Kura za maoni CCM Arumeru kurudiwa

MADAI YALIOMUUA KOLIMBA CCM JUU YA 'UKWELI ALMASI' WA CHAMA KUKOSA DIRA WALA HAYANA TOFAUTI KUBWA NA YALE YA MWANASAYANSI GALILEO GALILEI KWA VIONGOZI WA DINI DUNIANI

Hata Mwanasayansi Galileo Galilei alipata kukatwa kichwa kwa maagizo ya viongozi wa dini baada ya kuelezea kwamba sura ya dunia ni dwara na kwamba inakwenda inachukua umbo mchongoko mfano wa yai.

Ni majuzi tu baada ya miaka zaidi ya 400 kupita ambapo Marehemu Galileo ametokea kuombwa radhi na viongozi wa dini baada ya kubainika wazi kwamba madai yake ki-uhakika ndio hasa ukweli wa mambo ulivyo.

Kwa nini mtu aje aone ajabu hii CCM Kombokombo ya 'Kamanda' Kikwete kuja kujikamua ujasiri wa kumuomba radhi Horrace Kolimba badala ya kumhonga mwanaye na viji-cheo cha U-DC, wakati Kolimba mwenyewe wala hajamaliza hata robo karne tangu auweke wazi huo 'udhaifu almasi' wa Chama Cha Mapinduzi miaka kadhaa iliopita????

Mkuu napata mashaka kama unaelewa historia ya Galileo vizuri. Galileo hakuuwawa ila alikufa baada ya kupata homa kali na ugonjwa wa moyo. Walichofanya kanisa ni kumtoboa macho kwa kuwa walidhani kuwa jua linaizunguka dunia badala ya dunia kulizunguja jua kama alivyoamini Galileo. Weka kumbukumbu vizuri mkuu. Hata hivo ni kweli ccm wamepoteza dira na hawaujui ukweli.
 
Ina maana hakuna fursa kwa wanachama wenye sifa kujitokeza kugombea na majina yao kujdailiwa na vikao vya juu vya chama?.....
Huwezi kusema wananchi hawana fursa ikiwa wanao wawakilishi wao ktk mkutano mkuu. Hata Obama kapita bila ridhaa ya wananchi (ukitaka kutazama hivyo) Na huwezi kusema inaruhusiwa tu ikiwa rais anagombea awamu ya pili. Ila kama atajitokeza mtu kugombea dhidi yake RUKSA na kama angepatikana mtu kugombea dhidi ya Dr. Slaa ilikuwa ruksa..Halafu kama wajumbe wa baraza kuu wote wamekuja na jina moja kwa chama kidogo kama Chadema kwa nini inawapa shida kuelewa..
 
mimi sielewi hapa kama hakufikisha 51% kwanini wamerudia wawili tu?kwani hawa wengine hawana haki!swali langu je kwani hao wabunge wangine wa ccm walishinda kwa zaidi ya 51% duh CCM mmechanganyikiwa
 
Mkuu Mwigulu,

Asante kwa kuja hapa na kutoa ufafanuzi. Lakini wewe kama msimamizi wa uchaguzi ilitakiwa hili kulijua toka mapema na kuliweka wazi. kwamba uchaguzi haukuisha kwani hakuna aliyepata zaidi ya asilimia 50 kama katiba inavyosema.

Hapa ungelikuwa muungwana tu na kusema ulifanya makosa na bahati nzuri kamati kuu imegundua na kuyarekebisha makosa hayo. Kuanza kutumia njia nyingine yoyote kuelezea hili kosa binafsi nitasema ni ubabaishaji. Kila mtu anakosea, lakini ni vizuri kukiri kosa na kusonga mbele.

Hayo makosa madogo madogo inatakiwa vijana tena na elimu zenu nzuri tu msiyafanye. CCM imakuwa ikidhalilishwa sana kwa watendaji kutokufuata taratibu. Ifike mahali mjirekebishe na nyie kama vijana muwe wa kwanza kujifunza na kufanya mabadiliko.

Unajua ningelikuwa mimi ningesema tu, "Sorry guys, I screwed up!" lakini bahati wazee kule CC wamerekebisha.

Hivi unappoteza muda wako kusikiliza ngonjera za hawa wahuni, kwani umesahau ni hawa hawa waliotuambia Uspika sasa ni zamu ya Mwanamke? tatizo mtoto wa Sumari hatakiwi hakuna jambo lingine, na kama CHADEMA wakijipanga ipasavyo hili jimbo ni lao pasi na shaka yoyote.
 
