Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 16,817
- 62,027
Nataka nitoe disclaimer kuwa siungi mkono mapinduzi ya kijeshi kama namna ya kufikia malengo ya kisiasa.
Hata hivyo mimi kama mwanajamii ambaye naishi ndani ya jamii, nina wajibu wa kuchangia maoni na kuonya ikibidi pindi ninapoona muelekeo hatari kwa mustakbali wa Taifa.
Ni hivi, nimesoma mitandao mingi ya jamii na kusoma sentiment za wananchi kuhusiana na nchi yao nimeshtushwa kuona mambo ya fuatayo
1. Wananchi wengi wanaocomment kuhusiana na mambo ya Jeshi la wananchi, wanaonekana kupoteza imani na jeshi hilo au kulidharau, wengi wanalilaumu kuwa halikufanya ipasavyo kuzuia mauaji ya wananchi wengi october 29, na wanaliona limekaa kulinda masilahi ya kisiasa ya CCM kuliko nchi na katiba yake.
2. Wananchi wanaocomment kuhusiana na kundi la uasi liitwalo TFF wameonekana kuwa na huruma na kundi hilo, kuunga mkono malengo yake na wengine kuonyesha hata shauku ya kujiunga na kundi hilo.
Kwa namna yoyote viashiria hivi siyo vyema, ni hatari mno kwa mustakbali wa Taifa. Ni lazima serikali na baraza la Taifa la usalama vikae chini na vione ni namna gani vinaondoa matishio haya.
Mimi kwa maoni yangu ni kuwa:
1. Matendo ya utekaji na kuuawa wananchi yasiyokoma, yamewapotezea wananchi imani kwa serokali, na wengi wanaona inahusika. Lakini pia yamewaondolea wananchi imani kwa vyombo vya usalama, maana haya mambo yamegeuka ni desturi ktk nchi yetu.
2. Kutoheshimu katiba hasa haki ya wananchi ya kuchagua na kuchaguliwa. Sasa hivi nchini, hakuna uchaguzi wa haki, siyo kuanzia kwa serikali za mitaa mpaka rais. Kote huko ni magumashi matupu. Hii inawafanya wananchi waone kuwa utawala ulioko madarakani si wao, na hata unapoamrisha majeshi wanayaona majeshi kama washirika wa utawala usio wa wananchi. Kwa hiyo ni lazima kama taifa tukubaliane, Je huko mbeleni tunataka utawala wa demokrasia kweli au tunataka kundi dogo ndo lituchagulie viongozi.
3. Ufisadi na upigaji uliokithiri, huku mafisadi papa wakipeta wakati wananchi wakihaha kupata japo pesa za kujikimu. Wananchi wanaona ufisadi ukitamalaki, hatusikii mtu kufikishwa mahakamani kwa sababu ya rushwa, au kusimamishwa kupisha uchunguzi wa ubadhirifu. Imekuwa ni suala la kabadilishana vyeo tu, mteue huyu, mtengue yule basi. Hii kitu imezidisha chuki na hasira kwa wananchi.
4. Tatizo la ajira.
Watu wengi hasa vijana wana tatizo hili, hii pia inatengeneza pool ya watu ambao ni rahisi kusajiliwa (recruited) kujiunga na vikundi hatari. Ipo haja ya serikali kuweka mkazo sana kwenye kuwezesha wananchi kuliko kujali kukusanya mapato peke yake. Tatizo la ajira kwa vijana ni bomu linalosubiri kupasuka.
4. Lazima mageuzi (reforms) ya kisiasa na kiuchumi yafanyike nchini. Nchi imevimba sana hii, lolote linaloweza kuchochea uasi wa silaha lazima lishughulikiwe kwa njia stahiki. Mahakama iachwe huru itende haki, isifanye kazi kwa vimemo au simu, vyombo vya uthibiti navyo visitumike kama fimbo ya kuonea watu au taasisi zao.
Hivi viashiria vya wananchi kuanza kuzungumza kuunga mkono njia za nguvu ni kitu hatari mno. Tukae chini kama Taifa tusolve hii kitu la sivyo tuendako ni kubaya mno.
