Kupewa mara moja tu kwa mwezi...

Paul mathew

JF-Expert Member
Jan 20, 2012
275
60
Habari zenu wana jf,

Nimeoa na nina miaka 4 ya ndoa yangu, kadri siku zinavyokwenda napunguziwa dozi ya mapenzi, zilizopita ilikuwa 5 mpaka 6 per month sasa hivi ni 1per month na anakuwa mkali yaani mpaka nibembeleze kama naomba employment...

Ukipewa unaambiwa utapata tarehe kama hi next month nampenda sitaki kumsaliti naheshimu ndoa yangu.

Naombeni ushauri nifanyaje walau niongeze dozi
 
Kumlazimisha, watakwambia ni ubakaji. Eti pata ridhaa ya mwenzio. Unalo....kuwa makini usije ingia kwenye uzinzi
 
Pamoja ya kuwa kwamba ndoa ina mambo mengi ambayo yanatakiwa kufanyika,lakini tendo la ndoa kama jina lake lilivyo ni kiunganishi muhimu sana katika ndoa.

Siwezi kuwa na uhakika mkeo ana tatizo gani ambalo haliweki kwako wazi mpaka hali inafika hapo.

Mi ningekushauri ukae chini na mke wako, mueleze ni namna gani una mthamini na kumpenda na kwamba katu hufikirii kutoka nje ya ndoa yenu.

Mwambie aweke wazi ni kwanini hali imefika hapo, natumaini atakueleza.

Kama ukiona huridhiki na majibu unaweza ukaanza kufanya uchunguzi wa chini chini ili kubaini kama anatoka nje ya ndoa au ana affaair na mtu mwingine anayechukua nafasi yako.

Naomba kuwasilisha.
 
Mithali 14:1 Kila mwanamke aliye na hekima hujenga nyumba yake; bali aliye mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
1. Je, ninajenga nyumba yangu au naibomoa?
2. Je, ninawekeza kwenye ndoa yangu? Natumia uwezo wangu kuiboresha?
3. Je, naonyesha kumthamini na kumjali mume wangu?
4. Je, natumia nguvu zangu na uwezo wangu kwa ajili ya familia yangu?
5. Je, natengeneza mazingira kwa maneno na matendo yangu yakumfanya mume wangu afurahie na kupenda kuwa nyumbani?
6. Je, naridhika na kuihudumia familia yangu?
7. Je, hisia zangu na upendo wangu ni kwa ajili ya mume wangu au mtu mwingine? Je, muonekano wangu, maneno mazuri na ushawishi mwema ni kwa ajili ya mume wangu au watu wengine?
8. Je, natimiza mahitaji ya mume wangu?
9. Je, ni mwaminifu kwa mume wangu? Nina uhusiano wowote wa siri ambao sitaki mume wangu ajue?
10. Je, mume wangu yupo huru kuwa muwazi kabisa kwangu hata kunikosoa?
11. Je, ninaruhusu mawazo ambayo siyo safi kuwa ndani yangu kupitia redio, televisheni au vitabu?
12. Je, nimekuwa kimbilio na faraja kwa mwanaume ambaye ndoa yake ina matatizo?
13. Je, natafuta ushauri na faraja kutoka kwa mwanaume mwingine (mchungaji, kiongozi wa kanisa, mshauri, mfanyakazi mwenzangu) na sio mume wangu kwanza?
14. Je, ninauhusiano wa karibu zaidi na mwanaume mwingine kuliko nilivyo na mume wangu?
15. Je, nimekuwa mkali na mwenye maneno yasiyo ya upole au ni mwenye maneno mazuri na yenye upole na unyenyekevu?
16. Je, naonekanaa rahisi rahisi kwa wanaume wengine au naonekana ni mtu mwenye msimamo? Je, naruhusu mizaha isiyofaa na watu wengine?
17. Je, kuna kitu katika mavazi yangu, muonekano au maongezi ambacho kinaweza kuwa kichocheo kwa wanaume kuwa na tamaa?
18. Je, ninavyoongea na wanaume kazini au popote naonyesha kuwa mimi ni mwanamke wa kristo au nakuwa nawaonyesha upendo na ukaribu wa kupitilizia ambao unapaswa uonyeshwe na wake zao?
19. Je, nimeweka mipaka katika mahusiano yangu na watu wa jinsia ya kiume? Ni mipaka gani hiyo?
20. Je, kuna mausiano niliyonayo ambayo yanaweza kuleta utata kwa watu?
21. Je, mume wangu na watu wengine wanao nifahamu wanaweza kusema kuwa mimi ni mwanamke mwenye busara na anayejiheshimu?
22. Je, nimeazimia moyoni mwangu kuwa safi mbele za Mungu? Je, ni mfano wa kuigwa na wanawake wengine wanaoishi maisha ya kumfuata Mungu?
Mithali 31:10 Mke mwema, ni nani awezaye kumuona? Maana kima chake chapita kima cha marijani.
PRINT HII KARATASI MPELEKEE AJIBU MASWALI YOTE HAYO HAPO JUU TENA WEWE UKIMUULIZA MWENYEWE

