Kupeleka watoto wachanga chekechea imekuwa kama fasheni

ha hahaa hakumbe umeliona na wewe hili .. sehemu ya kutembea mtoto kwenye school bus
hahahaha kuna mmoja hapa jirani yangu yeye amemkodishia Bodaboda inampeleka shule
ukikaa nyumbani unapaona shule pale wala hamna hata barabara ya kuvuka useme atashindwa kwenda mwenyewe
 
hahahaha kuna mmoja hapa jirani yangu yeye amemkodishia Bodaboda inampeleka shule
ukikaa nyumbani unapaona shule pale wala hamna hata barabara ya kuvuka useme atashindwa kwenda mwenyewe
ha hahahaha pesa inamuwasha mama
 
heh
Unaona ulivyo kilaza? Alafu unakua hapa unatoa povu eti kila dada wa nyumbani unaepata ni majanga! Wale ni binadamu pia siyo punda, sasa wewe unataka hata chakula alie jikoni tena baada ya ninyi kula alafu utake akufanyie kazi vizuri?

Ishi nae kama familia moja uone kama hatakaa hadi anaolewa akiwa hapo kwako.
mkuu pengine kabla hujaandika hili neno "kilaza" ungeuliza ni kwa nini nilimlamba makofi huyo binti. Kuna wakati inafikia inakubidi kuvuka mipaka ili kuweka sawa baadhi ya mambo ktk familia la sivyo utajalia.
Mwanafunzi bora huuliza swali kwanza mkuu:D:D
 
NILICHOGUNDUA HUMU ASILIMIA KUBWA HAWANA UELEWA
1.JUU YA NINI DAY CARE NA SHUGHULI ZAKE.
2.TOFAUTI KATI YA DAY CARE CENTRE NA NURSERY SCHOOL
ndio maana ubishi mwiingi mbele kiza
 
Mm mtoto wa pili na watatu wamelelewa na madada hawapungui 25 mpaka nilipoamua kuchukuwa mtoto wa wifi kutoka kijijini na kuamia kumsomesha huku Dar ndio amekuwa msaada mkubwa kwangu mpaka sasa huyu watatu ametimiza miaka 4.
Namshukuru Mungu kwa hilo. Tangu nimeanza kukaa na Beki tatu mwaka 1989 huyu niliyenaye ni wa 10 na yuko mwaka wa 4 sasa.
 
Namshukuru Mungu kwa hilo. Tangu nimeanza kukaa na Beki tatu mwaka 1989 huyu niliyenaye ni wa 10 na yuko mwaka wa 4 sasa.
Una watoto wangapi? Nyumba unayokaa ina ukubwa gani? Iko fenced au kuna muingiliano na majirani? What are your working hours?
 
Malezi ya watoto yanafanywa na mama tu. ..hao wasichana wa kazi mnawapa kazi isiyowahusu. ..kuwa bize na kutafuta pesa alafu unalelewa mtoto na house girl.

Akiharibika/zoba. ..unaanza lawama
 
Naweza kubali kwa upande fulani

Nina dada yangu mfanyakazi, yeye huwa anamtoa mdada wa kazi kijijini halafu kazi yake ni kulea mtoto tu ila kazi nyingine kama kufua nguo za mtoto na kupika anawambia wasifanye, yule dada akitoka kazini anazifanya yeye mwenyewe hata kama ni usiku, na anadumu na wadada wa kazi hata kwa miaka zaidi ya mitano.

Sasa wale wanawake ambao mko bize sana na kazi na mnarudi usiku sana, poleni kwa kweli
Dada yako ana bahati tuu, hawa ma housegirl hawaeleweki. Mimi kuna kipindi nilikuwa naamka saa kumi alfajiri napika uji na chakula cha mtoto cha siku ili yeye kazi yake ni kukipasha, kumlisha na kuhakikisha mtoto ni msafi.. Lakini alichokuwa anakifanya Mungu mwenyewe anajua. Chakula anamwaga, anamshindisha mtoto na juice. Working mothers tunapitia mitihani na hawa watu jamani.. kama mtu hajapata hiyo experience hawezi kuelewa.
 
sheria zinaweza kukinzana, lakini uhalisi unabaki palepale, mtoto huzaliwa na kunyonyeshwa na mama yake, hivyo mwenye malezi sahihi ya mtoto ni mama na si vinginevyo, ila nyie wanawake mnaojiita wa kisasa hamna lolote, ni majanga tu!!
kupika hamtaki, mnataka b3 apike.
kufua hamtaki, eti mtakatika kucha, kila kitu b3, ndiyo maana mnaibiwa waume zenu na ma b3
mkuu ukikuta mwana mama hapendi kupikapika HUYO HAJUI MAPISHI ! lakini mwana mama bingwa wa jiko hata achoke vipi ataingia jikoni!
 
Dada yako ana bahati tuu, hawa ma housegirl hawaeleweki. Mimi kuna kipindi nilikuwa naamka saa kumi alfajiri napika uji na chakula cha mtoto cha siku ili yeye kazi yake ni kukipasha, kumlisha na kuhakikisha mtoto ni msafi.. Lakini alichokuwa anakifanya Mungu mwenyewe anajua. Chakula anamwaga, anamshindisha mtoto na juice. Working mothers tunapitia mitihani na hawa watu jamani.. kama mtu hajapata hiyo experience hawezi kuelewa.
sema wewe mkuu labda uteleweka
 
Tatizo ni ubishoo wa wazazi na kujifanya busy for nothing, mzazi ana kucha ndefu kama jini na smart phone kubwa ataweza kukaa na mtoto kweli
 
Kelele nyingiii tuacheni na watoto wetu jamani, Mimi mwanangu ana miaka mi 2 na Shule nimemuanzisha, majukumu yanatubana ndio, huyu wa miaka mi 2 ana mdogo wake wa miezi 7 na bado nina majukumu ya kikazi , sasa mnataka tuwaachie Dada wa nyumbani watoto wote hawa? Ataweza? Bora aende Shule tu
jamani mfano huo hapo mtoto ana miaka 2 na mdogo wake miezi 7 sasa afanyaje lzm mkubwa aende shule ili dada abaki nyumbani mtoto wa miezi 7
 
mbaya Zaidi mtoto wa miaka miwili na yeye anapewa homework
HAO WANAENDESHA NURSERY SCHOOL SIO DAY CARE CENTRE MKUU.NINA ANDAA PROFESSIONAL DAY CARE CENTRE TAKUKARIBISHA UTEMBELEE UONE NA UJIFUNZE UBORA NA TOFAUTI YA DAY CARE NA NURSERY NA KWA JINSI GANI HAO WANAO WAPA HOME WORK WATOTO WA DAY CARE WANAVYO WAHARIBU VICHWA NA.MWISHO WA SIKU WATOTO HAO WANAVYOKUWA WAVIVU KITAALUMA
 
Najiuliza, huyu mtoto mzazi asipojishughulisha atakula nini?? Likizo inatambulika kuwa ni miezi 3 tu. Kazini, mama haruhusiwi kutoka toka tena mbaali. Kongowe na ofisi Posta Mpya. Kama mama ni golikipa, ni ushamba kumpeleka mtoto chekechea kabla ya 5yrs. Lakini kama ni mfanya kazi, apeleke huko day care.

Nadhani umefika wakati sasa hizo sehemu watu wanakofanyia kazi kuwa na day care center ili iwe rahisi kwa wazazi japo kuwatupia jicho watoto wao wanapokuwa kazini. kwa kweli kuwapeleka watoto wadogo kwenye hizo shule haipendezi lakini majukumu ndiyo hayo na asiye fanya kazi asile. Ila bado naomba zile boarding kwa watoto hawa bado sana jamani tuwe na huruma kidogo!
 
Kizazi tunachokitengeneza kwa sasa, tutegemee kuja kulia sana badae. Watoto wanajifunza tabia za ajabu wakiwa huko maday care ,na hii ni kwa sababu mzazi analazimisha mtoto ashinde hadi saa kumi jioni ndo amfate. Sasa mtoto wa miaka 2 atafundishwa nini masaa yote hayo tangu aaubuhi? Kinachotokea walimu wao wanawaacha watoto wacheze ama walale, hapo ndo wanapofundishana ushoga na mapenzi mana kuna vitoto vijanja huwa vinachungulia wazazi wao na kutaka kujaribu na wenzao. Hili swala athari zake ni za badae mtoto akikua ndo mzazi anastuka. Tukubali kuwa ni tatizo. Mimi mwanangu ataenda boarding akianza form one.
 
jamani mfano huo hapo mtoto ana miaka 2 na mdogo wake miezi 7 sasa afanyaje lzm mkubwa aende shule ili dada abaki nyumbani mtoto wa miezi 7
sio vya kucheka Mkuu watu wamekua ni mashuhuda na watabiri wa maisha ya watoto wa wenzao kama vile wao ni miungu
 
Back
Top Bottom