Kwa ufafanuzi sahihi ni kwamba kilichofanyika leo na CC ya NEC ya CCM ni kupanua demokrasia ya maamuzi kwa kurejesha majina mawili ya mshindi wa kwanza katika kura za maoni na mshindi wa pili ili sasa Mkutano Mkuu wa jimbo upigie kura majina hayo mawili na baadae kutoa fursa kwa vikao vya juu yaani Kamati za siasa za wilaya na mkoa na baadae CC kujadili na kumpitisha mmoja wapo. Sioni mkanganyiko tena. kwani katika hesabu za kawaida kati ya hao wawili, lazima mmoja apate zaidi ya asilimia hamsini ya kura zote au wagongane au wafungane kwa kupata asilimia hamsini kila mmoja. huo ndiyo uzuri wa demokrasia. lazima ifuate ili kumpata mtu anayekubalika zaidi kuwakilisha chama chetu.
Wale ambao hawana hoja, na badala yake wanataka kupinga kila kitu, sasa niwakati wa kuaibika.

lini mmeanza kufuata demokrasia zaidi ya kuangalia makundi.we sema kuna kundi limeona halina maslai juu ya mteule wa kwanza kuelekea 2015. na huyo sidhani kama atapita kwa awam ya pili
 
Kwa ufafanuzi sahihi ni kwamba kilichofanyika leo na CC ya NEC ya CCM ni kupanua demokrasia ya maamuzi kwa kurejesha majina mawili ya mshindi wa kwanza katika kura za maoni na mshindi wa pili ili sasa Mkutano Mkuu wa jimbo upigie kura majina hayo mawili na baadae kutoa fursa kwa vikao vya juu yaani Kamati za siasa za wilaya na mkoa na baadae CC kujadili na kumpitisha mmoja wapo. Sioni mkanganyiko tena. kwani katika hesabu za kawaida kati ya hao wawili, lazima mmoja apate zaidi ya asilimia hamsini ya kura zote au wagongane au wafungane kwa kupata asilimia hamsini kila mmoja. huo ndiyo uzuri wa demokrasia. lazima ifuate ili kumpata mtu anayekubalika zaidi kuwakilisha chama chetu.
Wale ambao hawana hoja, na badala yake wanataka kupinga kila kitu, sasa niwakati wa kuaibika.

Mkuu nashukuru kwa kuja jamvini. Kuna lile swala la kuwa Sioi alitembeza rushwa na pia kamati ya siasa ya mkoa ikiongozwa na RC na Mama Chitanda ya kwamba hawamtaki Sioi apitishwe. Unalizungumziaje hilo, angalau tupate kauli yenye ukweli.
 
Ninacho kiona mimi hapa ni kwamba tayari malalamiko kuhusu kupata kura nyingi kwa Sioi kulianza kama kuleta mkanganyiko ndani ya chama, ukizingatia uchaguzi mkuu mambo kama haya ndio yaliwa cost sehemu nyingi ndipo sasa CC ikaamua kupanua wigo kwa kufanya ilivyoamua
Na kama tunakumbukumbu nzuri hii si mara ya kwanza kubadili taratibu za uchaguzi pindi hali ya hewa ikichafuka
Sioni tatizo katika hili ilimradi tu iwe ni kwa nia nzuri na maslahi kwa chama chao, kama chama chochote kinacyoweza kufanya kunusuru maslahi ya chama
 
Kwa ufafanuzi sahihi ni kwamba kilichofanyika leo na CC ya NEC ya CCM ni kupanua demokrasia ya maamuzi kwa kurejesha majina mawili ya mshindi wa kwanza katika kura za maoni na mshindi wa pili ili sasa Mkutano Mkuu wa jimbo upigie kura majina hayo mawili na baadae kutoa fursa kwa vikao vya juu yaani Kamati za siasa za wilaya na mkoa na baadae CC kujadili na kumpitisha mmoja wapo. Sioni mkanganyiko tena. kwani katika hesabu za kawaida kati ya hao wawili, lazima mmoja apate zaidi ya asilimia hamsini ya kura zote au wagongane au wafungane kwa kupata asilimia hamsini kila mmoja. huo ndiyo uzuri wa demokrasia. lazima ifuate ili kumpata mtu anayekubalika zaidi kuwakilisha chama chetu.
Wale ambao hawana hoja, na badala yake wanataka kupinga kila kitu, sasa niwakati wa kuaibika.
Mwigulu asante kwa ufafanuzi wako, umenza hoja vizuri lakini ukamalizia vibaya sentensi ya mwisho.

Watu wanahoji huo utaratibu wa pass the post 50% haukujulikana kwa ngazi zote za chini tangu jimbo, wilaya, mkoa hadi CC ndiyo pekee inaoujua? au unataka kutuambia kuwa kuna taratibu tofauti kwenye chaguzi za CCM kulingana na ngazi husika, kwamba ngazi fulani watatumia simple majority nyingine 50%.

Tofauti ya taratibu hizo ndizo zinapelekea watu kuwa na wasiwasi labda kuna mchezo fulani wa kutaka kum favour mmoja wa wagombea.
 
[FONT=Tahoma, Calibri, Verdana, Geneva, sans-serif]Maamuzi ya kamati kuu ya Leo yawavuruga Millya, Ester Maleko, Ally Bananga na Sioi. Hayo yalidhihirika Leo kwenye Kikao chao walichokifanya kwenye moja ya kata za jimbo la arumeru Mashariki. Kikao chao wameseama watapambana kufa na kupona hadi Sioi ashinde tena. Wanasikitika sana kwa ccm kuwafanyia Uhuni kwa kitendo cha kutokujali gharama wlizotumia kwenye mchakato uliopita.[/FONT][FONT=Tahoma, Calibri, Verdana, Geneva, sans-serif]
[/FONT]
[FONT=Tahoma, Calibri, Verdana, Geneva, sans-serif]Pia wamekemea kitendo cha kusema Lowasa Katoa hela kwa ajili ya Sioi wakati hela hizo zimetolewa na Fred Lowasa pamoja na rafiki zake.[/FONT]
[FONT=Tahoma, Calibri, Verdana, Geneva, sans-serif]
[/FONT]
[FONT=Tahoma, Calibri, Verdana, Geneva, sans-serif]Pia Millya amekemea kitendo cha watu kuzungumzia tu namna alivyofeli kidato cha pili pale moringe sekondari na kuwashangaa kwa Kuwa Mbona aliporudia na kufaulu hawakusema tena? Waache kuzungumzia upande mmoja tu. na lazima jamii ielewe Kuwa ile ilikuwa ni bahati mbaya ndo maana aliweza kuendelea na masomo ya juu tena nje ya nchi.[/FONT]
 
Hivi unappoteza muda wako kusikiliza ngonjera za hawa wahuni, kwani umesahau ni hawa hawa waliotuambia Uspika sasa ni zamu ya Mwanamke? tatizo mtoto wa Sumari hatakiwi hakuna jambo lingine, na kama CHADEMA wakijipanga ipasavyo hili jimbo ni lao pasi na shaka yoyote.
Mkuu Matola siasa za nchi hii huzijui? rejea uchaguzi wa uenyekiti CDM, "hapa watu wananusuru chama kwa maslahi ya chama" tofauti hapa ni namna tu ya kukinusuru
 
we are watching with great interest,it is amazing but believable because of the of party envolved,'ni mchezo wa kawaida kwao, kwa hiyo no comment, we should expect anything from them!
 
Only wise people can understand this game.Someone must be excluded intensionally and no body in the CC is ready to bear the burden to speak out WHO so auromatically u'll see WHO is their (CC) choice.Only voters can prove them wrong by voting for the right candidate as MP among all party contestants.They can not choose for US anymore but G and peoples voice is the God's one.All the best wana Arumeru!
 
Hakuna mahala kanuni za CCM inasema mgombea ubunge lazima apate asilimia 50 isipokuwa nafasi ya rais tu..
Kanuni za wagombea wa CCM ngazi ya Uwakilishi/Ubunge inasema hivi:-
(iv)​
Ngazi ya Baraza la Wawakilishi/Bunge:
(1)​
Wagombea watapigiwa kura za maoni na Mkutano Mkuu wa CCM wa kilaJimbo la Uchaguzi linalohusika,(2) Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu ya CCM ya Wilaya itawajadili wagombea.(3) Kwa upande wa Tanzania Bara, Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu ya CCMya Mkoa itawajadili wagombea na kuwatolea mapendekezo yake kwa KamatiKuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa. Kwa upande wa Tanzania Zanzibar, Kamatiya Siasa ya Mkoa itawajadili wagombea na kuwatolea mapendekezo yake kwaKamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa ambayo nayo itatoamapendekezo yake kwa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa.(4) Kamati Kuu itawajadili wagombea wote na kutoa mapendekezo yake kwaHalmashauri Kuu ya CCM ya Taifa kwa ajili ya uteuzi wa mwisho.Katika kufanya kazi hiyo kwa upande wa Wabunge/Wawakilishi wanaomalizamuda wao, Kamati Kuu itazingatia pia tathmini itakayokuwa imefanyika ya
utendaji kazi wao katika kipindi kinachomalizika..
 
