Kuna watu wengine wanavifuata hivi vyama vya upinzani kishabiki

Kuna watu wengine wanavifuata hivi vyama vya upinzani kishabiki

Mwishokambi

JF-Expert Member
Joined
Nov 23, 2020
Posts
473
Reaction score
1,682
Nimefuatilia sana kwanini baadhi ya wananchi wakiwemo viongozi wa dini wanapendwa sana na wananchi, kwa mfano Askofu Bagona anayefanana kichwa na msanii Mwijaku amekuwa akiisema sana vibaya serikali kwa kisingizo cha uhuru wa kutoa maoni, kauli zake zinatumiwa sana na wapinzani wa serikali.

Father Kitima ambaye ni msuluhishi wa migogoro ya kiuongozi ndani ya Chadema anaonekana wa maana sana kwa wapinzani wa serikali kutokana na kauli zake za kuisema vibaya serikali bila logic yoyote.
Wako wengi, akina Mdude Nyagali, sijui Sativa na wengine ambao wanaikashifu serikali wanaonekana watu wa maanaaaa mbele ya wananchi kuliko viongozi wa serikali.

Mwingine ni huyu kiongozi wa chama cha wanasheria, Boniface Mwabukusi, yeye ni mfuasi wa Chadema na wala hajifichi na ameshinda urais wa chama hicho chenye mwelekeo wa kisiasa kwa sababu tu ya kuipinga serikali.

Mwabukusi, anapoongea hajulikani kama anachoongea ni msimamo wa chama anachokiongoza ama maoni yake binafsi.
Kwa mfano leo amenukunuliwa kwenye page yake ya X akiponda wanasheria walioandika kanuni za maadili kuwa hajui wamesomea chuo gani.

Wewe Mwabukusi unajiona umesoma saana wakati kila mtu anajua elimu yako ya kuunga unga, wewe mwenyewe umewahi kuhojiwa na chuo kimoja cha pale Biafra Kinondon ukisema kuwa ulikuwa dereva wa mabasi, ukasoma kwa kujiunga unga hadi umemaliza, sasa wewe unaiona una akili sana kuliko mawakili wa serikali.
Kama wewe msomi sana tukuone basi pale Kisutu ukapangue kesi ya uhaini ambayo inamkabili mwenzake na ukishindwa anakwenda kuhukumiwa kifo.

Ni ujinga tu, wananchi wengi wanaounga mkono vyama hivi vya kisiasa vya upinzani wanafanya hivyo kwa ushabiki tu.
Ukimuuliza kwanini unashabikia Chadema, jibu Lissu ni mpinzani wa kweli, kafanya nini, hana hoja, huyo huyo kwenye kata yake kuna vituo vya afya, zahanati, maji, pembejeo, mikopo kutoka maendeleo ya jamii, amani na usalama lakini anapinga serikali.

Ukiwa mtu wa kubet lazima upinge serikali, sasa chama hakitaki kwenda kusaini maadili unakilazimishaje kushiriki kwenye uchaguzi.
Mnataka kutuaminisha uongo kuwa Lissu ndio atakuja kubadilisha maisha ya wananchi, dunia hii ambayo Trump kila kukicha anaongeza trade barriers kwa washindani wake wa kibiashara huku nchi za kiafrika zikiumia, migogoro ya kisiasa inavyotuharibia uchumi ndio Lissu akatuletee maisha bora.

Au mnataka Lissu awe Rais ili Mdude awe Mkuu wa Wilaya, Yericko awe Katibu Mkuu wa Wizara, acheni utani nyie.
 
