Uchaguzi wa mwaka 2010 haukufuata mchakato huu......Utaratibu ulibadilishwa lakini baada ya uchaguzi utaratibu ulirudishwa na kwa kuanzia ulitumika katika uchaguzi mdogo wa jimbo la Igunga......Kwa utaratibu wa CCMKamati kuu ndiyo yenye maamuzi ya mwisho ya nani akiwakilishe chama katika uchaguzi husika....Na huu ni utaratibu ambao kimsingi una mapungufu mengi,kuna haja ya wanaCCM wa eneo husika wakaachiwa mamlaka ya kuchagua ni nani awawakilishe katika uchaguzi husika(sitegemei kuona vyama vingine vinatumia utaratibu kama huu wa CCM).....Kimsingi yote haya yanafanyika kutokana na makundi/mpasuko mkubwa uliopo ndani ya CCM ambapo mgawanyiko wa kimakundi ndani ya chama unapelekea makundi husika kupambana na kila kundi kutaka kumuweka mgombea linayemtaka yeye....
Utaratibu umetumika kwa mujibu wa Ibara ya 20(Kifungu cha 1 cha 2 na cha 3 cha Katiba ya CCM)
20. (1) Mwanachama anayeomba nafasi ya
uongozi wa aina yoyote katika CCM
hatakubaliwa kuwa amechaguliwa mpaka awe
amepata zaidi ya nusu ya kura halali zilizopigwa.
(2) Katika uchaguzi wa kujaza nafasi nyingi
kwa pamoja, ushindi utahesabiwa kwa kufuata
wingi wa kura alizopata mwombaji wa nafasi
hiyo zaidi ya wenzake, bila kujali kama kura
hizo zinafikia nusu ya kura halali zilizopigwa.
(3) Kanuni za Uchaguzi wa CCM zitaweka
vifungu mahsusi, vitakavyowezesha uwakilishi
wa Wanawake katika vikao vya CCM hatimaye
kuwa si chini ya asilimia 50 ya wajumbe wote
wanaochaguliwa kujaza nafasi za makundi,
kwa kila ngazi ya uongozi wa Chama.