Acha Uvivu
JF-Expert Member
- Apr 28, 2011
- 524
- 131
Huyo 'Sioi Mi Msumari' kweli hatoweza 'kuoa' kura katika round ya pili baada ya kuchomachoma na 'msumari'=mshiko, round ya kwanza.
Kwahiyo Jimbo la Arusha mjini ambako ndio roho ya Arusha hawakulitaka!!?? kama nimekuelewa vizuri.Nitarudia kusema haya... CCM wakitaka kushindwa watashindwa lakini wakilitaka jimbo la Arumeru watalichukua na hakuna wa kumzuia....Hizi porojo zetu sisi wote hapa ni matumaini HOPE ambayo inategemea na CCM wanataka nini, lakini bado kabisa wananchi hawana nguvu ya maamuzi...Mtanisamehe ila ndio ukweli unaouma sana.
Huitajiki kuwa na Degree ili ufahamu kwamba hili jimbo tayari limekwenda CHADEMA. CCM itaingia kwenye uchaguzi ikiwa vipande vipande, nawashauri viongozi wa CHADEMA kama wanaisoma thread hii wasitangaze mgombea wao mpaka Magamba watangaze mgombea wao, kuna kazungurukee hapa inataka kufanyika.
Huo ndio ukweli wenyewe...the funny thing is wanagombea nafasi ya pili nyuma ya Nassari, Chadema inatisha.
Mi nawasahuri CCM kutokana na hali tete waliyonayo ni vyema wasishiriki huu uchaguzi maana utawamaliza tu!
Ukweli una tabia moja kuu, nayo ni kusimama kuwa kweli milele. CCM hapo wanajipa matumaini ya kutumia dola ili kushinda huo uchaguzi na sio kura za wananchi na ndio maana wameshindwa kuheshimu maoni ya kura za wanachama wao, hivi ni lini uliwahi kusikia CCM kura za maoni unahitajika upate over 50%?Matola,
Umesema huitajiki kuwa na degree kufahamu jimbo linakwenda Chadema, halafu hapo hapo unapata wasiwasi unatoa na ushauri kwa Chadema wasimtangaze kwanza mgombea wao, mwisho wa uchaguzi najua utakuja humu Jamvini na kusema tumeibiwa kura tulikuwa tumeshinda.
KATIBA YA CCM
20. (1) Mwanachama anayeomba nafasi ya
uongozi wa aina yoyote katika CCM
hatakubaliwa kuwa amechaguliwa mpaka awe
amepata zaidi ya nusu ya kura halali zilizopigwa.
[/QUOTE
wewe nape tumia ID yako
Mkuu,
Mimi ni Mwakalinga aka Mtanzania na Wakongwe hapa wanajua. Natumia majina yangu kamili wala sihitaji kuficha ID.
Siku chache baada ya Wiliam Sarakikya kutaka kuhamia Chadema huku aliekuwa mshindi wa tano (Msani) akihamia chadema chama cha Mapinduzi wamekubaliana na matakwa ya Wiliam Sarakikya kuwa uchauguzi huo urudiwe, kamati kuu ya ccm (CC) kupitia msemaji wake Nape Nauye amesema uchaguzi huo utarudiwa tarehe 1-3-2012, huku akiwataja watakao chuana kuwa ni Wiliam Sarakikya na Sioi Sumari alie tumia zaidi ya mil 100 kwenye uchaguzi uliopita.
Hapana......Hapa tunazungumzia utaratibu......Kila chama si kina taratibu mkuu?,achana na suala la past ama present issues...Swala ni je,utaratibu uliotumika kuwapata wagombea Urais na wale wa viti maalum ulikuwa ni sahii?,upo kwenye katiba ya CHADEMA?......Balantanda..that was then this is now, talk on the present issues.
Which is better, kuchangiwa na wapiga kura wako (CDM) au kuwahonga wapiga kura (CCM)?
Walilitaka sana isipokuwa hapakuwa na jinsi ila naweza sema hivi pengine hata Arumeru walishindwa mwaka 2010 ukizingatia wananchi waliojiandikisha kupiga kura na matokeo ya kura...Na yapo majimbo kibao wameachia na mengine kuzuia ili mradi wawe na nguvu ya rais na bungeni.Kwahiyo Jimbo la Arusha mjini ambako ndio roho ya Arusha hawakulitaka!!?? kama nimekuelewa vizuri.
Hapa tunajadili siasa za pande zote hata wewe umeuliza uteuzi wa Chadema wa urais na viti maalumu so hakuna mwenye ngoswe hapa.Ya Ngoswe............
Mkuu nakuhakikishia kwenye masuala ya kutafuta wagombe wa nafasi mbali mbali CDM nayo ni moja ya vyama havina kabisa hiyo demokrasiaBalantanda..that was then this is now, talk on the present issues.
Which is better, kuchangiwa na wapiga kura wako (CDM) au kuwahonga wapiga kura (CCM)?
Sawa kabisa una point mkuu, kwani katiba ya Chadema inasema vipi?...Na uchaguzi halali ni upi au unatakiwa uwe vipi?..Hapana......Hapa tunazungumzia utaratibu......Kila chama si kina taratibu mkuu?,achana na suala la past ama present issues...Swala ni je,utaratibu uliotumika kuwapata wagombea Urais na wale wa viti maalum ulikuwa ni sahii?,upo kwenye katiba ya CHADEMA?......
Halafu......Achana na suala Rushwa ndani ya CCM....Nilichotaka mimi unieleze ni kwa nini Nassari anaendesha harambee ya kuchangisa fedha za kumsaidia katika uchaguzi ilhali bado hajapitishwa na chama kama mgombea Ubunge wa CHADEMA?.......Isije suala hili likaja kuleta matatizo mbeleni(endapo Nassari atachaguliwa) na kuleta mgogoro miongoni mwa walioomba kuteuliwa kugombea ubunge kwa tiketi ya CHADEMA....Hili ni angalizo tu
Teh teh.........Lol!.....Hapa tunajadili siasa za pande zote hata wewe umeuliza uteuzi wa Chadema wa urais na viti maalumu so hakuna mwenye ngoswe hapa.
Muda wote katiba ya CCM inasema hivyo. Kwenye kura za maoni za mwaka 2010 CCM walibadili utaratibu na wakaamua wanachama wote wapige kura. Kwasababu ya ugumu wa ku organise uchaguzi wa wanachama wote mara mbili, wakaweka waraka wa uchaguzi ambao ulikuwa unasema mshindi atapatikana kwa a simple majority.
Kwenye by-elections kama hii ya Arumeru au ile ya Igunga wanatumia utaratibu ule ule wa zamani wa Mkutano mkuu wa CCM wa wilaya kwenye kura za maoni. Kwahiyo kwa maoni yangu mimi nilitegemea hata hicho kifungu cha asilimia 50 kitumike. Nilishangaa kwenye hili la Arumeru wakatumia simple majority.
Nafikiri msimamizi alichemsha na akatumia waraka wa uchaguzi wa 2010 kuendesha kura ya maoni kwa kutumia mkutano mkuu wa CCM wa wilaya. Kitu ambacho kilikuwa makosa.
wanaojua zaidi wamesahihisha na kwa mawazo yangu mimi wako sahihi.