Huwezi kusema wananchi hawana fursa ikiwa wanao wawakilishi wao ktk mkutano mkuu. Hata Obama kapita bila ridhaa ya wananchi (ukitaka kutazama hivyo) Na huwezi kusema inaruhusiwa tu ikiwa rais anagombea awamu ya pili. Ila kama atajitokeza mtu kugombea dhidi yake RUKSA na kama angepatikana mtu kugombea dhidi ya Dr. Slaa ilikuwa ruksa..Halafu kama wajumbe wa baraza kuu wote wamekuja na jina moja kwa chama kidogo kama Chadema kwa nini inawapa shida kuelewa..
Bob....

Suala si kupata shida kuelewa.....Suala hapa ni Demokrasia....Kutoa wigo kwa wana CHADEMA wenye sifa kujitokeza kugombea Urais kama ilivyo kwa Ubunge na majina yao kujadiliwa na kupitishwa na vikao vya juu vya chama..Kumbuka hata huyo Obama naye wakati wa awamu ya kwanza alipitia katika mchujo ambao uliwashirikishwa wanachama wengine wa chama cha Demokrasia(mfano Hilary Rodham Clinton).....Na mgombea wa CHADEMA kwa mwaka 2010 hakugombea kwa mara ya pili,aligombea kwa mara ya kwanza....Endapo atagombea mwaka 2015 hiyo ndiyo itkuwa mara ya pili....

Btw.....Inawezekana kweli wajumbe wote wa Baraza kuu wakaja na jina moja?.......

Cha msingi(kwa lengo la kuboresha) ni kutoa fursa kwa wanachama wote wanaojiona wana sifa za kugombea Urais wawe huru kujitokeza na kugombea kuteuliwa na chama katika uchaguzi wa Rais......N mtazamo tu...

Bala.
 
Kwa ufafanuzi sahihi ni kwamba kilichofanyika leo na CC ya NEC ya CCM ni kupanua demokrasia ya maamuzi kwa kurejesha majina mawili ya mshindi wa kwanza katika kura za maoni na mshindi wa pili ili sasa Mkutano Mkuu wa jimbo upigie kura majina hayo mawili na baadae kutoa fursa kwa vikao vya juu yaani Kamati za siasa za wilaya na mkoa na baadae CC kujadili na kumpitisha mmoja wapo. Sioni mkanganyiko tena. kwani katika hesabu za kawaida kati ya hao wawili, lazima mmoja apate zaidi ya asilimia hamsini ya kura zote au wagongane au wafungane kwa kupata asilimia hamsini kila mmoja. huo ndiyo uzuri wa demokrasia. lazima ifuate ili kumpata mtu anayekubalika zaidi kuwakilisha chama chetu.
Wale ambao hawana hoja, na badala yake wanataka kupinga kila kitu, sasa niwakati wa kuaibika.

Kwanza kabisa nikushuru kwa kujaribu kutoa ufafanuzi. Kinachofanya huu mchakato wenu uonekane ni MZENGWE wa kutaka kumng'oa Sioi ni mambo yafuatayo

1. Kama CC imekaa ni wazi kuwa imewajadili wagombea wote hao wawili na kuona kuwa wote wanafaa ndiyo maana majina yao yamerudishwa ili wapigiwe kura tena na mkutano mkuu wa wilaya. Sasa CC ina haja gani tena ya kuja kujadili tena wampitishe nani kama lengo ni demokrasia? au demokrasia maana yake ni kupitishwa na CC jina la mwisho? au ni njia nyingine ya kulipana posho za kukutana kunywa chai na kujifanya mnajadili mambo muhimu wakati maamuzi magumu ya kujivua gamba mnayakimbia?

2. Je lengo la maamuzi haya ni kuaibisha watu au kutafuta haki ili apatikane mgombea aliyepata kura halali?, au CCM imeamua kufanya mchakato huu specifically kwa Arumeru ili kuaibisha watu fulani fulani?

Mimi nilitarajia kuwa uamuzi wa mkutano mkuu wa wilaya sasa umepewa nafasi ya mwisho katika kufikia uamuzi wa nani awe mgombea ubunge katika wilaya yao, kama ambavyo ulivyo mkutano mkuu maalum wa CCM Taifa katika kufikia hatua ya mwisho ya kupigia kura majina yanayopelekwa kwao kutoka katika vikao vya juu. Mbona CCM inakuwa na DOUBLE STANDARDS?
 
Mkuu Matola siasa za nchi hii huzijui? rejea uchaguzi wa uenyekiti CDM, "hapa watu wananusuru chama kwa maslahi ya chama" tofauti hapa ni namna tu ya kukinusuru
Sidhani kama njia waliyotumia ni nzuri kunusuru naona kama wanaongeza makovu zaidi.
 
