Hakuna mahala kanuni za CCM inasema mgombea ubunge lazima apate asilimia 50 isipokuwa nafasi ya rais tu..
Kanuni za wagombea wa CCM ngazi ya Uwakilishi/Ubunge inasema hivi:-
(iv)
Ngazi ya Baraza la Wawakilishi/Bunge:
(1)
Wagombea watapigiwa kura za maoni na Mkutano Mkuu wa CCM wa kilaJimbo la Uchaguzi linalohusika,(2) Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu ya CCM ya Wilaya itawajadili wagombea.(3) Kwa upande wa Tanzania Bara, Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu ya CCMya Mkoa itawajadili wagombea na kuwatolea mapendekezo yake kwa KamatiKuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa. Kwa upande wa Tanzania Zanzibar, Kamatiya Siasa ya Mkoa itawajadili wagombea na kuwatolea mapendekezo yake kwaKamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa ambayo nayo itatoamapendekezo yake kwa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa.(4) Kamati Kuu itawajadili wagombea wote na kutoa mapendekezo yake kwaHalmashauri Kuu ya CCM ya Taifa kwa ajili ya uteuzi wa mwisho.Katika kufanya kazi hiyo kwa upande wa Wabunge/Wawakilishi wanaomalizamuda wao, Kamati Kuu itazingatia pia tathmini itakayokuwa imefanyika ya
utendaji kazi wao katika kipindi kinachomalizika..