KATIBA YA CCM
20. (1) Mwanachama anayeomba nafasi ya
uongozi wa aina yoyote katika CCM
hatakubaliwa kuwa amechaguliwa mpaka awe
amepata zaidi ya nusu ya kura halali zilizopigwa.
[/QUOTE
wewe nape tumia ID yako
Umechanganya ma-file, Mtanzania atabaki kuwa ni Mtanzania na mabandiko yake yameenda shule. Kwa kukusaidia tu, Mtanzania sio Nape!
I knew you will rush to comment on this post... vipi engineer wa gogoro la Chadema linaendeleaje, sisi letu huku mambo mswano kura hazikutosha sasa wamebaki wawili ile mbinu yetu ya 50/50 haitaapply tena, labda tusingizie kura nyingi zimeharibika kwa hiyo hakuna tena aliyefikisha 50% unajua tena lazima yule jamaa aapishwe hofu yetu mamvi tu msalimie nape nisikucheleweshe na sredi yako ya gogoro la CDM.Kumbe Chadema wameishapitisha jina la mgombea wa kiti cha ubunge Arumeru, kwa hiyo March 3 mlisema mtatangaza jina la mgombea ni zuga bwegee.
Muda wote katiba ya CCM inasema hivyo. Kwenye kura za maoni za mwaka 2010 CCM walibadili utaratibu na wakaamua wanachama wote wapige kura. Kwasababu ya ugumu wa ku organise uchaguzi wa wanachama wote mara mbili, wakaweka waraka wa uchaguzi ambao ulikuwa unasema mshindi atapatikana kwa a simple majority.
Kwenye by-elections kama hii ya Arumeru au ile ya Igunga wanatumia utaratibu ule ule wa zamani wa Mkutano mkuu wa CCM wa wilaya kwenye kura za maoni. Kwahiyo kwa maoni yangu mimi nilitegemea hata hicho kifungu cha asilimia 50 kitumike. Nilishangaa kwenye hili la Arumeru wakatumia simple majority.
Nafikiri msimamizi alichemsha na akatumia waraka wa uchaguzi wa 2010 kuendesha kura ya maoni kwa kutumia mkutano mkuu wa CCM wa wilaya. Kitu ambacho kilikuwa makosa.
wanaojua zaidi wamesahihisha na kwa mawazo yangu mimi wako sahihi.
Hivi inakuwaje watu wanafanya uchaguzi bila kujua kanuni? CCM wanaendelea kujivua nguo hadharani.
Ni dalili njema kwa ustawi wa taifa.
Hapo nimekukubali Mkuu, kwa maana nyingine ni kwamba wagombea wengine wote watashirikiana kuona Sioi hapati kura zao kwenye uchaguzi huu!!!! Hiyo itampa nafasi Sarakikya apitishwe kwe mizengwe ile ile ya CCM maghamba kama ilivyo ada!!!!!!!Lengo la CCM ni kuhakikisha Sioi hagombei maana itaweka chama katika sura ya kiukoo zaidi. Mi nisema huko nyuma https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...aba-yake-arumeru-mashariki-3.html#post3360164 kuwa CCM haiwezi ku-affort' nepotism politics kwani wananchi wengi wamewashitukia kuwa viongozi wanaandaa watoto wao kuja kutawala watoto.
Kwa kuwa wagombea wote walioshindwa hawamuungi mkono Sioi, maana yake wafuasi wao pia, na hiyo ni ishara ya wazi kuwa Sioi hatagombea kwa ticket ya CCM.
Mnazungusha uongo weee wakati inajulikana wazi kwamba huyo Sioi Nassari ni chaguo la Lowassa, na wanataka kumpiga chini -Vita ndani ya chama inaendelea..
Mnazungusha uongo weee wakati inajulikana wazi kwamba huyo Sioi Nassari ni chaguo la Lowassa, na wanataka kumpiga chini -Vita ndani ya chama inaendelea..
I knew you will rush to comment on this post... vipi engineer wa gogoro la Chadema linaendeleaje, sisi letu huku mambo mswano kura hazikutosha sasa wamebaki wawili ile mbinu yetu ya 50/50 haitaapply tena, labda tusingizie kura nyingi zimeharibika kwa hiyo hakuna tena aliyefikisha 50% unajua tena lazima yule jamaa aapishwe hofu yetu mamvi tu msalimie nape nisikucheleweshe na sredi yako ya gogoro la CDM.
Wacha woga Ritz hiyo si kweli ila dogo Nasri anapiga jalamba, mtu akipiga jalamba coach ndiye anachagua mchezaji wa kuingia uwanjani!!!! Tarehe 1/3/2012 CDM watachagua mgombea wa ARUMERU!!!! Ila kwenye mchakato Joshua Nasari yumo pia, naona unatetemeka au vipi????Mkuu mkandara,
Mbona Chadema wameishapitisha jina la Nassari, kabla ya mchakato wa kuwachuja wagombea ambao kwa mujibu wa Chadema mgombea watamteuwa March 3.
Kibaya zaidi wagombea wenzake wamelalamika mwenzao kafanyiwa harambee na viongozi wa chama hakiwemo Lema, wamekusanya Sh10 milioni pamoja na magari manane kwa ajili ya kampeni za ubunge.
CCM kwa kujifariji na matukio ya zamani....tunaongelea kitendo mnachotaka kumfanyia mtoto wa marehemu si kizuri hata washili hawatafurahi.CDM bana wapo bize na taratibu za wenzenu, waacheni jamani au mmesahau mlivyopata mgombea rais na viti maalum?
Nipo sana tu ila nina kazi nyingine ktk siasa za Bongo hapa JF..Dah unajua uzee tena nimetaarifiwa tu ya kwamba Sioi ni mtu wa Lowassa basi nikakimbilia keyboard bila kujua ubini wake. Samahani mkuu wangu lakini ndivyo ilivyo Lowassa atakuwa na wakati mgumu sana CCM kuliko wengi wanavyofikiria.Mkuu Mkandara,
Sijakuona kitambo mzee wangu. Unachosema ni kweli kwa 100%. Ila umechanganya majina, kijana huyo anaitwa SIOI Sumari. Naona umeunganisha majina ya wagombea 2 kutoka vyama tofauti.
Kosa la kijana [Sioi] ni kuwa mtoto wa Marehemu Mzee Sumari, halafu kuwa mkwe wa EL na kibaya kuliko yote James ole Millya kujiingiza kwenye siasa za Arumeru ambako kumemchafulia huyo Sioi. Hata kama Sioi angekuwa na sifa za kugombea, kitendo cha kuwa karibu na Lowassa na kuwatumia wapambe wa Lowassa kwenye vuguvugu za kampeni kunanzisha mgogoro upya kabisa kati ya Mary Chatanda vs James ole Millya.
Kijana ana bahati mbaya sana, maana anaweza kuhukumiwa kwa makosa ambayo sio yake hata kama alikuwa na sifa zote za kuteuliwa kuwa mgombea.
Na hao waliotoa rushwa kumpitisha Sioi wawajibishwe tafadhali. Hebu tupe habari, kuhusu swala la uraia wamefikia wapi, au wamelipotezea?