Hata hivyo mimi kama mwanajamii ambaye naishi ndani ya jamii, nina wajibu wa kuchangia maoni na kuonya ikibidi pindi ninapoona muelekeo hatari kwa mustakbali wa Taifa.
Ni hivi, nimesoma mitandao mingi ya jamii na kusoma sentiment za wananchi kuhusiana na nchi yao nimeshtushwa kuona mambo ya fuatayo
1. Wananchi wengi wanaocomment kuhusiana na mambo ya Jeshi la wananchi, wanaonekana kupoteza imani na jeshi hilo au kulidharau, wengi wanalilaumu kuwa halikufanya ipasavyo kuzuia mauaji ya wananchi wengi october 29, na wanaliona limekaa kulinda masilahi ya kisiasa ya CCM kuliko nchi na katiba yake.
2. Wananchi wanaocomment kuhusiana na kundi la uasi liitwalo TFF wameonekana kuwa na huruma na kundi hilo, kuunga mkono malengo yake na wengine kuonyesha hata shauku ya kujiunga na kundi hilo.
Kwa namna yoyote viashiria hivi siyo vyema, ni hatari mno kwa mustakbali wa Taifa. Ni lazima serikali na baraza la Taifa la usalama vikae chini na vione ni namna gani vinaondoa matishio haya.
Mimi kwa maoni yangu ni kuwa:
1. Matendo ya utekaji na kuuawa wananchi yasiyokoma, yamewapotezea wananchi imani kwa serokali, na wengi wanaona inahusika. Lakini pia yamewaondolea wananchi imani kwa vyombo vya usalama, maana haya mambo yamegeuka ni desturi ktk nchi yetu.
2. Kutoheshimu katiba hasa haki ya wananchi ya kuchagua na kuchaguliwa. Sasa hivi nchini, hakuna uchaguzi wa haki, siyo kuanzia kwa serikali za mitaa mpaka rais. Kote huko ni magumashi matupu. Hii inawafanya wananchi waone kuwa utawala ulioko madarakani si wao, na hata unapoamrisha majeshi wanayaona majeshi kama washirika wa utawala usio wa wananchi. Kwa hiyo ni lazima kama taifa tukubaliane, Je huko mbeleni tunataka utawala wa demokrasia kweli au tunataka kundi dogo ndo lituchagulie viongozi.
3. Ufisadi na upigaji uliokithiri, huku mafisadi papa wakipeta wakati wananchi wakihaha kupata japo pesa za kujikimu. Wananchi wanaona ufisadi ukitamalaki, hatusikii mtu kufikishwa mahakamani kwa sababu ya rushwa, au kusimamishwa kupisha uchunguzi wa ubadhirifu. Imekuwa ni suala la kabadilishana vyeo tu, mteue huyu, mtengue yule basi. Hii kitu imezidisha chuki na hasira kwa wananchi.
4. Tatizo la ajira.
Watu wengi hasa vijana wana tatizo hili, hii pia inatengeneza pool ya watu ambao ni rahisi kusajiliwa (recruited) kujiunga na vikundi hatari. Ipo haja ya serikali kuweka mkazo sana kwenye kuwezesha wananchi kuliko kujali kukusanya mapato peke yake. Tatizo la ajira kwa vijana ni bomu linalosubiri kupasuka.
4. Lazima mageuzi (reforms) ya kisiasa na kiuchumi yafanyike nchini. Nchi imevimba sana hii, lolote linaloweza kuchochea uasi wa silaha lazima lishughulikiwe kwa njia stahiki. Mahakama iachwe huru itende haki, isifanye kazi kwa vimemo au simu, vyombo vya uthibiti navyo visitumike kama fimbo ya kuonea watu au taasisi zao.
Hivi viashiria vya wananchi kuanza kuzungumza kuunga mkono njia za nguvu ni kitu hatari mno. Tukae chini kama Taifa tusolve hii kitu la sivyo tuendako ni kubaya mno.
