Usishindane na watu dogo, waweza kuta wamefanikiwa yote haya wakiwa wadogo na kupoteza vyote, kutangulia sio kufika, wewe nenda na kasi yako, soma vya kutosha, piga kazi sana, hapa hapa bongo waweza kupiga kazi 2 kwa siku, moja mpaka jioni, jioni waingia tena sehemu nyingine, iwe kufundisha au technical, mishe mishe itakupeleka pabaya kwanza adhabu yake kubwa na ule uoga wa kukamatwa utakufanya usifaidi kabisa hela yako, utafanikiwa tu, kila mtu anayo riziki yake duniani, swala ni lini, ila bidii kwa kila kitu ufanyacho, hata iwe bustani, kuku, ofisi, kufundisha, yaani chochote kile wewe fanya kwa umakini na nenda mbele zaidi ya wenzako, hata wakuone unajipendekeza poa tu, una maana yako, hii ndiyo siri ya ushindi..