Kura ya maoni: Zitto vs Dr Slaa

Ni nani ungependa agombee urais mwaka 2015 kwa tiketi ya CHADEMA?

  • Zitto Z. Kabwe

    Votes: 180 15.3%
  • Wilbrod P. Slaa

    Votes: 996 84.7%

  • Total voters
    1,176
  • Poll closed .
Status
Not open for further replies.
Tashangaa sana kama Zitto atatoshwa wakati ni CDM ni chama cha Demokrasia na Maendeleo sio kama CUF tangia nimeifahamu mgombea urais ni mmoja tu Lipumba.
 
Mimi nasema Dr. Slaa ndiye anayefaa kuwa Rais wanchi hii. Anauwezo wakuongoza na ni mchapakazi asiyeweka pesa mbele kama zito. Oooh i wish the Dr. slaa to be my pres.. now!! kura yangu natoa kwa Dr. slaa. our next pres is Dr.Slaa. Thanks!
 
Mi nitasema siku zote daima, kura yangu siwezi kumpa baba Chachage hata siku 1 labda aoneshe possitive changes on his political carrier, kitendo cha kuyafuga yale masalia aliyokuwa akiyaweka mjini lakin akiyatetea lakin mwisho wa siku Mungu akaamua kuwaumbua wanafiki na unafiki wao leo hii masalia yapo uchi tena yamerudi kwa baba zao kule maCCMemuni ni ushahidi tosha huyu comrade ni hatari kwa usalama wa CHADEMA towards 2015. Period
 
Ingawa Mada ni ya kichokozi, '' Mimi nimeshindwa kumuelewa zito anapotanagaza mapema kuhusu dhamira yake ya kutaka Urais. Ingawa si kinyume na sheria lakini hazitendei haki kanuni za Umoja wa kichama hasa wakati huu ambapo chama kiko katika harakati za M4C kujiandaa kushika dola 2015. Zito haonekani mara nyingi katika harakati na matukio ya kichama. Hakuonekana Uzinduzi wa M4C pale Jangwani na katika Routes nyingine za M4C. Nadhani huu si wakati wa kutangaza nia, kuna mambo mengi ya Msingi na Muhimu kwa wanaCDM na waTZ kwa ujumla wanapaswa kuyaona na hivyo kuwaandaa kuwa chini ya dola itakayoongozwa na CDM. Tuwaandae waTZ kwanza, kisha tuwaombe ridhaa ya kuwaongoza..
 
Tusubiri muda ufike hii kuanza hivi mapema ni kuanza kuvurugana mapema, muda ukifika afanye hivyo na kama katiba itakuwa imeweka umri tofauti na wa mwanzo kwani atakuwa na vigezo.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom