Kura ya maoni: Edward N. Lowassa v/s Bernard K. Membe

Kura ya maoni: Edward N. Lowassa v/s Bernard K. Membe

Ni nani ungependa agombee urais mwaka 2015 kwa tiketi ya CCM?

  • Bernard Membe

    Votes: 70 15.3%
  • Edward Lowassa

    Votes: 189 41.4%
  • None of them (Labda mwingine)

    Votes: 198 43.3%

  • Total voters
    457
  • Poll closed .
Nimeangalia kura hizo naona kumbe watu bado mnampenda Lowassa
Jibu hapo ni "None of them"
 
Lowasa ni fisadi mkuu, ana kashfa nyingi zinazomzunguka, huyu jamaa hafai kabisa kuwa kiongoz wa nchi. kwa upande wa Membe mi sijasikia kashfa yoyote toka kwake na pia simjui kiundani zaidi, huyu angalau ana nafuu kidogo.
Zitaje na uweke ushahidi hapa dhaifu wee!
 
My vote to Lowassa,Membe atatuuza kwa Waarabu na anaonekana kuwa kiongozi asiyeweza kusimama peke yake,anaonekana amekiegemea mno kifua cha Salma.Si ajilaze kwa mkewe?
 
Kwa nini haw wawili? kwani ccm hakuna wanaotufaa kwa urais jamani? kila siku EL, EL, EL what so special in him guys?
 
Wadau nawakilisha hili suala ili kupata kura za maoni za viongozi hawa ndani ya chama cha CCM.

Toa hoja na mawazo yako na upige kura pia kuona nani anafaa kati ya wawili. Zingatieni kuwa hatushindanishi na viongozi wengine ambao kila mmoja amekumbatia moyoni kuwa anafaa. Haijalishi wewe ni Chadema au CCM inachojalisha ni unaona yupi bora kati ya hawa wawili. Kuwa hata kama wote ni devils who is the lesser devil kati ya wawili?

Ni yupi unaona atafaa ama niseme nani angalau anatia matumaini kuwa walau anafaa kuteuliwa kuweza kuongea nafasi ya Urais kwa tiketi ya CCM kwa mwaka 2015?

Ni vema ukimataja utowe walau sababu zako ambazo unaona ni msingi wa maamuzi yako. Wadau hasira na pumba naomba ziachwe nje ya hii thread na tuweze kupata jibu thabiti.

Nawasilisha.

Natamani sana ije thread ya kati ya Lowasa na Slaa, hebu ngoja nikaianzishe
 
Kura za kinafki! Kura za maoni wapige CCM sio watu wengine! CHADEMA wanajua kuwa akigombea MEMBE hawapati, lazima wajifanye kumshabikia MAMVI! Wanajua Mamvi akisimama watapeta tu! Kama na we uliyeleta post umepewa hela na Mamvi, ukome! Kwa nini ulete ya watu wawili tu, kuna aliyetanga kati ya hao anataka uraisi?
 
Sijaona mtu,,,wote wanatumwa na chama wala si mapenzi yao kuwaongoza watz,,mod emu ondoa uzi huu,,we need changes,,YES we can!!!!!
 
EL anafaa maana ni m2 mwenye mawazo ya kitajiri ana take any opportunity inapojitokeza ...............
nyie endeleeni kutafuta wazelendo km nyerere mfe masikini!
 
Uraisi ni zamu ya mikoa ya bara.Uraisi umekaa mikoa ya pwani kwa zaidi ya miaka 30 na akipewa membe mikoa ya pwani itakuwa imengoza nchi kwa miaka 40. Hatukubali. ni Zamu ya mikoa ya bara.
 
Kura za kinafki! Kura za maoni wapige CCM sio watu wengine! CHADEMA wanajua kuwa akigombea MEMBE hawapati, lazima wajifanye kumshabikia MAMVI! Wanajua Mamvi akisimama watapeta tu! Kama na we uliyeleta post umepewa hela na Mamvi, ukome! Kwa nini ulete ya watu wawili tu, kuna aliyetanga kati ya hao anataka uraisi?

Mkuu
ungelijua kuwa huyo unayemwita Mamvi simjui naye hanijui pia na wala si mfaasi wa chama chake,usingesema hivyo.
 
Joka la mdimu tu lile he is another dhaifu in disguise hatutak prezdaa mpiga domo tunataka mtendaji ths tmy

Dada unataka mtendaji gani mwizi huyo! Jamani mnataka nchi hii iuzwe kabisa na jizi EL? Unafahamau uhusiano wa EL na Rostam Aziz? Unafahamu kuwa ni mmoja wa walioficha mabilioni huko Uswisi? Please, please. Hatutaki utendaji usiokuwa na faida kama vile kwenda kuwafokea wakurungezi hadharani. Tunataka mtu atakayesema sasa gesi, madini, mbuga za wanyama, bandari zetu zinazalisha pesa kwa ajili ya maendeleo ya watanzania na si wageni. EL hana hilo, ataendelea kutengeneza Richmond kadhaa tu huku watu wetu wakitaabika na ugumu wa maisha. EL akikamata nchi RA atarudi kwa spidi ya umeme kutuibia. EL, no no no no no no no no!
 
Kama nchi hii imekosa kabisa wagombea na hao ndio pekee waliobaki ndani ya Tanzania basi afadhali Membe amuongoze Lowasa!
 
Wadau nawakilisha hili suala ili kupata kura za maoni za viongozi hawa ndani ya chama cha CCM.

Toa hoja na mawazo yako na upige kura pia kuona nani anafaa kati ya wawili. Zingatieni kuwa hatushindanishi na viongozi wengine ambao kila mmoja amekumbatia moyoni kuwa anafaa. Haijalishi wewe ni Chadema au CCM inachojalisha ni unaona yupi bora kati ya hawa wawili. Kuwa hata kama wote ni devils who is the lesser devil kati ya wawili?

Ni yupi unaona atafaa ama niseme nani angalau anatia matumaini kuwa walau anafaa kuteuliwa kuweza kuongea nafasi ya Urais kwa tiketi ya CCM kwa mwaka 2015?

Ni vema ukimataja utowe walau sababu zako ambazo unaona ni msingi wa maamuzi yako. Wadau hasira na pumba naomba ziachwe nje ya hii thread na tuweze kupata jibu thabiti.

Nawasilisha.

Mbona unatulazimisha tuchague mmoja kati yao (katika maelezo yako) wakati kwenye pole kuna fursa ya kutompendekeza yeyote?

Kwa nini unataka tuchague mwenye nafuu kwani hakuna watu wengine, si nilisikia ccm kuna hazina kubwa ya viongozi?

simtaki lowassa kwa sababu sina imani naye, ameshakuwa na madaraka toka enzi za Nyerere na bado tu anataka.
simtaki membe kwa sababu alisema anayo majina ya walioficha pesa nje lakini hatutajii mpaka leo, hafai kuwa kiongozi wa nvhi, kiongozi wa nchi lazima awe shupavu muwazi na mwenye uwezo wa kuchukua maamuzi magumu kwa manufaa ya nchi.

Thanks
 
Na Najsi kwangu mimi kumpigia Kura Mwana Magamba yeyoye
 
Back
Top Bottom