Kuolewa kwa kulazimisha

Kuolewa kwa kulazimisha

sijui maisha ya brenda na atoto lakini asikudanganye mtu kwamba ukiwa unajiweka mjini mwenyewe utaondoka kwenye uhusiano mgumu kirahisi. Watu wananaswa kwenye mahusiano magumu kwa sababu nyingi hasa za kisaikolojia. Unajikuta unamlewa mtu kaa teja kwa sababu labda za majeraha ya utotoni ambayo hata huyajui, au kwa sababu ya mahusiano mabaya ya wazazi, au kwa sababu umewahi kuwa kwenye uhusiano mbovu zaidi kwa hiyo unauona huo wa afadhali (yaani umezoea shida), au uko kwenye malipizi (karma) - huku kwenye dini yetu wanasema kupatilizwa maovu yako mwenyewe au ya wazazi n.k. Wengine wanajiona wa thamani ndogo (low self esteem) kwa hiyo wanaona sawa kufanyiwa ubaya, tena wanajiona wenye bahati kuwa na wenza husika; wengine hawana malengo kwa hiyo hawaoni shida kukaa kwenye uhusiano miaka hata 10 - wanaendeshwa na matukio tu; wengine wengi wana picha mbaya kuhusu mahusiano - wameshaamini hakuna mahusiano matamu hata akiona couple imeshikana mikono anaamini inaigiza tu ila maisha yao ya ndani ni kama yake n.k.

Nimecheka kama mazuri. 75% yalishawahi kunihusu ndo maana sitakaa nimzodoe mtu anayekaa kwenye mahusiano tasa miaka 2, 3, 5, 10 20.... Akae tu maana akija kufanikiwa kutoka atakuwa amekua sana na akitoa ushauri lazima ueleweke maana ni "first hand information". Ukiona mtu yuko kwenye uhusiano mgumu ukamhubiria mpaka akatoka ujue mchango wako ni mdogo sana - alikuwa ameshafikia kiwango kikubwa cha uelewa na kilichomtoa ni utashi wake. Ukiona mmemwambia lakini hasikii basi ujue dozi ya mateso haijatosha kumfanya afunguke na kuvuka kiwango cha ujinga alio nao ndo maana ana excuse kwa kila kituko anachofanyiwa.

Mlioko kwenye mahusiano sugu si kwamba hamjaambiwa. Mmeshaambiwa sana tena wengine kwa upofu wenu mnawasaliti watu wanaojaribu kuwafungua macho. Unaskia "baby eti rafiki yako fulani ameniambia wewe ni malaya sana, huna fyucha na mimi...unanichuna tu..."!! Ukija kufunguka macho na kuona kila kitu kama kilivyo ndo unaanza kuwakumbuka mitume na manabii wote uliowafukuza na kuwasaliti. Ndo maisha. Unafanya mtihani, unafeli, unasapu, unafeli au unafaulu..ukikata tamaa unadisko halafu unaanza kusema "wanawake/wanaume wabaya!!!" kumbe we ndo tatizo. Kwenye maisha huwezi kuchagua maswali ila unaweza kuchagua kufaulu au kufeli. Nshaanza lekcha sikumbuki hata pointi ilikuwa nini.

hata wanaume wabaki wawili duniani kuna aina za wanaume hatutakaa tuwachukue. Acha tusome namba huku huku nje kuliko kuzisomea vyumbani. Kwani maisha ni nini hata umgande mwanaume kama luba kama mwili, akili na roho havijakupa go ahead? Pamoja na wingi wetu wanawake wanawake wanaofaa kuolewa nao ni scarce kwa hiyo hata wanaume wanapata shida kupata wenza wazuri. Usifikiri mambo ya mahusiano ni magumu kwa jinsi moja na marahisi kwa jinsi moja. Kama kuoa ni rahisi wanaume wote "eligible" kwa umri na hadhi wangeshaoa.

Ukiona mume anaibiwa (sijui ni baiskeli??) basi ujue hakujiandaa kwa ndoa na si sababu ya competition. Hao waume waliotulia unataka kusema wana wake wakamilifu au competition hawaioni au hawana viwango vinavyotosheleza mahitaji ya soko hili lenye ushindani??


too smart my teacher......
 
Nakubaliana na sentensi yako ya mwisho. Kusema wanawake independent wako choosy ni swala zima la "perceived power relations" na mambo mengine. Kiatu usichokivaa usikitolee maoni (ushajieleza kwenye mabano). Kwamba unaweza kuzeeka ukiwa mseja, ndiyo inawezekana na mimi nimeshaona wengi tu akiwemo bibi wa miaka 80 na kitu hajawahi kuolewa wala kuzaa, ni tajiri, ameajiri dereva na watoto wa ndugu zake ndo wanamtunza nyumbani na kumwangalizia nyumba zake. Nimeshaona pia wababa watu wazima wakiwa na watoto wao wa ujanani tu au ndugu zao. Huwaoni kwa sababu hauishi kwenye huo ulimwengu.
 
Nakubaliana na sentensi yako ya mwisho. Kusema wanawake independent wako choosy ni swala zima la "perceived power relations" na mambo mengine. Kiatu usichokivaa usikitolee maoni (ushajieleza kwenye mabano). Kwamba unaweza kuzeeka ukiwa mseja, ndiyo inawezekana na mimi nimeshaona wengi tu akiwemo bibi wa miaka 80 na kitu hajawahi kuolewa wala kuzaa, ni tajiri, ameajiri dereva na watoto wa ndugu zake ndo wanamtunza nyumbani na kumwangalizia nyumba zake. Nimeshaona pia wababa watu wazima wakiwa na watoto wao wa ujanani tu au ndugu zao. Huwaoni kwa sababu hauishi kwenye huo ulimwengu.

Thanks nimekupata vizuri kwa kweli......ila we bana una akili nyingi, hope kidogo zingepitliza, loh!!

Halafu hii point kumbe ulikuwa umeishaimention somewhere nilikuwa sijaisoma, but am glad we said the same!! "Pamoja na wingi wetu wanawake wanawake wanaofaa kuolewa nao ni scarce kwa hiyo hata wanaume wanapata shida kupata wenza wazuri"
 
Mjeuri huyu unadhani hamjui "Mr right".

Mmh at your own risk, nenepeana tu na huo ureject uone nani atakukubali

Mr right si ni mr mmwaga midolari eti eeh??
We siku ile si ulinipa moyo ukaniambia kila mtu na mtuwe? Mbona leo tena wanigeuka!! Au wangu mie alishazolewa na sunami?
 
Mr right si ni mr mmwaga midolari eti eeh??
We siku ile si ulinipa moyo ukaniambia kila mtu na mtuwe? Mbona leo tena wanigeuka!! Au wangu mie alishazolewa na sunami?
Sasa si kila mtu ana definition yake ya "Mr right", wewe kwako ni yule pedeshee muuza mawese na kati ya bima teh

Eeh usijali kila mtu na mtuwe, utampata reject mwenzio muharibu vizuri watoto
 
Thanks nimekupata vizuri kwa kweli......ila we bana una akili nyingi, hope kidogo zingepitliza, loh!!

Halafu hii point kumbe ulikuwa umeishaimention somewhere nilikuwa sijaisoma, but am glad we said the same!! "Pamoja na wingi wetu wanawake wanawake wanaofaa kuolewa nao ni scarce kwa hiyo hata wanaume wanapata shida kupata wenza wazuri"
kuna mtu nimemwambia akili nyingi ni tatizo hata hajanielewa au mimi sijamuelewa lakini nimemuomba radhi. Ulale salama. Jumatano inakaribia.
 
Sasa si kila mtu ana definition yake ya "Mr right", wewe kwako ni yule pedeshee muuza mawese na kati ya bima teh

Eeh usijali kila mtu na mtuwe, utampata reject mwenzio muharibu vizuri watoto

Tooooba!! Km ndio hivyo acha nitafute dawa, alafu nikazane na mazoezi, hivi hakuna mazoezi ya kutengeneza kichwa na gusura?
 
Tooooba!! Km ndio hivyo acha nitafute dawa, alafu nikazane na mazoezi, hivi hakuna mazoezi ya kutengeneza kichwa na gusura?
Wale hawajali sana sura na guchogo. Maintain tu mwili , ublack + kipilipili basiiii
 
Kabisa best, ni heri nipate kimojawapo kuliko nikose vyote, yaani jehanamu naianzia duniani!!!😕 hapana kwakweli.

Hahahaa nanii hapendi vizuri....
Ila hapa wataturukia weee chezea wanaume wa jf
 
Watu wengi are in such denial of the state of their relationships... Na si wanawake tu.... Wanaume wangapi wameishia kuwa walevi kisa mwanamke. .. ....

Mtu anaona dalili lakini anategemea ataonewa huruma.... Au mwenzake atabadilika .. Mwingine haoni kabisaa... Atatafuta kila sababu......

Nisipomtafuta hanitafuti.... He's just busy.

Kila kitu anakasirika tu na hanijali kabisa.........ana stress tu za kazi

Nisipopanga mimi tukutane hafikirii kabisaa.......anachoka sana so kila akipata muda anataka apumzike

Hajawahi kunihakikishia future ya uhusiano... ........anajifikiria /Ananichunguza

Aliniambia sifai kuwa na mtu kama yeye...... Ana insecurities

Naona yuko na mimi kwa sababu tu yuko lonely, japata anayemtaka......... Atanipenda tu

Ananipiga /ananitukana,..... Ndo kalelewa hivyo lakini ananipenda

Hapo alipo Kuna mtu akimwambia tuoane, ataenda kumgongea pastor usiku wafungishe ndoa. Hujui tu

Jithamini.
Jipende.
Jijali.
Kama ambavyo wewe Kuna mtu anakutafuta juu chini lakini huna habari na hutaki kabisa, muelewe mwenzako.
Wewe si wa kwanza kupenda usipopendwa. Utampta mtakayependana.

Word my sis..umesema yote
 
sijui maisha ya brenda na atoto lakini asikudanganye mtu kwamba ukiwa unajiweka mjini mwenyewe utaondoka kwenye uhusiano mgumu kirahisi. Watu wananaswa kwenye mahusiano magumu kwa sababu nyingi hasa za kisaikolojia. Unajikuta unamlewa mtu kaa teja kwa sababu labda za majeraha ya utotoni ambayo hata huyajui, au kwa sababu ya mahusiano mabaya ya wazazi, au kwa sababu umewahi kuwa kwenye uhusiano mbovu zaidi kwa hiyo unauona huo wa afadhali (yaani umezoea shida), au uko kwenye malipizi (karma) - huku kwenye dini yetu wanasema kupatilizwa maovu yako mwenyewe au ya wazazi n.k. Wengine wanajiona wa thamani ndogo (low self esteem) kwa hiyo wanaona sawa kufanyiwa ubaya, tena wanajiona wenye bahati kuwa na wenza husika; wengine hawana malengo kwa hiyo hawaoni shida kukaa kwenye uhusiano miaka hata 10 - wanaendeshwa na matukio tu; wengine wengi wana picha mbaya kuhusu mahusiano - wameshaamini hakuna mahusiano matamu hata akiona couple imeshikana mikono anaamini inaigiza tu ila maisha yao ya ndani ni kama yake n.k.

Hawana malengo nakubaliana na wewe, kujitambua pia na kujithamini....wapo na elimu zao lakini nao pia ni hayo hayo nashindwa kuelewa kwanini wanawake hatujiamini...
 
Kama umesoma economics, wanasema money is scarcity resource, hali imekuwa hivyo hivyo kwa wanaume,wanaume tumekuwa adimu siku hizi hasa waoaji, hivyo unapompata mwanaume inatakiwa umgande kama luba a.k.a kupe mengine yanakuja mbeleni, lasivyo utaisoma namba mwaka wenyewe ndo unayoyoma huu, compitition ni kubwa mno kuliko mnavyofikiria ladies, ndio maana siku hizi hawa waume za watu wanaibiwa kwakuwa wake zao wanajisahau baada ya kuvishwa pete,

Hako kamsemo sikapendi kweli,mnajipa kichwa mmekua adimu,na wanawake tunachanganyikiwa kweli...kama yupo yupo tu sio kujishikiza kwenye relationship isioeleweka sababu tu wanaume ni adimu
 
Back
Top Bottom