 za sukari kuwasaidia wasiojiweza. Kama hutaki ujulikane unaweza kumpa Imam, Paroko au mchungaji.
Kuna kisa nilikutana nacho Arusha. Chalii mmoja wa Mererani alimjengea mjane nyumba self contained umeme na maji na akamwambia mama usinipe asante ila niingize kwenye sala zako za kila siku kwa Mungu. Ni baada ya kusikia mama anafukuzwa kwenye nyumba kwa kukosa kodi.
Unapotoa usitegemee asante, fanya hayo kwa kumshukuru Mungu kwa kile alichokupa. Christmas inakuja, kuna familia haziwazi hata sikukuu itakuwaje matatizo ni mengi. Kuziwezesha familia hizi kula mlo wa sikukuu si jambo dogo. Fikiria.