 
Hebu na wewe mchunie tuone itakuaje ila pia labda una fujo sana uwanjani au sio mbunifu kila siku ni national anthem tu
 
Afya ya akili yako itaharibika punde.Fanya haraka ukae nae chini muone tatizo liko wapi.Akileta ubishi wewe mwanaume bwana hushikwi mkono kuvuka barabara.
 
Ongea nae mueleze kua hufurahi hiyo mara moja kwa mwezi,duh sijui niseme unabahati yani wengine kila nanihii anaitaka kila siku mpaka unajitia kazi ukimuona anaenda kulala siku yalikizo ni 7 kwenye mwezi mzima au asafiri..
 
Tusiwe wepesi wa ku-judge,ajaribu kuongea nae kwanza pengine kuna sababu.

Ennie...Nimetumia neno Possibly....sikufanya judgement.....nimempa assumption kama wanavyofanya wengine ili wakati wa kulifanyia kazi awe nazo...........Encarta Encyclopedia (2009) inafafanua neno hilo kama ifuatavyo....

pos·si·bly [póssəblee]
adverb
1. perhaps: likely, or maybe so, but not definitely so
2. as possibility: as something that is possible or may be realized a new park to include a pond and possibly a playground
3. suggests effort: used to indicate the magnitude of effort or difficulty They've done everything they possibly could.
4. adds emphasis: used to express shock, disbelief, or amazement What could he possibly mean?
How could you possibly have believed that?

5. suggests impossibility: used in negative sentences and phrases to emphasize that something cannot be done or cannot happen I couldn't possibly tell you.



 
Pole mkuu......kwa mnaosema amuulize mwenzake hebu wekeni maswali ya mfano tujue na rationale ya kila swali tafadhali

I am not expecting swali kama; mke wangu siku hizi mbona hupendi kufanya mapenzi na mimi.......as kama kuna tatizo kwa upande wa mke anatakiwa yeye kutafuta platform ya kuzungumzia hili as she knows better

Lizzy , Kipipi, Pretta, MJ 1, Kaunga, AshaDii, Erociuos......, Madame X (Li avatar????), Mwali, ........

I stand to be corrected ila kwanza maswali ya kuulizwa mke kama huyu incase mume anatafuta haki yake kama huyu, maana kwa sie waelekea kibla hapo tena sunna tu ya nusra ya pili ndo yaweza kuwa considered
 
Amekuzidi kipato huyo mkeo au ana kazi nzuri kuliko wewe? Amekuzidi kielimu mkuu?

Hapo hakuna penzi kabisa, hebu mchunguze upate source ya yeye kubadilika namna hiyo ni nini?
 
Huyo mwanamke angekuwa mke wangu ningeisha mrudisha kwao, bora nikae bila mke kuliko kukaa na mke kama huyo.
 
Pole kwa yote ndugu, ningekushauri kukaa chini na mwenzi wako na kuzungumza. Pengine ana tatizo dogo labda atahitaji kumwona daktari au mwamasaikolojia (psychologist), unaweza kuwa msaada mkubwa kwake baada ya kuzungumza. Yakishindikana hayo yote basi waweza kuchetuna ingawa ni ushauri mbaya. lol!
 
pole mwee ila talk to her yawezekana ana stress ongea nae vizuri ataingia kwenye line tu uwe mpole kiaina
 
Back
Top Bottom