Kura ya maoni: Edward N. Lowassa v/s Bernard K. Membe

Kura ya maoni: Edward N. Lowassa v/s Bernard K. Membe

Ni nani ungependa agombee urais mwaka 2015 kwa tiketi ya CCM?

  • Bernard Membe

    Votes: 70 15.3%
  • Edward Lowassa

    Votes: 189 41.4%
  • None of them (Labda mwingine)

    Votes: 198 43.3%

  • Total voters
    457
  • Poll closed .
sioni anayeweza kati ya hawa maana lowasa ni fisadi na membe ni kama jk so labda waangalie mwingine
 
Mh. Edward Ngoyai Lowassa is the coming President of the United Republic of Tanzania 2015, kama CCM hawatamsimamisha Lowassa, CHADEMA ni opportunity yao kuichukuwa nchi hii
 
Mh. Edward Ngoyai Lowassa is the coming President of the United Republic of Tanzania 2015, kama CCM hawatamsimamisha Lowassa, CHADEMA ni opportunity yao kuichukuwa nchi hii
 
Hana lolote huyo, huyo ni mnafiki. Kwa nn hajawataja hao mafisadi ambao alisema anawajua. nawatahadharisha watanzania tutakuwa tumepotea tukimchagua huyu mnafiki
 
Wadau nawakilisha hili suala ili kupata kura za maoni za viongozi hawa ndani ya chama cha CCM.

Toa hoja na mawazo yako na upige kura pia kuona nani anafaa kati ya wawili. Zingatieni kuwa hatushindanishi na viongozi wengine ambao kila mmoja amekumbatia moyoni kuwa anafaa. Haijalishi wewe ni Chadema au CCM inachojalisha ni unaona yupi bora kati ya hawa wawili. Kuwa hata kama wote ni devils who is the lesser devil kati ya wawili?

Ni yupi unaona atafaa ama niseme nani angalau anatia matumaini kuwa walau anafaa kuteuliwa kuweza kuongea nafasi ya Urais kwa tiketi ya CCM kwa mwaka 2015?

Ni vema ukimataja utowe walau sababu zako ambazo unaona ni msingi wa maamuzi yako. Wadau hasira na pumba naomba ziachwe nje ya hii thread na tuweze kupata jibu thabiti.

Nawasilisha.


Ni dharau kuwaambia wana JF kuwa hata kama wewe ni CDM we piga kura kuonyesha who's the lesser devil. No this is not the manner in which great thinkers should behave. Huwezi kuwa ni mwanachama wa chama kingine na chama hicho kinao watu who can make right candidate yet you live in a planet that makes you not make the right decision. Ndio maana nasema bora kiongozi mbaya wa CDM kuliko kiongozi mzuri wa CCM katika kuongoza nchi come 2015. Au bora kiongozi mbaya wa chama kingine kuliko kiongozi mzuri toka CCM. Nina sababu. Huwezi kuongoza nchi bila kuwa na dira. CCM walikuwa na Azimio la Arusha wakaliua na kulizika wakaleta Azio la kitapeli za Zanzibar na mpaka leo hii huwa hawataki kuliongelea hata kidogo achilia mbali kuandikwa sehemu yoyote. Ndio maana hata wamekuwa wagumu kutekeleza ilani zao za uchaguzi na wakabaki kurushiana mpira wa 'oh mimi sikutengeneza ilani walitengeza wengine, mara oh mimi simo na mengine mengi' Haya yanatokea mchana kweupe na wale mnaowaona ni wazuri CCM kuweza kukabidhiwa madaraka makubwa ya kutupeleka tunakotaka taka kwenda wamo lakini hawajitengi nahali ya kuenenenda bila mwongozo. Ni vema kama wangekuwa wamesemakuwa tunafata hitikadi fulani basi tungewapigia kura. Lakini kwa kuwa na wao ni wakimya sasa tuwape madaraka ili watupeleke wapi- Ubepari, Ujamaa, Mchanganyiko wa ubepari na ujamaa (social democracy) au wapi. Wote wawili hawafai katika uongozi wa dunia ya kileo
 
