ZZK ni kijana smart na anafaa kuwa Mgombea wa Urais, na kwa hakika ana uwezo na uelewa mpana sana wa mambo mbalimbali ukilinganisha na WPS(ambaye ni popular kwa sababu ambazo 'zinajulikana'). Semeni kweli jama, WPS hana hoja zaidi ya kupiga kelele na radicalism, siyo mbunifu na wala hana qualities za uongozi, labda kama uanaharakati. Pia ile kauli yake ya nchi 'haitatawalika' inamgharimu sana, maana watu wana hofu hata kama yeye atashinda na kuwa Rais hatoweza kutawala kwa amani, nchi inaweza kuingia kwenye machafuko maana wanaccm watamrudi na wao kwa hasira. Pia udini na historia mbaya ya kampeni zake za 2010 za makanisani ni mambo ambayo yatamrudisha nyuma sana 2015 kama atapewa bendera apeperushe.
kama CDM inataka kushinda iweke mtu mpya na mwenye mvuto na si WPS ambaye amezoeleka na bahati mbaya sana ni mzee tena mgonjwa.
Kosa mtakalokuja kufanya CDM ni kutuletea mgombea Urais kama Slaa, hivi akishinda itakuwaje ataongea nini sasa, ataendelea kumtukana Kikwete na viongozi waliotangulia kwa hoja yake moja tu aliyonayo ya 'ufisadi' ama ataanza kuhaha kushika hapa na pale? Slaa ni mtu asiye na objectivity na ninadhani ana matatizo kwenye elimu yake na msingi wake wa maadili, hafai kuwa Rais wa nchi! Kama kanisani kwa mungu walimwona hafai wakamfukuza sasa atakuja kufaa leo hii huku duniani?
ZZK amejifunza uongozi na ameiva, na ninadhani anafaa kupewa nafasi aoneshe kipaji chake, na akikosa mara ya kwanza CDM mtakuwa mmemuandaa kwa ajili ya baadaye! Maana umaarufu wenu unakuwa kwa kasi na ipo siku mtapata Urais wa nchi, sasa kuweni makini, msiwe na haraka msikurupuke, tumieni vipaji vya vijana wenu vizuri!
WPS hana sifa ya kugombea Urais achilia mbali sifa za kuwa rais kwa sababu ni mdini, ana taswira ya udini (hata kama atakuwa siyo mdini kivile bado sisi wananchi wa kawaida tunamuona ni padri!) na hivyo hafai kuongoza taifa la watu wenye imani mchanganyiko kama Tanzania. Mkitaka muishie pale pale pa 2010 wekeni WPS na mtaona hamtofika popote, mkitaka kusonga mbele zaidi ya 2010 wekeni ZZK ama Freeman Mbowe (hawa wana dini zao lakini hawana taswira ya udini). kwa kuwa kura ni ya ZZK vs WPS, basi nachagua ZZK zaidi ya WPS.
WPS amesomea dini tu, hana elimu nyengine ya kidunia, watu wengi wana mashaka na elimu yake. Pia afya yake ni mgogoro na umri umemtupa mkono hawezi kupiga kampeni nzito za kutafuta Urais nchi nzima hii