Ndugu zangu wa Chadema naomba niwakumbishe jambo moja la msingi sana. Adui anaweza kutumia mbinu ya kitoto sana kukuangamiza. na mbinu hii inaitwa HILA. Hila ni pale adui anapokuletea jambo ukaliona kama ni zuri kwa muonekano wa kwanza ila ukishajiingiza linakurudi na linakuweka katika hali ambayo inakugharimu au kukuweka katika hali mbaya kuliko ulivyokuwa kabla ya kukubali kuingia kwenye mtego. CCM na mapandikizi yao wanatumia mbinu ya ya kuleta hoja kuujadili uraisi kwa sasa ili Wanachadema wajisahau wabaki wanalumbania uraisi halafu hiyo iwe chanzo cha migogoro na kujisahau kupambana na ufisadi na kukujenga chama, halafu wapate upenyo wa kuwamaliza Chadema. Ukiangalia viongozi wengi wa chadema hawajihusishi sana na suala la nani agombee 2015, wengi wako bussy kukijenga chama katika maeneo mbalimbali ya nchi. Huyu Dr. Slaa anayejadiliwa hapa nakumbuka katika mahojiano na mwandishi mmoja wa habari aliulizwa kama atagombea 2015, akajibu hivi: Vikao vya chama ndio vinamteua Mtu atakayeshika bendera kukiwakilisha chama katika nafasi ya uraisi, Hivyo mimi siwezi kusema sasa hivi kama nitagombea au la. Hayo ni maamuzi ya vikao wakati ukifika. Nawaomba wana CDM tuachane na hoja za namna hii kwa sasa. hoja yetu kubwa iwe ni kupambana na ufisadi na kukijenga chama. Ili tuweze kuwangoa hawa Magamba.