Kupewa mara moja tu kwa mwezi...

Nivea NAKUSHUKURU SANA KWA WARAKA WAKO Leo nikirud nyumbani nalianzisha darasa. Asante sana
 
Pole sana mkuu.
Sijui imani yako ila kama ni mkristo, tafuta mchungaji wa ukweli ufanye naye maombi. Mambo haya huwa yanaandamana sana na mambo ya kipepo. Vita vyetu si vya damu a nyama bali ni vya kiroho zaidi.
Nimebold mchungaji wa ukweli maana wengi wao wamekaa kibiashara ziadi.Mwenyezi Mungu atunusuru na hili janga
 
kama unabembeleza kama unaomba emplyment na unanyimwa basi hau-qualify kwenye hiyo position!!!:bange:

hahahahaaaaa!!!............pole sana, katafute kazi inayokufaaa.........!!!!

:happy:
 
mambo haya bana.....sasa kwa nini....?....khaa!!...

Sijui mnamuonea aibu kumwambia ukweli ?
Si mwambieni tu? Mnammung'unyia maneno ya nini ?
Braza mleta mada ni hivi : -
Hapo hamna ndoa! Ilikwisha expire!
Huo sio mshahara wa kupata mwezi mpaka mwezi .
 
Nimewahi kusikia kesi kama hizi nyingi lakini mara nyingi hutokea kama mume yuko bize sana na kazi na kushindwa kuonyesha ukaribu na mapenzi kwa mkewe, hutokea pia kama mke kapata nyumba ndogo na saa nyingine ni frustration ambazo mke anaweza kuwa kazipata kwa sababu mbali mbali either za kiofisi au za kifamilia.

Jaribu kutumia njia rahisi zaidi ya kuwa karibu naye na kumjali. Mnunulie zawadi mbali mbali na pia mtoe out mara kwa mara na anza ku-observe mabadiliko. Onyesha kumkumbuka na kum-miss pia mtumie hata meseji za mapenzi na kumtania. Kama ni matatizo ya kisaikolojia na frustration yanaweza kuishi kwa njia hii.

Hili zoezi likishindikana, fanya uchunguzi wa kina isije kuwa kuna kidudu mtu kishaanza kukuibia.
 
kama unabembeleza kama unaomba emplyment na unanyimwa basi hau-qualify kwenye hiyo position!!!:bange:
Hahahahaaaaa!!!............pole sana, katafute kazi inayokufaaa.........!!!!:happy:
ka! Coments zingine bana, wakati namuoa mbona niliqualify iweje leo sina qualification?
 
Hivi kati yako na huyo mwenzako, ni nani hasa aliyemuoa mwenzake?
 