Mh. Edward Ngoyai Lowassa is the coming President of the United Republic of Tanzania 2015, kama CCM hawatamsimamisha Lowassa, CHADEMA ni opportunity yao kuichukuwa nchi hii


Naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja kwamba Lowassa ni jembe hayo mambo yaliyotokea ni siasa za maji taka tu...Lowasa apewe nchi tuache kudanganywa...kutoe nchi kwa watu wanadhubutu kusema na wenye uwezo wa kifedha siyo masikini wengine mara tu wakipata wanaanza kufikiria kujenga mahoteli kusomesha machangazi, masheji watoto wa jirani na mwisho wa siku tunabakia palepale
 
Devils, who cares. Sichagui mashetani mimi.


Hakuna chaguo.. katika pool ya ccm wanachama milion 4 hizo ''devils'' mbili ndiyo majembe yao wanayotanguliza... Surphuric acid na cynide ipi iwezayo kumpatia mgonjwa nafuu ? Ni dhahiri moja inauwa palepale na nyingine inauma taratibu na utumbo unakatika huku mhusika hakishuhudia maumivu lakini wate atakufa...

Hitimisho wote hawafai kwa mstakabali wa Tanzania tuipendayo... bring new face no these not those ''dressed chimpasee''
 
Devils, who cares. Sichagui
mashetani mimi.


Hakuna chaguo.. katika pool ya ccm wanachama milion 4 hizo ''devils''
mbili ndiyo majembe yao wanayotanguliza... Surphuric acid na cynide ipi
iwezayo kumpatia mgonjwa nafuu ? Ni dhahiri moja inauwa palepale na
nyingine inauma taratibu na utumbo unakatika huku mhusika hakishuhudia
maumivu lakini wate atakufa...

Hitimisho wote hawafai kwa mstakabali wa Tanzania tuipendayo... bring
new face no these not those ''dressed chimpasee''

Mkuu,piga kura yako "labda mwingine"
 
hawatafaa wote,kwani watatumia muda mwingi kulipa visasi kw maadui zao
 
Lowasa ni jembe nalikubali sana coz ni man of Action sio porojo za membe!
 
Hana lolote huyo, huyo ni mnafiki. Kwa nn hajawataja hao mafisadi ambao alisema anawajua. nawatahadharisha watanzania tutakuwa tumepotea tukimchagua huyu mnafiki
Mnafiki nani mkuu?hebu funguka kidogo!
 
bora membe aisee, hatutaki kuingizwa kwenye maden mengine ya ajabu
Sasa mchague Membe lakini kumbuka walibya nao watakuja kudai chao tena na usumbufu.
 
Hizi kura za maoni zipigwe marufuku. Zinawafundisha watu jinsi ya kupiga kura. Bernadeta Kilian na hao experts na spin doctors wote ni marafiki. They conspire to make people vote as dertemined by the pollsters.
 
Atakayeshinda katika poll hii naomba apambanishwe na Dr. Slaa!!!
 
Duh!! Great thinkers!! Mnamlinganisha Lowassa na Joka kuu? Lol
 
Hakuna hata mwenye nafuu hapo. Wote ni maiti. Tofauti yao ni kuwa wamekufa siku tofauti. Hata kunuka kwao ni tofauti.
nicas mdogo wangu, nakuambia hakuna mtu mwenye nguvu na ambaye atagombea uraisi zaid ya lowassa na nakuhakikishia ukitaka ccm ishinde imsimamishe huyu ila ikiloba step tu imekula kwao.
tuache unafiki tuongee reality, kuna nani ambaye anaweza japo kuonyesha uthubutu wa uwajibikaji kama alivyo lowassa ukicompea na wengine hao??
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom