Kwa kweli Mungu awabariki wasanii na watu wengine jasiri katika kukemea kwa kupaza sauti juu ya uhuru ulipungua. Wakati huu watu tumekuwa waoga kukosoa yanayoendelea mfano kutokutolewa tamko vyeti feki vya watu kama DAB. au kwa kuwa ni wakubwa ndo wapo juu ya sheria? Wenye kuweza kutolea tamko wamekaa kimya ili mradi tu wanapata mkate wao wa kila siku lakini watu wa kada ya chini ndo wanaotumbuliwa kwa vyeti feki. Tunakoelekea ni hatari mno tusishabikie hali hii. Wasomi na wapenda ustaarabu wa demokrasia tuendelee kupaza sauti zetu juu ya uhuru unaopotea hadi kwenye majukwaa ya SIASA. Siasa na kazi ndo mpango mzima. Bila siasa ni ubabe tu no freedom. Tukikosa amani na kazi hazitaenda. Kila siku wafanyakazi tunaangalia tu vyombo vya habari na mitandao ya kijamii kufahamu nani kafanya nini au kafanywa nini badala ya kuelekeza mawazo yetu kwenye shughuli za kujenga taifa. Ni hatari sana kwa kweli. Tuache watu wawe huru mradi tu sheria haivunjwi. Mungu atubariki viongozi wetu watuongoze kwa misingi ya haki. Waliokuwa wababe na wapole wote njia yao ni ardhini tusifanye ya kuudhi wengine tukidhani hapa duniani ni pa kudumu.
ivi ukishajijua umbo lako likoje c unajitafutia na dress code isiyotia shaka uyu vip izo gym anafanyaga nini au anatengenezaga shape afanane na ...
Unaogopa nini kumalizia!!ivi ukishajijua umbo lako likoje c unajitafutia na dress code isiyotia shaka uyu vip izo gym anafanyaga nini au anatengenezaga shape afanane na ...
inasikitisha sana hii....Kwakuwa tu anapenda kuwa live kwenye media na mitandaoni basi yuko tayari kufanya lolote ili aendelee kusikika
NIPASHE NDIO LIMEOZA KABISAKweli kuna udhaifu mkubwa katika media za Tanzania.
Halafu waandishi wa habari ni waoga hawahoji kwa kuuliza maswali magumu ya msingi ili kuondoa ukakasi, wao waandishi kazi yao ''kunakili'' yale yanayotoka ktk meza kubwa neno kwa neno.
Angalau hapa Jamiiforums tunahoji masuala kwa kina waje wajifunze au kama wanaogopa basi waandishi waseme ''mitandao ya jamii inasema hivi, je wewe bwana mkubwa una nini la kusema juu ya hoja hii ilivutia maswali mengi katika mitandao ya jamii.
Mimi nilikuwa nanunua gazeti moja litokalo kila siku na nilikuwa nawaaminia ! Ila kwa Sasa nimegundua ile dhana ya kuhoji imewatoka hivyo nimewaacha kabisa na nikiangalia niwapo barabarani kwenye foleni ni wengi wamechukua uamuzi wangu ! Wasipojirekebisha watafunga biashara kwani siwezi kutoa buku langu kusoma masifio ! Huwa nilikuwa nahitaji habari mbadalabagamoyo tatizo ni bahasha na kutanguliza maslahi binafsi mbele! Ukionekana ni mjuaji sana unahoji sana mkutano mwingine huitwi ng'ooo