Nimeanzisha thread hii ili kumjibu mdau mmoja aliyeuliza hilo swali hasa baada ya kujiona yeye hana kitu na umri unasonga wakati vijana wenzake wana mafanikio. Nitajibu swali hili kwa namna mbili, moja ni mfumo rasmi na pili sio mfumo rasmi.
MFUMO RASMI
Darasa la kwanza miaka 7, darasa la saba 12, kidato cha nne 16, kidato cha sita 18, toa miezi ya kusubiria matokeo ya kidato cha nne na cha sita kama miezi 10 hivi, kwahiyo first year ataanza na 20 na degree ya miaka 3 atamaliza na 23. Hapa kuna mwaka mzima wa kusubiri cheti kitoke chuo maana huwezi kuajiriwa serikalini kwa kutumia transcript ya matokeo bila cheti. kwahiyo kazi ataanza na 25 yrs.
Mshahara wa serikalini kwa degree ya miaka mitatu ni TGS D1= 710,000/= au kwa walimu ni TGTS D1= 716000/= baada ya makato atabakiwa kama na 560,000/= huyo hakatwi na bodi ya mkopo. (mishahara haihusu taasisi na mashirika ya umma wala kada ya afya).
Tuseme huyu kijana wa 25yrs hana mke wala familia inayomtegemea, pia hanywi pombe wala hahongi wanawake na kwenda kazini anatumia gari moja tu na pia amepanga chumba kimoja tu na ajibane kwenye kula chai 1000, mchana 2000 na usiku 2000. kula kwa siku 5000 kwa mwezi 150000/=, nauli kwa siku 800 kwa siku 20 ni 16000/=, chumba kwa mwezi 50000(bei ya Dar), umeme kwa mwezi 15000/=, maji 10000/=, sabuni, mafuta, dawa ya meno 10000/=.
Jumla ya matumizi ni laki 2.5 ukitoa kwenye take home inabaki laki 3. inamaana akiishi maisha niliyosema hapo juu ana uwezo wa kusave laki 3 kila mwezi ambapo kwa mwaka ni 3.6 mill.
Kutoka 25yrs hadi 30yrs ni miaka 5. Kwahiyo 5yrs atakuwa na 18 mill.
Anunue gari kwa mtu 7 mill atabakiwa na 11 mill. Je 11 mill inatosha kwa kiwanja na nyumba ?
Jibu haiwezekani.
NB: Hapo nimechukulia huyo mtumishi hajanunua nguo mpya wala kitanda wala tv, redio na pasi kwa kipindi chote cha miaka 5.
MFUMO USIO RASMI
Hapa kila kitu kinawezekana mtu anaweza kutoka la saba au kidato cha nne akalima nyanya au miti ya mbao huko mafinga na kama mambo yakienda vizuri misimu miwili tu akamiliki vyote hivyo hata kabla ya 25yrs.
Nawasilisha.