Bw.Mwabukusi amekuwa mwepesi sana kukosoa serikali na kuongea maneno ya kijinga kuliko hata anavyoiongelea Chadema, anaogopa kuikosoa Chadema kwa sababu watanzania ambao wanafurahi serikali ikitukanwa au mawakili waliomchagua watamuona msaliti.
Tangu aingie kwenye uongozi wa chama hicho amekuwa akitumia muda mwingi kukosoa serikali kuliko hata kukosoa mambo yanayofanywa na chama cha Chadema ambacho yeye anakishabikia.
Huu kwangu nauita undezi uliopitiliza, wewe ukiamka tu asubuhi ukiona serikali imefanya jambo fulani unatokea kwenye page yako unapinga, lakini katika page yako huonekani kuwaeleza ukweli wala kuwashauri chadema.
Wewe kama mwanasheria unaona sawa kwa Chadema kukataa kwenda kwenye mkutano wa kusaini kanuni za maadili?
Wewe unaona sawa kweli kiongozi anakiri hadharani kuwa atafanya uasi, halafu unasema uhaini hauwezi kufanywa kwa maneno tu? Ina maana uhaini unatokea ghafla tu, uhaini hauna mipango wala vikao.
Umesahau Genocide ya Rwanda, kalamu ya waandishi tu ilipelekea watu zaidi ya 900,000 kupoteza maisha.
Mtu anaposema jukwaani kuwa tutazuia uchaguzi kwa kuhamasisha maandamano barabarani hiyo haiwezi kuwa kosa kwa sababu ni jambo la kisiasa, je wakihamasika kweli wananchi na kwenda barabarani? We hujawahi kumuona Mchungaji Mtikila akihamasisha wananchi jukwaani wananchi wakaenda kuwavamia wahindi? Ulikuwa mshamba mshamba kipindi hicho hata makinda ya ndege mdomoni hayajakutoka.
Tumia muda wako mwingi kushauri Chadema hata kama watakuchukia, that is leadership sio wewe kazi yako kuponda tu serikali ili wananchi wakuone wewe mwamba kumbe unaonekana mshamba tu.
 
Nimefuatilia sana kwanini baadhi ya wananchi wakiwemo viongozi wa dini wanapendwa sana na wananchi, kwa mfano Askofu Bagona anayefanana kichwa na msanii Mwijaku amekuwa akiisema sana vibaya serikali kwa kisingizo cha uhuru wa kutoa maoni, kauli zake zinatumiwa sana na wapinzani wa serikali.

Father Kitima ambaye ni msuluhishi wa migogoro ya kiuongozi ndani ya Chadema anaonekana wa maana sana kwa wapinzani wa serikali kutokana na kauli zake za kuisema vibaya serikali bila logic yoyote.
Wako wengi, akina Mdude Nyagali, sijui Sativa na wengine ambao wanaikashifu serikali wanaonekana watu wa maanaaaa mbele ya wananchi kuliko viongozi wa serikali.

Mwingine ni huyu kiongozi wa chama cha wanasheria, Boniface Mwabukusi, yeye ni mfuasi wa Chadema na wala hajifichi na ameshinda urais wa chama hicho chenye mwelekeo wa kisiasa kwa sababu tu ya kuipinga serikali.

Mwabukusi, anapoongea hajulikani kama anachoongea ni msimamo wa chama anachokiongoza ama maoni yake binafsi.
Kwa mfano leo amenukunuliwa kwenye page yake ya X akiponda wanasheria walioandika kanuni za maadili kuwa hajui wamesomea chuo gani.

Wewe Mwabukusi unajiona umesoma saana wakati kila mtu anajua elimu yako ya kuunga unga, wewe mwenyewe umewahi kuhojiwa na chuo kimoja cha pale Biafra Kinondon ukisema kuwa ulikuwa dereva wa mabasi, ukasoma kwa kujiunga unga hadi umemaliza, sasa wewe unaiona una akili sana kuliko mawakili wa serikali.
Kama wewe msomi sana tukuone basi pale Kisutu ukapangue kesi ya uhaini ambayo inamkabili mwenzake na ukishindwa anakwenda kuhukumiwa kifo.

Ni ujinga tu, wananchi wengi wanaounga mkono vyama hivi vya kisiasa vya upinzani wanafanya hivyo kwa ushabiki tu.
Ukimuuliza kwanini unashabikia Chadema, jibu Lissu ni mpinzani wa kweli, kafanya nini, hana hoja, huyo huyo kwenye kata yake kuna vituo vya afya, zahanati, maji, pembejeo, mikopo kutoka maendeleo ya jamii, amani na usalama lakini anapinga serikali.

Ukiwa mtu wa kubet lazima upinge serikali, sasa chama hakitaki kwenda kusaini maadili unakilazimishaje kushiriki kwenye uchaguzi.
Mnataka kutuaminisha uongo kuwa Lissu ndio atakuja kubadilisha maisha ya wananchi, dunia hii ambayo Trump kila kukicha anaongeza trade barriers kwa washindani wake wa kibiashara huku nchi za kiafrika zikiumia, migogoro ya kisiasa inavyotuharibia uchumi ndio Lissu akatuletee maisha bora.

Au mnataka Lissu awe Rais ili Mdude awe Mkuu wa Wilaya, Yericko awe Katibu Mkuu wa Wizara, acheni utani nyie.
CCM ina uhalali upi wa kuongoza serikali labda kwa Akili yako.Yawezekana tunajadili na watu wasiofuatilia chaguzi nchi hii.
 
Back
Top Bottom