Kura: Zilipendwa vs Seduce me

Kura: Zilipendwa vs Seduce me

PIGA KURA: ZILIPENDWA V/S SEDUCE ME


  • Total voters
    118
Kwa kawaida huwa sipendi kuingia kwenye mtego wa u timu.Siku zote mtu hafundishwi muziki mzuri ni upi kwa sababu kila mtu ana hisia zake juu ya wimbo fulani.Siyo sawa kushindanisha nyimbo zenye ladha na msisimko tofauti.Hapo mtakuwa mnawashindanisha watu!Nimezisikiliza nyimbo zote.Kila moja ina ladha yake.Achana na mambo ya kuangalia kama kuna ujumbe au la...zote zina mdundo mzuri.Mimi ni muumini wa watu wanaoshirikiana kuimba kwa pamoja mtindo ambao unaitwa 'call and responding' kwani unaongeza ladha kwenye wimbo kwa kusikia sauti tofauti tofauti.Tuwe wakweli Diamond ni msanii mwenye kipaji cha kweli....anaweza kuimba na kumiliki jukwaa kwa kucheza.Lakini pia ana uwezo wa kupiga gita kitu ambacho wabongo fleva wengi hawawezi.Wanaosema ana roho mbaya siyo kweli.Kwanza ameunda kundi la WCB,ina maana yuko tayari kufanya kazi na watu wengine na huo ndio mwanzo wa kuwa na live band kitu ambacho ni muhimu kwa muziki wa dunia ya leo.Tusiwahukumu kwa makandokando yao,tuwahukumu kwa muziki wao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hizi nyimbo zote ni nzuri. Kila moja ina uzuri wake, ya kiba kuwa ya kimataifa inaweza ikawa sawa kwasababu hata diamond anazo nyingi za kimataifa. I love both songs!
 
Hawa vijana wanawachezea sana walimwengu wapenda mziki wa kibongo na kwa hili nawapongeza sana vijana wetu.

Juzi wote wametoa single, mmoja akilenga soko lanje na wengine la ndani. Kwa maana ingine wanapokezana au kupeana gape wanaposet goals zao.

Ukisikiliza nyimbo zao kwa makini utagundua hawaimbi stail inayofanana. Kila mmoja ana mziki wake wa aina yake na unaopendwa ndani na nje. Hata wale vijana wa camps zao wanaopinga huyu na huyu wote wanazikubali na kuzipenda sana nyimbo za hawa vijana

Wote wana asili ya Kigoma wamekuwa wamoja tangu mapema Kiba na queen wanaimba na kisha akaja Diamond. Nionavyo mimi hii ni staili yao hii wanaitumia kuhadaa kuwa wanashindana,biff nk lakini mpango wao mkubwa ni kuendelea kuhodhi tasnia hii ya Mziki wa Bongo.
 
9172ae79d5050a6e6968da29a0bd319b.jpg
 
WCB wametoa nyimbo kibao tuu wakati Alikiba akiwa kimya akifanya tour zake, huu ni mwendelezo tuu wa WCB kutoa single zake ilizonazo tusichukulie sana katika fikra za kushindana shindana japo ushindani upo...
na WCB wanaonyesha kuwa bado wanahifadhi kubwa ya nyimbo ndani ya kapu lao la kuweza kutoa muda wowote fans wao wakitaka watoe...

wanaaachia wimbo ovyo Kama season ya Game of thrones
 
Back
Top Bottom