Bob....

Suala si kupata shida kuelewa.....Suala hapa ni Demokrasia....Kutoa wigo kwa wana CHADEMA wenye sifa kujitokeza kugombea Urais kama ilivyo kwa Ubunge na majina yao kujadiliwa na kupitishwa na vikao vya juu vya chama..Kumbuka hata huyo Obama naye wakati wa awamu ya kwanza alipitia katika mchujo ambao uliwashirikishwa wanachama wengine wa chama cha Demokrasia(mfano Hilary Rodham Clinton).....Na mgombea wa CHADEMA kwa mwaka 2010 hakugombea kwa mara ya pili,aligombea kwa mara ya kwanza....Endapo atagombea mwaka 2015 hiyo ndiyo itkuwa mara ya pili....

Btw.....Inawezekana kweli wajumbe wote wa Baraza kuu wakaja na jina moja?.......

Cha msingi(kwa lengo la kuboresha) ni kutoa fursa kwa wanachama wote wanaojiona wana sifa za kugombea Urais wawe huru kujitokeza na kugombea kuteuliwa na chama katika uchaguzi wa Rais......N mtazamo tu...

Bala.
Sawa tuzungumzie Demokrasia.. Hivi demokrasia inaaza pale mtu anapopewa nafasi ya kugombea au demokrasia ni pale watu wanapopewa nafasi ya kumchagua kiongozi wamtakaye... Sioni tafsiri halisi haswa ni ipi. Kama Chadema wameamua badala ya kila mtu achukue form halafu baraza linawachambua kulingana na vigezo vyao kwa nini isiwe rahisi kuwapa nafasi hiyo baraza hilo lije na majina ambayo wao tayari wanayaona yana sifa hizo kuliko mimi hapa Mkandara nichukue form kwa fikra kwamba nataka niwe rais (ambition) kumbe uwezo huo sina ila nije umbuliwa ktk vikao vya chama!. Ni vizuri sana kupendekezwa kuliko kujipendekeza hasa ktk nafasi hii ya Urais (a Leader).

Chadema haimkatazi mtu kugombea Urais isipokuwa msingi wa kumpata kiongozi wenu ni wa wanachi wenyewe wakijua tunamtaka kiongozi wa aina gani anayetufaa maana hili sio Jeshi, Polisi au shirika kutafuta mwenye CV baabu kubwa. Hivyo ipo sababu ya kuwapa mabaraza haya mawili kumchagua kiongozi wao ambaye atawawakilisha wote, japokuwa kama kuna Upinzani unapewa ruksa kuweka Upinzani.

Kama Chadema wangefuata mfumo wa Marekani au Ulaya basi tusingempata mtu kama Dr. Slaa maana hakutaka kugombea wala hakujua hazina alokuwa nayoi isipokuwa sisi wanachama. Na hii ndio sifa kubwa ya chama hiki kuwapa nafasi wananchi wenyewe kupitia wajumbe wao wamchague kiongozi anayewafaa.
 
Mimi nilitarajia kuwa uamuzi wa mkutano mkuu wa wilaya sasa umepewa nafasi ya mwisho katika kufikia uamuzi wa nani awe mgombea ubunge katika wilaya yao, kama ambavyo ulivyo mkutano mkuu maalum kufikia hatua ya mwisho ya kupigia kura majina yanayopelekwa kwao kutoka katika vikao vya juu. Mbona CCM inakuwa na DOUBLE STANDARDS?
Mara zote mgombea anayechaguliwa na Mkutano Mkuu wa Wilaya jina lake hupelekwa kwenye ngazi ya mkoa kujadiliwa na baadae hupelekwa CC kwa ajili ya kujadiliwa...CC ndiyo hupitisha na kutangaza majina ya wagombea wa CCM katika chaguzi zote.....
 
Kumbe Chadema wameishapitisha jina la mgombea wa kiti cha ubunge Arumeru, kwa hiyo March 3 mlisema mtatangaza jina la mgombea ni zuga bwegee.

aliyekwambia jina la mgombea kutoka chadema linatangazwa jf na some jf member ni nani?
Pelekeni shule vilaza wenu, hasa mwigulu....hata katiba yenu hawaijui.

Oooh....mmezoea kuamua mnachotaka, this time mnatumia katiba, next time mnatupa katiba kule, mnatumia maneno ya makamba au mwigulu..
Why cant you stop using money in every litle thing?!! Blinded kengez!!
 
Back
Top Bottom