[h=2]
icon1.png
Re: Kupewa mara moja tu kwa mwezi.[/h]
Mithali 14:1 Kila mwanamke aliye na hekima hujenga nyumba yake; bali aliye mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
1. Je, ninajenga nyumba yangu au naibomoa?
2. Je, ninawekeza kwenye ndoa yangu? Natumia uwezo wangu kuiboresha?
3. Je, naonyesha kumthamini na kumjali mume wangu?
4. Je, natumia nguvu zangu na uwezo wangu kwa ajili ya familia yangu?
5. Je, natengeneza mazingira kwa maneno na matendo yangu yakumfanya mume wangu afurahie na kupenda kuwa nyumbani?
6. Je, naridhika na kuihudumia familia yangu?
7. Je, hisia zangu na upendo wangu ni kwa ajili ya mume wangu au mtu mwingine? Je, muonekano wangu, maneno mazuri na ushawishi mwema ni kwa ajili ya mume wangu au watu wengine?
8. Je, natimiza mahitaji ya mume wangu?
9. Je, ni mwaminifu kwa mume wangu? Nina uhusiano wowote wa siri ambao sitaki mume wangu ajue?
10. Je, mume wangu yupo huru kuwa muwazi kabisa kwangu hata kunikosoa?
11. Je, ninaruhusu mawazo ambayo siyo safi kuwa ndani yangu kupitia redio, televisheni au vitabu?
12. Je, nimekuwa kimbilio na faraja kwa mwanaume ambaye ndoa yake ina matatizo?
13. Je, natafuta ushauri na faraja kutoka kwa mwanaume mwingine (mchungaji, kiongozi wa kanisa, mshauri, mfanyakazi mwenzangu) na sio mume wangu kwanza?
14. Je, ninauhusiano wa karibu zaidi na mwanaume mwingine kuliko nilivyo na mume wangu?
15. Je, nimekuwa mkali na mwenye maneno yasiyo ya upole au ni mwenye maneno mazuri na yenye upole na unyenyekevu?
16. Je, naonekanaa rahisi rahisi kwa wanaume wengine au naonekana ni mtu mwenye msimamo? Je, naruhusu mizaha isiyofaa na watu wengine?
17. Je, kuna kitu katika mavazi yangu, muonekano au maongezi ambacho kinaweza kuwa kichocheo kwa wanaume kuwa na tamaa?
18. Je, ninavyoongea na wanaume kazini au popote naonyesha kuwa mimi ni mwanamke wa kristo au nakuwa nawaonyesha upendo na ukaribu wa kupitilizia ambao unapaswa uonyeshwe na wake zao?
19. Je, nimeweka mipaka katika mahusiano yangu na watu wa jinsia ya kiume? Ni mipaka gani hiyo?
20. Je, kuna mausiano niliyonayo ambayo yanaweza kuleta utata kwa watu?
21. Je, mume wangu na watu wengine wanao nifahamu wanaweza kusema kuwa mimi ni mwanamke mwenye busara na anayejiheshimu?
22. Je, nimeazimia moyoni mwangu kuwa safi mbele za Mungu? Je, ni mfano wa kuigwa na wanawake wengine wanaoishi maisha ya kumfuata Mungu?
Mithali 31:10 Mke mwema, ni nani awezaye kumuona? Maana kima chake chapita kima cha marijani.
PRINT HII KARATASI MPELEKEE AJIBU MASWALI YOTE HAYO HAPO JUU TENA WEWE UKIMUULIZA MWENYEWE

nivea mbona una busara hivyo umeolewa au uko single?
 
Last edited by a moderator:
Habari zenu wana jf, nimeoa na nina miaka 4 ya ndoa yangu, kadri siku zinavyokwenda napunguziwa dozi ya mapenz, zilizopita ilikuwa 5 mpaka 6 per month sasa hivi ni 1per month na anakua mkali yaani mpaka nibembeleze kama naomba employment ukipewa unaambiwa utapata tarehe kama hi next month nampenda sitaki kumsaliti naheshim ndoa yangu. Naombeni ushauri nifanyaje walau niongeze doz.

labda unampaka shombo tuu,na anakolezwa kwa wengine..jitaidi siku uwajibike ipasavyo kila siku atakua anaomba huyo.....dunia yako chaguo lako chagua kuacha uvivu,chagua kua mbunifu, na hakikisha umeipata Gspot ya mkeo....
 
mkuu ndio maana mwanaume kuwa na mke mmoja ni ngumu,tafuta kidumu mkuu utakufa kwa presha bure!
 
Habari zenu wana jf, nimeoa na nina miaka 4 ya ndoa yangu, kadri siku zinavyokwenda napunguziwa dozi ya mapenz, zilizopita ilikuwa 5 mpaka 6 per month sasa hivi ni 1per month na anakua mkali yaani mpaka nibembeleze kama naomba employment ukipewa unaambiwa utapata tarehe kama hi next month nampenda sitaki kumsaliti naheshim ndoa yangu. Naombeni ushauri nifanyaje walau niongeze doz.
hahaha,anataka gangster love huyo,
 
Kuna tatizo kubwa kwenyd ndoa yenu.Binadam akiwa hali chakula kama inavyotakiwa hupelekwa hosptl kwani ni lazima kutakua na tatizo.Na mke wako atakua na matatizo.Kama ham yake iko chini aeleze mtafute solution,kama hataki kuna tatizo ambalo ni serious!
 
Hebu tafakari vizuri.........hiyo mara moja kwa mwezi huwa anaitoa tarehe za mshahara? Yaani mwisho wa mwezi
 
nachukizwa sana na hali hii.....na ninalaani kitendo hiki....mimi kama mwanamke ninakemea ukiukwaji wa haki za binadamu.....

Preta inatia matumaini kama hata nyie mnajua tunahaki zetu ambazo nyingi wenzio huwa wanatudhulumu tena kwa uonevu wa kukusudia tu nasi huwa tunabebeshwa misalaba isiyokuwa ya kwetu......lol
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom